Tafsiri
Mamlaka kwa mikoa ni dhana ambayohaina tofauti na dhana ya kisiasa ya madaraka mikoani. Mamlaka mkoani ni kuuachia mkoa fursa ya kuchagua viongozi wake; mkoa kulinda wakazi wake na rasilimali zao; kuwa na chombo chake cha kutunga sheria na kuwa na mkoa kuwa na mikakati na mipango yake ya kujiendeleza kijamii, kiuchumi, kiutamaduni , kisiasa na kiteknolojia.
Sababu kubwa ya kuwepo kwa haja ya mikoa inayojitawala angalau kiuchumi na kijamii ni kurudisha kwa mujibu wa katiba madaraka na mamlaka kwa wananchi pale walipo. Kihistoria, serikali kuu kwa sababu moja au nyingine ililazimika kuhodhi madaraka na mamlaka hata yale ambayo haikustahili kuwa nayo.
Enzi hizo uadilifu, uaminifu na utiifu kwa uongozi uliopo ulikuwa wa kiwango cha juu zaidi kuliko ilivyo hivi sasa. Mawasiliano, udhibiti na uwajibikaji, hali kadhalika, ni kitu kilichowezekana na kilichokuwa kikifanyika.
Katika miaka hii mikoa imeanza kuwa na mashaka na maamuzi ya wale wanaoongoza serikali kuu na hasa katika masuala ya ardhi, madini na uwekezaji. Wakati wakazi wa maeneo na mikoa husika wamekuwa hawaambulii chochote cha maana, viongozi wa wizara na serikali kuu wamekuwa wakifaidika na mali asili zilizoko katika mikoa ambayo wao hawakuzaliwa huko. Wazawa na wakazi wa mikoa husika wanaona kwa hiyo ipo haja ya kuweka utaratibu na muundo wa serikali utakaohakikisha kuwa rasilimali za mkoa zinafaidiwa na wakazi wake na sio kinyume cha hivyo.
Viongozi wote wa mkoa waliopo hivi sasa wanaonekana kuwajibika kwa serikali kuu na sio wakazi wa mkoa wahusika. Viongozi hawa wamekuwa kama ndio wenye mamlaka na madaraka na wananchi kuwa wasio na nguvu au uwezo wowote juu ya maisha na mustakabali wao kiuchumi na kijamii.
Mathalani, mkuu wa mkoa, awe mtu mbaya au mzuri, hachaguliwi na wananchi wa mkoa husika bali na rais. Wakazi mikoani wanaamini kwamba wakati umefika sasa kwa wao kumchagua mkuu wao wa mkoa kama wanavyochagua wabunge wao. Wanaamini hili litawafanya viongozi wa mkoa kuwajibika zaidi.
Wanataka pia serikali itambue hili na kumpa uwezo kiongozi watakaomchagua wao wenyewe. Badala ya mkuu wa mkoa wa sasa wanaamini kwamba mkoa unastahili kuwa na Waziri Mkuu wa Mkoa au Gavana wa mkoa.
Gavana huyo atapatikana ndani au nje ya bunge la mkoa, kutegemeana na upatikanaji wa mtu mwenye uwezo wa menejimenti, visheni, kipaji cha kubuni mambo mapya, kuzitumia kikamilifu rasilimali za mkoa na ustadi wa kuwa na mikakati na mipango inayowawezesha wakazi wa mkoa kufankisha kile walichoazimia kukifanya kwa wakati na kwa ufanisi na ufanifu wa hali ya juu.
Bunge la mkoa tofauti na bunge la kitaifa litakuwa sio tu na uwakilishi wa wabunge wa kawaida bali pia wa watu kulingana na makundi ya kimaslahi na wale wenye vipaji, uwezo na utaalamu ambao unaaminika unaweza kuwa mtaji kwa maendeleo ya mkoa husika. Kila kitu kitakuwa kimeelezwa katika katiba za mkoa na kanuni na taratibu za utawala wa mikoa huru kiuchumi na kijamii.
Ili kuongeza kasi ya maendeleo ya mikoa, kila mkoa utalazimika kuwa na redio, televisheni na gazeti la umma la mkoa; achilia mbali vyombo vya habari vinavyoanzishwa na vitakavyoanzishwa na wawekezaji mbalimbali toka ndani na nje ya nchi. Urahisi huu wa mawasiliano ukiambatana na ufikivu mkubwa zaidi wa simu za mkononi mkoani utaongeza kwa kiasi kikubwa kasi ya maendeleo katika mikoa ambayo sasa haitakuwa imefungwa kwenye mkanda wa suruali ya baba au kamba za sketi ya mama kimaendeleo.
Aidha, katiba za mkoa na sheria zitakazofuatia zitailinda mikoa na ufisadi, wizi, rushwa na matumizi mabaya ya serikali kuu ya kitaifa kama inavyofanyika kwa kawaida katika nchi ambazo zinafuata mfumo wa shirikisho au muungano wa kimikoa, k.m. , Ujerumani, Urussi, Uchina, India, Brazil, Afrika Kusini na kadhalika.
Wabunge katika bunge la mkoa watalipwa mishahara kulingana na elimu na ujuzi walio nao kama wanavyolipwa wakazi wengine. Hii ina maana, kama mbunge ni mwalimu wa sekondari mwenye shahada ya kwanza, atalipwa mshahara wa mwalimu wa sekondari mwenye shahada ya kwanza. Kama ni mhadhiri wa chuo kikuu atalipwa mshahara wa mhadhiri. Na kama ni daktari wa hospitali atalipwa mshahara wa daktari. Kwa utaratibu huu wabunge wa mkoa wataenziwa kazi zao na maslahi yao yataendana na kuendelea kujiendeleza pia katika taaluma zao. Posho zitakuwa zaidi ni za kujikimu tu na hivyo kupunguza sana matumizi ya serikali katika eneo hili.
Hii ina maana kutokana na kuwepo kwa mabunge ya mkoa, bunge la kitaifa sasa, litahitaji muda mdogo tu kuzungumzia masuala ya kitaifa na kimipango. Tunaamini bunge hilo litahitaji juma moja tu kila baada ya miezi mitatu ili kufanya kazi zake na sio zaidi ya hapo. Bunge hilo jipya la taifa litakuwa ni la wawakilishi wa majimbo tu na hakuna uwakilishi wa jumuiya au wabunge wa kuteuliwa. Kwa namna hii nchi itaokoa mabilionikama sio matrilioni ya shilingi zitakazoelekezwa kwenye maendeleo ya wananchi mikoani. Aidha, kwa mantiki hii serikali ya JMT inaweza ikawa na serikali ndogo yenye mawaziri wasiozidi 14 tu ( Angalia makala za nyuma kuhusu hili ).
Kwa mikoa kuwa na Waziri mkuu wa mkoa au Gavana, mikoa italazimisha kisheria kuwa na serikali ya kweli ya Muungano wa Tanzania. Mikoa itakuwa imevunjwa na kuwa Tanganyika ndogongogo zinazojitawala na kujiamulia mambo yake kama Zanzibar na SMZ zinavyofanya. Kumbuka kuna mikoa ambayo ina wakazi wengi mara mbili au hata sita ya wakazi wote wa Zanzibar. Haki katika hili itakuwa imetendeka.
Waziri Mkuu wa Mkoa au Gavana wa Mkoa atachagua mawaziri wasiozidi kumi na mbili kushughulikia hasa maeneo yenye fursa za mkoa kujiendeleza kiuchumi au kutatua kwa kasi matatizo na changamoto zinazowakabili wakazi wa mkoa husika bila ngojangoja kama inayotokea katika muundo na mfumo wa serikali wa hivi sasa.
Serikali za mikoa, mathalani, Kagera inaweza kuamua kuuza sukari yote inayozalishwa mkoani humo Burundi kama soko linaruhusu na kisha wakanunua sukari ya bei rahisi kutoka Uganda au Rwanda au nchi nyinginezo duniani.
Serikali ya mkoa wa Katavi au Rukwa inaweza kuamua kuuza mahindi yake Zambia au Malawi au Kongo kama biashara huko ni nzuri ili mradi inahakikisha wananchi wake wanabakia na akiba tosha ya chakula hadi kufikia msimu ujao iwe kwa kile walicholima au kile ambacho watanunua kutokana na faida ya kuuza mahindi yao nchi za nje. Mkoa uanaweza kujigeuza kitovu cha kudumu cha biashara ya nafaka na nchi zinazouzunguka kwa faida ya mkoa na wakazi wake.
Mikoa ya Geita, Mwanza, Shinyanga, Mara, Ruvuma, Tabora, Ruvuma, Mbeya, Iringa na kadhalika inaweza ikapitia upya mkataba wa uchimbaji madini na kuhakikisha wakazi kwenye maeneo husika sio tu wanalipwa malipo halali bali wanakuwa na hisa katika makampuni ya uchimbaji madini. Wachimbaji waliopo wakizira, watatafutwa wawekezaji toka Uchina, Korea, Japani, Urussi na kwingineko kuwanunua na kisha wawekezaji upya wakaendesha shughuli zao kwa mujibu wa sheria mpya za mkoa husika.
Kwa kuwa mkoa utakuwa huru kiuchumi na kijamii, mkoa utaruhusiwa kuingia katika ushirikiano na nchi, makampuni na watu ndani na nje ya nchi kwa maendeleo ya mkoa na wakazi wake. Hii ina maana pia kuwa mikoa itakuwa na haki ya kupokea misaada toka nchi na watu mbalimbali duniani kwa maendeleo yake na wakazi wake.
Ieleweke ya kwamba mikoa huru kiuchumi, kijamii na kisiasa sio lazima iwe inatawaliwa na chama tawala kama chama tawala hakikushinda katika mkoa huo. Chama kinachoshinda mkoani ndicho kitakachounda serikali ya mkoa na sio vinginevyo. Hili litaruhusu kuwepo ushindani wa kweli wa kisiasa, kuchumi na kijamii kwa maendeleo makubwa zaidi ya wakazi wa mikoa bila maendeleo yao kuchafuliwa na siasa na sera mbovu za serikali kuu.
Faida kubwa ya muundo na mfumo huu wa kisiasa ni kwamba utakuwa ni chuo kikuu kwa viongozi wa baadaye wa nchi. Anayekuja kuwa waziri mkuu baada ya kuwa waziri mkuu wa mkoa, hatakuwa na mengi mapya ya kujfunza kama ilivyo kwa wanaoteuliwa kwa nafasi hiyo hivi leo. Kadhalika mawaziri wa mikoa watachangia sio haba kuwa na mawaziri ambao wanajua uwaziri ni nini na hawaendi kujifunza uwaziri katika serikali kuu na kuwapotezea wananchi muda na maendeleo yao.
KUNA wanaoogopa eti tukiwa na serikali za shirikisho tutavunja umoja na amani yetu. Kabla ya kukubaliana au kutofautiana na watu wenye mawazo kama hayo hebu tujiulize na kujaribu kujibu maswali yafuatayo:
. Hivi dunia leo sio inalazimisha watu wa maeneo na jamii ndogo kujitawala ?
. Je, jamii ndogo na maeneo madodo hayastahili kulinda na kuzitumia rasilimali zao kwa faida yao kwanza kabla ya watu wengine?
. Hivi serikali kuu zinakuwa na uchungu na uzalendo wa kutosha kuhusu maeneo na jamii ndogo au kuna unafiki na ubinafsi?
. Ni jamii zinazodhulumiwa au serikali kuu inayowadhulumu ndiyo watavunja amani na umoja wa nchi?
. Je, jamii na maeneo madogo yanaridhika yale yanayokipata toka serikali kuu?
. Je, jamii na maeneo madogo yanaridhika na jinsi misaada toka nje inavyotumika?
. Je, kiuchumi jamii na maeneo madogo yatafaidika zaidi kwa kuwa na serikali zao au kwa kutegemea serikali kuu?
. Je, jamii na maeneo madogo yatafanya biashara nzuri zaidi na nchi jirani au ni taifa zima ndilo linaloweza haya?
. Je, matatizo yanayokabili jamii na eneo dogo yatamalizwa haraka zaidi na serikali ndogo za kijamii au kieneo au serikali kuu?
. Je, fursa za kiuchumi zilizopo mkoani au jamii na eneo dogo zinaweza kutumika haraka zaidi kwa kuwa na serikali ya mkoa au kwa kusubiri serikali kuu ikumbuke mkoa husika ?
. Je, kijamii ni rahisi kujenga nyumba kwa kila familia kwa jamii na eneo dogo au kujenga nyumba kwa kila familia kwa nchi nzima?
. Ni mikoa mingapi yenye vyuo na vyuo vikuu Tanzania hivi leo?
. Ni mikoa mingapi yenye redio ya umma au binafsi ya mkoa inayosikika mkoa mzima hivi leo?
. Ni mikoa mingapi yenye gazeti la umma au binafsi la mkoa linalouzwa mkoa mzima hivi leo?
. Ni mikoa mingapi yenye televisheni ya umma au binafsi ya mkoa inayoonekana mkoa mzima hivi leo?
. Ni mkoa gani unaojua ni mazao au bidhaa au huduma au madini a u mafuta au rasilimali nyingine inayoweza kuharakisha maendeleo ya mkoa kuliko ilivyo hivi sasa?
. Je, mikoa ikiwa huru kiuchumi na kijamii itaweza kujitosheleza katika masuala ya maji, umeme, nishati na huduma mbalimbali za jamii muhimu?
. Je mikoa ambayo vyama vya upinzani vina wabunge au wawakilishi wengi ingetawaliwa na vyama hivyo maendeleo yao yangekuwa duni kama ilivyo hivi sasa ?
Haya ni maswali muhimu kujiuliza, kutafakari na kuyajibu ili kuona kwanini katika nyakati zetu serikali huru za mikoa ni kitu cha lazima na kisichoepukika. Ila ni lazima wananchi wafunguliwe macho kwanza na wao wenyewe waone faida na hasara za kukosa mikoa iliyo huru kiuchumi, kijamii na kisiasa.
Friday, December 16, 2011
Wednesday, November 2, 2011
Aljazeera tishio kwa nchi za Magharibi na Afrika
MAREKANI na Ulaya zimekuwa sio tu zikisambaratisha nchi zinazoendelea kwa kutumia vyombo vyao vya habari vyenye uwezo na nguvu za kutisha lakini pia wakati mwingine zimekuwa zikipandikiza redio, magazeti na vyombo vingine vya habari vya jana na leo ili kusambaratisha nchi ambazo zinapuuza maslahi yao na zinazokataa kuwa chini yao.
Hivi leo Marekani na Ulaya zinagaragazwa na Televisheni ya Aljazeera ambayo baada ya muda sio mrefu inafuatiwa pia na Radio Aljazeera tena kwa lugha za Kizungu.
Ni kwanini Aljazeera inakuwa tishio? Inakuwa tishio kwa sababu ya kukataa kutangaza uongo na kufichua ukweli bila kumuonea au kumpendelea mtu au kundi fulani la watu mahala popote pale duniani. Hivi ndivyo uandishi wa habari unavyotakiwa tofauti na tunavyoona jinsi CNN, MSNNBC, Fox, Sky, CBS na wengineo wanavyotumika kwa ajili ya kuficha ukweli juu yao na kuangaza na kuanika uongo juu ya wengine hata isipolazimu kufanya hivyo ili tu wazungu waonekane watu wa maana na sisi wengine tusio na maana.
Hivi sasa kuna maandamano katika nchi kadhaa ulimwenguni ikiwemo Marekani kwenyewe ambako watu wanaukataa mfumo wa uchumi wa kiwizi wa kibepari unaoruhusu asilimia 1 tu ya Wamarekni kula zaidi ya asilimia 90 ya kile kinachozalishwa Marekani na duniani kwa ujumla.
Mfumo huu si mwingine ila ni ule ambao kwao watu wachache pengine maelfu tu na wala sio laki wanadhibiti fedha, mitaji, uchumi, biashara, huduma na uwekezaji duniani. Watu hawa wachache wanaweka tena asilimia kama 10-15 ya watu toka sehemu mbalimbali duniani kudanganya asilimia 85 au zaidi ya watu wao kwa ajira zisizo na tija, mikopo isiyolipika na ufahari usiodumu.
Hali iliyofikiwa na mfumo wa namna hii ndio ile hali Karl Marx alioyoiita ' demokrasia ya kibepari inapotumika ili kukomba fedha zote zilizoko kwenye hazina ya serikali na kisha kuziweka fedha mifukoni mwa wanasiasa na matajiri wachache wanaoishi kwa kutapeli, kulangua, riba, rushwa na ufisadi wa kila namna.' Akatahadharisha demokrasia kama hii si mfumo unaoweza kumfaa binadamu wa jana,leo wala kesho. Utasambaratisha taifa na watu wake hatima ya yote!
Hakuna kitu kibaya duniani kama nchi moja kukubali kuolewa na nchi nyingine kama baadhi ya nchi za Kiafrika zinavyofanya katika mahusiano yake na Marekani, Uingereza, Ufaransa, Uchina, Italia, Urussi na wengineo kwa sababu mwanamme kama taifa bado ni mwanamme asiyetosheka na ambaye hukudharau ukishamtegemea kwa kila kitu.
Aidha, mataifa makubwa duniani yamefanikiwa si haba kwa kuwafanya wananchi wake wajinga, mbumbumbu na wasiojua chochote kinachoendelea katika dunia hii. Na ndio maana wengi wao wamejikuta wako hadharani wakiwa na chupi zilizofika kwenye magoti kiuchumi na kijamii! Aibu yao inazua sio tu wasiwasi bali pia hasira na kutaka kuleta mabadiliko yatakayowafanya waondokane na ujinga na udhalilishwaji wao na mabwana au watawala wao.
Hii ina maana kwamba ukoloni haujawahi kwisha na hautawahi kwisha duniani. Ile asilimia moja niliyoizungumza inaifanya dunia yote koloni lake. Asilimia 10-15 chini yao wanagawana vipande vipande vya dunia. Na katika hawa kuna wakuu wa idara za serikali, matajiri na watawala wa kuzaliwa wenye utajiri wa kurithishwa-kwa maneno mengine wenye mtaji ndio wakoloni wapya katika dunia yetu.
Ndio maana katika kila nchi ya Kiafrika ni sawa ukihesabu kuwa rais na mawaziri wake wote wanatawaliwa na mfadhili au huyo anyejiita mkoloni wa zamani. Si watu huru hasa katika nchi zetu nyingi za Kiafrika. Hawana hiari ya hiki au kile, na hata kuwepo kwao madarakani kunategemea ni nani hao wakubwa wanaomtaka. Kumbuka Kabila wa Kongo, Sankara wa Bourkina Fasso na Machel wa Mozambique.
Hivi sasa katika kutapatapa na kuona mashamba ya bibi ya dunia yanatoweka na Mchina, Mbrazili, Mrussi na Mhindi wanakuja kwa kasi kubwa kujitafutia na wao riziki halali miongoni mwa Waafrika nchi za Magharibi zimeanza kutaharuki na kuanza kuwa za mwanzo kwenda kinyume na maadili ya demokrasia.
Marekani hivi sasa inazuia matangazo ya Aljazeera yasisikilizwe na wananchi wake; Ulaya inataka kuifosi Ugiriki ikubali kuwatunuku wananchi wake ugumu wa maisha usiosthaimilika ili Ugiriki ipate mikopo; Uingereza inataka kuilazimisha Afrika kukubali usenge na ushoga ili nchi za Kiafrika ndiio zifikiriwe kwa mikopo. Hakuna mantiki hata kidogo.
Wanachosahau jamaa hawa ni kwamba, huwezi kuwadanganya watu wote kwa muda wote. Aljazeera kwa ujasiri na ubinadamu imeamua kufanya kazi ya kuwazindua wanyonge duniani bila kujali wako kwenye mataifa tajiri au maskini. Na kwa sababu hiyo ile asilimia 1 ya juu kabisa ya mabepari duniani na vibaraka wao katika kila nchi kwa kila hali ni lazima wawe maadui wa Aljazeera.
Hata hivyo zama za ukweli zikishafika ni upumbavu kujifukia kichwa chini kwenye mchanga kama mbuni kwa kudhani kuwa wewe usipoonekana macho au wewe usipoona wengine basi hauonekani kabisa.
Afrika kwa miaka zaidi ya 50 imetenda dhuluma kubwa kwa wazee, wanawake, vijana, wanavijiji, wakulima, wafanyakazi, wanafunzi na watoto wake. Huu ni muda mwafaka wa kuondokana na vyombo vya habari vya kudanganya na kuzaini kwani Aljazeera ikishaanza kutangaza kwa lugha za Kiafrika kwa televisheni na redio zake tutajikuta matatani na wananchi wetu.
Wale wanaopiga danadana na kuruhusu wananchi kuandika katiba mpya, wanaochezea demokrasia, wanoruhusu ufisadi na rushwa, wanaoruhusu maliasili za nchi kuchotwa sawa na bure na wanaoamua kutowathamini watu wao na kuthamini zaidi watu kutoka nje wanapaswa kukoma mara moja na kuutazama mustakabli mpya kwa nia njema ya kujinusuru wao wenyewe, mataifa yao na vizazi vyao. Na wakati ni huu, hakuna kabisa muda wa kupoteza, kusubiri au kungoja ngoja. Chelewa, chelewa, utamkuta Aljazeera keshaingia ndani na mwana tena si wako!
Hivi leo Marekani na Ulaya zinagaragazwa na Televisheni ya Aljazeera ambayo baada ya muda sio mrefu inafuatiwa pia na Radio Aljazeera tena kwa lugha za Kizungu.
Ni kwanini Aljazeera inakuwa tishio? Inakuwa tishio kwa sababu ya kukataa kutangaza uongo na kufichua ukweli bila kumuonea au kumpendelea mtu au kundi fulani la watu mahala popote pale duniani. Hivi ndivyo uandishi wa habari unavyotakiwa tofauti na tunavyoona jinsi CNN, MSNNBC, Fox, Sky, CBS na wengineo wanavyotumika kwa ajili ya kuficha ukweli juu yao na kuangaza na kuanika uongo juu ya wengine hata isipolazimu kufanya hivyo ili tu wazungu waonekane watu wa maana na sisi wengine tusio na maana.
Hivi sasa kuna maandamano katika nchi kadhaa ulimwenguni ikiwemo Marekani kwenyewe ambako watu wanaukataa mfumo wa uchumi wa kiwizi wa kibepari unaoruhusu asilimia 1 tu ya Wamarekni kula zaidi ya asilimia 90 ya kile kinachozalishwa Marekani na duniani kwa ujumla.
Mfumo huu si mwingine ila ni ule ambao kwao watu wachache pengine maelfu tu na wala sio laki wanadhibiti fedha, mitaji, uchumi, biashara, huduma na uwekezaji duniani. Watu hawa wachache wanaweka tena asilimia kama 10-15 ya watu toka sehemu mbalimbali duniani kudanganya asilimia 85 au zaidi ya watu wao kwa ajira zisizo na tija, mikopo isiyolipika na ufahari usiodumu.
Hali iliyofikiwa na mfumo wa namna hii ndio ile hali Karl Marx alioyoiita ' demokrasia ya kibepari inapotumika ili kukomba fedha zote zilizoko kwenye hazina ya serikali na kisha kuziweka fedha mifukoni mwa wanasiasa na matajiri wachache wanaoishi kwa kutapeli, kulangua, riba, rushwa na ufisadi wa kila namna.' Akatahadharisha demokrasia kama hii si mfumo unaoweza kumfaa binadamu wa jana,leo wala kesho. Utasambaratisha taifa na watu wake hatima ya yote!
Hakuna kitu kibaya duniani kama nchi moja kukubali kuolewa na nchi nyingine kama baadhi ya nchi za Kiafrika zinavyofanya katika mahusiano yake na Marekani, Uingereza, Ufaransa, Uchina, Italia, Urussi na wengineo kwa sababu mwanamme kama taifa bado ni mwanamme asiyetosheka na ambaye hukudharau ukishamtegemea kwa kila kitu.
Aidha, mataifa makubwa duniani yamefanikiwa si haba kwa kuwafanya wananchi wake wajinga, mbumbumbu na wasiojua chochote kinachoendelea katika dunia hii. Na ndio maana wengi wao wamejikuta wako hadharani wakiwa na chupi zilizofika kwenye magoti kiuchumi na kijamii! Aibu yao inazua sio tu wasiwasi bali pia hasira na kutaka kuleta mabadiliko yatakayowafanya waondokane na ujinga na udhalilishwaji wao na mabwana au watawala wao.
Hii ina maana kwamba ukoloni haujawahi kwisha na hautawahi kwisha duniani. Ile asilimia moja niliyoizungumza inaifanya dunia yote koloni lake. Asilimia 10-15 chini yao wanagawana vipande vipande vya dunia. Na katika hawa kuna wakuu wa idara za serikali, matajiri na watawala wa kuzaliwa wenye utajiri wa kurithishwa-kwa maneno mengine wenye mtaji ndio wakoloni wapya katika dunia yetu.
Ndio maana katika kila nchi ya Kiafrika ni sawa ukihesabu kuwa rais na mawaziri wake wote wanatawaliwa na mfadhili au huyo anyejiita mkoloni wa zamani. Si watu huru hasa katika nchi zetu nyingi za Kiafrika. Hawana hiari ya hiki au kile, na hata kuwepo kwao madarakani kunategemea ni nani hao wakubwa wanaomtaka. Kumbuka Kabila wa Kongo, Sankara wa Bourkina Fasso na Machel wa Mozambique.
Hivi sasa katika kutapatapa na kuona mashamba ya bibi ya dunia yanatoweka na Mchina, Mbrazili, Mrussi na Mhindi wanakuja kwa kasi kubwa kujitafutia na wao riziki halali miongoni mwa Waafrika nchi za Magharibi zimeanza kutaharuki na kuanza kuwa za mwanzo kwenda kinyume na maadili ya demokrasia.
Marekani hivi sasa inazuia matangazo ya Aljazeera yasisikilizwe na wananchi wake; Ulaya inataka kuifosi Ugiriki ikubali kuwatunuku wananchi wake ugumu wa maisha usiosthaimilika ili Ugiriki ipate mikopo; Uingereza inataka kuilazimisha Afrika kukubali usenge na ushoga ili nchi za Kiafrika ndiio zifikiriwe kwa mikopo. Hakuna mantiki hata kidogo.
Wanachosahau jamaa hawa ni kwamba, huwezi kuwadanganya watu wote kwa muda wote. Aljazeera kwa ujasiri na ubinadamu imeamua kufanya kazi ya kuwazindua wanyonge duniani bila kujali wako kwenye mataifa tajiri au maskini. Na kwa sababu hiyo ile asilimia 1 ya juu kabisa ya mabepari duniani na vibaraka wao katika kila nchi kwa kila hali ni lazima wawe maadui wa Aljazeera.
Hata hivyo zama za ukweli zikishafika ni upumbavu kujifukia kichwa chini kwenye mchanga kama mbuni kwa kudhani kuwa wewe usipoonekana macho au wewe usipoona wengine basi hauonekani kabisa.
Afrika kwa miaka zaidi ya 50 imetenda dhuluma kubwa kwa wazee, wanawake, vijana, wanavijiji, wakulima, wafanyakazi, wanafunzi na watoto wake. Huu ni muda mwafaka wa kuondokana na vyombo vya habari vya kudanganya na kuzaini kwani Aljazeera ikishaanza kutangaza kwa lugha za Kiafrika kwa televisheni na redio zake tutajikuta matatani na wananchi wetu.
Wale wanaopiga danadana na kuruhusu wananchi kuandika katiba mpya, wanaochezea demokrasia, wanoruhusu ufisadi na rushwa, wanaoruhusu maliasili za nchi kuchotwa sawa na bure na wanaoamua kutowathamini watu wao na kuthamini zaidi watu kutoka nje wanapaswa kukoma mara moja na kuutazama mustakabli mpya kwa nia njema ya kujinusuru wao wenyewe, mataifa yao na vizazi vyao. Na wakati ni huu, hakuna kabisa muda wa kupoteza, kusubiri au kungoja ngoja. Chelewa, chelewa, utamkuta Aljazeera keshaingia ndani na mwana tena si wako!
Saturday, October 15, 2011
Mola hawasaidii
Maziwa, mito bahari na chemchemi lukuki,
Nchi iliyo tajiri, lakini haizinduki,
Akili zakifakiri, ndizo zinazotamalaki,
Wasiojisaidia, Mola hawasaidii!
Ardhi yake bahari, nini hakistawiki?
Siasa za kikafiri, dhuluma zinahakiki,
Mkulima hanawiri, anyonywa mpaka haki,
Wasiojisaidia, Mola hawasaidii!
Wazee na matajiri, nchi wanaimiliki,
Ni heri nusu ya shari, kwao hilo hawaafiki,
Haijai bilauri, njaa yao haishibiki,
Wasiojisaidia, Mola hawasaidii!
Kiu yao ya tanuri, katu haimaliziki,
Ukubwa wao jeuri, na kazi haifanyiki,
Watakacho ufahari, wala si mikiki mikiki,
Wasiojisaidia, Mola hawasaidii!
Madini yamedhihiri, raia hanufaiki,
Akili zatahayari, uongozi kuafiki,
Ni nani mwenye habari, ambazo haziandikiki,
Wasiojisaidia, Mola hawasaidii!
Na misitu kwa ekari, mbao bei haishikiki,
Makazi yatuadhiri, watu hawathaminiki,
Wakubwa waona fahari, nje kwenda kuhakiki,
Wasiojisaidia, Mola hawasaidii!
Ndani hamna safari, ila zile za falaki,
Zanyong'onyea suduri, uhai hautamaniki,
Na walio na kiburi, hili halikubaliki,
Wasiojisaidia, Mola hawasaidii!
Viwanda tumeghairi, tunawapa mamluki,
Uzalishaji johari, bilavyo hatujengeki,
Viongozi washairi, na tungo hazighaniki,
Wasiojisaidia, Mola hawasaidii!
Kuwaomba matajiri, hulka siiafiki,
Twajidhalilisha ari, hamsini hatuamki,
Tuutazame urari, tutumie wetu mkuki,
Wasiojisaidia, Mola hawasaidii!
Vijana wanasubiri, na akili wastahiki,
Mapinduzi kuabiri, kama nchi haijengeki,
Na huu si ujibari, nia tutaiafiki,
Wasiojisaidia, Mola hawasaidii!
Nchi iliyo tajiri, lakini haizinduki,
Akili zakifakiri, ndizo zinazotamalaki,
Wasiojisaidia, Mola hawasaidii!
Ardhi yake bahari, nini hakistawiki?
Siasa za kikafiri, dhuluma zinahakiki,
Mkulima hanawiri, anyonywa mpaka haki,
Wasiojisaidia, Mola hawasaidii!
Wazee na matajiri, nchi wanaimiliki,
Ni heri nusu ya shari, kwao hilo hawaafiki,
Haijai bilauri, njaa yao haishibiki,
Wasiojisaidia, Mola hawasaidii!
Kiu yao ya tanuri, katu haimaliziki,
Ukubwa wao jeuri, na kazi haifanyiki,
Watakacho ufahari, wala si mikiki mikiki,
Wasiojisaidia, Mola hawasaidii!
Madini yamedhihiri, raia hanufaiki,
Akili zatahayari, uongozi kuafiki,
Ni nani mwenye habari, ambazo haziandikiki,
Wasiojisaidia, Mola hawasaidii!
Na misitu kwa ekari, mbao bei haishikiki,
Makazi yatuadhiri, watu hawathaminiki,
Wakubwa waona fahari, nje kwenda kuhakiki,
Wasiojisaidia, Mola hawasaidii!
Ndani hamna safari, ila zile za falaki,
Zanyong'onyea suduri, uhai hautamaniki,
Na walio na kiburi, hili halikubaliki,
Wasiojisaidia, Mola hawasaidii!
Viwanda tumeghairi, tunawapa mamluki,
Uzalishaji johari, bilavyo hatujengeki,
Viongozi washairi, na tungo hazighaniki,
Wasiojisaidia, Mola hawasaidii!
Kuwaomba matajiri, hulka siiafiki,
Twajidhalilisha ari, hamsini hatuamki,
Tuutazame urari, tutumie wetu mkuki,
Wasiojisaidia, Mola hawasaidii!
Vijana wanasubiri, na akili wastahiki,
Mapinduzi kuabiri, kama nchi haijengeki,
Na huu si ujibari, nia tutaiafiki,
Wasiojisaidia, Mola hawasaidii!
Friday, October 14, 2011
Dhahabu na madini mengineyo: Ipo bado nafasi ya Watanzania kunufaika zaidi
VIONGOZI wa Tanzania toka chini hadi juu wanakiri kwamba makosa yalifanyika katika kukaribisha wawekezaji katika uchimbaji madini nchini na inaelekea kitu kama hicho pia kinatokea katika shughuli za uchimbaji madini.
Makosa hayo ni pamoja na kufanya maisha na makazi ya wazawa wa maeneo husika kama vile hayana thamani kabisa; hawana urithi katika eneo husika wa madini na mali asili yake; kuwa serikali kuu ndiyo yenye sauti ya mwisho kuhusu maeneo ya wakazi na wenyeji husika; kwamba kuna watu waliopewa chochote kwa jina lolote lile ili kupata mikataba ambayo inawaruhusu kuchimba na kuchukua madini yetu sawa na bure; na kwamba baada ya Watanzania kuwa masikini kwa zaidi ya karibia miaka hamsini toka wawe huru; uwekezaji na ubinafsishaji huu kwa wageni ni hakikisho rasmi kwamba wataendelea kuwa masikini kwa miaka hamsini zaidi ijayo kama sio miaka 100 na zaidi.
Hata hivyo, wahusika wakuu ikiwemo kampuni moja maarufu na yenye jina kubwa duniani na iliyo na mirija katika makontinenti na nchi kadhaa ni kampuni iliyojenga sifa ya kuwatumia viongozi mbumbumbu, waroho na wasio na uchungu na watu wao na maendeleo yao ili kuwekeza kwenye nchi hizo na kuendeleza himaya na utajiri wake katika migodi, uchimabaji na uuzaji madini wakati mwingine katika nafasi ya ukiritmba na faida za kutisha.
Tanzania chini ya uongozi ulioridhika, kutoshekana na unaoamini kwamba Watanzania wengi wanaishi kwa zaidi ya miaka 1,000 hawana haraka kabisa na kulitazama upya jambo hili na kuchukua hatua mwafaka kwa wakati mwafaka. Na hili linafanyika wakati kuna ripoti zisizokanushika kwamba kuna mamia kama sio maelfu ya binadamu na wanyama katika maeneo fulani wanadhurika na wengine hata kufa kutokana na uchimbaji madini wa kampuni hii na nyingine kama hizo ambao zimepewa migodi kama zawadi na viongozi wetu.
Wakati tunaadhimisha miaka 12 ya kifo cha Baba wa Taifa ni wakati mzuri kutafakari kwanini mzee hakuwa na haraka na shughuli za uchimbaji madini. Na kwanini alikuwa mstari wa mbele kuanzisha Kitivo cha Jeolojia pale Mlimani na kisha kuhamasisha nchi zingine za Afrika Mashariki ili Tanzania iwe kituo kikuu cha utafiti wa madini Afrika Mashariki na kati. Juhudi ambazo kwa sababu moja au nyingine zimekwamishwa mahala fulani na leo tunaambiwa eti sababu moja ya kuruhusu uwekezaji sawa na bure eti ni kwa sababu hatuna vifaa wala wataalamu wanaoweza kutuwezesha sisi wenyewe kuchimba madini yetu. Jambo kama hili sio tu ni vigumu kueleweka na kuaminika bali linaonyesha kwamba tuliowapa kazi ya uongozi hawaongozi bali wanacheza na nchi na maisha yetu kutokana na sababu wanazozijua wao wenyewe.
Hata hivyo, nchi za Argentina, Bolivia, Ecuador na Peru zinatuonesha kwamba wananchi wanaweza kuikataa mikataba dhalimu iliyopitishwa kisiri na kiwiziwizi na walioko madarakani na kudai mikataba mipya itakayokuwa na manufaa na maslahi kwa wazawa wa maeneo husika na nchi nzima kwa ujumla.
Kwa wale waliotazama hali ilivyokuwa huko Argentina na jinsi Waargentina walivyosimama kidedea na kuifosi Barricks kubadili mikataba yake ya kidhalimu (Al Jazeera, Oktoba 14, 2011) atakuwa bila shaka amefaidika kwa mengi ikiwemo hatua kikundi cha kijamii kinachohitaji kupitia ili kuhakikisha mapinduzi haya ya kukabili makampuni ya kimataifa yenye tabia za kitapeli na kidhalimu kutokana na kuwatumia viongozi wenye ubinafsi na wanaojali maslahi ya kikundi kimoja katika nchi na wasioona mbali na mbele kwenye nchi masikini kama Tanzania.
Ingawa mikataba ya kuuza au kukodisha migodi kwa wageni imeshasainiwa na wageni wanaendelea kufaidika na dhahabu na madini yetu mengine bado hatujachelewa kabisa kuibadili hali hii. Tunaweza sisi wananchi, tukisaidiwa na wanasheria wetu na vyama vya siasa vyenye viongozi wenye uchungu na dhiki na umaskini wa Watanzania kuidhibiti hali hii na fumba na kufumbua tukajikuta tuna uchimbaji madini nchi wenye manufaa na tija kwa Watanzania walioko kwenye maeneo yaliko machimbo hayo na sisi tunaoishi mbali na maeneo hayo.
Kwa maneno mengine ni ujinga kukata tamaa kwamba kitu kilichoko katika ardhi yetu sisi wenyewe Watanzania hakiwezi kututoa kwenye umaskini wetu, lakini eti kinaweza kwenda kuwapa utajiri wawekezaji waliowekwa na viongozi wasiowatakia mema wananchi wa nchi hii utajiri mara mia au elfu katika kipindi cha miaka michache tu. Na kwamba pamoja na kuishi katika umasikini kwa zaidi ya miaka 50 kabla ya uchimbaji madini, tunaweza tena kwa roho mbaya na ubinafsi wa viongozi wetu kuendelea kuishi kwa miaka zaidi ya 50 kama sio 100 kama masikini wa kutupwa katika nchi yetu.
Ipo bado nafasi ya Watanzania kuwawajibisha viongozi wao na wale waliokula na kufaidika na uwekezaji wa wale wanaochma madini na mafuta nchini mwetu leo. Na sio kunufaika tu, bali hata kutajirika na wale waliohamishwa katika maeneo yanakochimbwa madini na mafuta kuwa na hisa katika makampuni yanayofanya shughuli hizo katika maeneo yao ya kuzaliwa ambayo leo wamefukuzwa na kujikuta hawana tena makwao.
Huu ni wakati mzuri sana wa kutumia mchakato wa katiba mpya kuijulisha bila uoga wala kificho serikali kwamba mali asili na
madini ni ya wakazi wa eneo, tarafa, wilaya na mkoa husika, kwanza kabla ya yote ni mali ya wakazi hao na sio mali ya serikali wala chama chochote cha kisiasa hapa nchini. Sio haki na ni dhuluma iliyopitukia mipaka kwa kiongozi yeyote aliyeko Dodoma au Dar es salaam au popote pale alipo kunufaika na madini ya Bulyanhulu, Merelani, Geita, North Mara na kwingineko wakati mkazi na mzawa wa eneo husika anahukumiwa kulalia utajiri na kuamkia ukata na kufa masikini baada ya kufagiwa toka eneo husika.
Endapo kuna wanasiasa au viongozi yeyote walionufaika kwa kutoa kibali cha umilikaji eneo, uchimbaji na uuzaji madini nje wanastahili kujiwajibisha wao wenyewe kabla hawajawajibishwa na nguvu ya umma.
Tulivyozoea huko nyuma, eti, serikali ilijichukulia kama baba na mama wa Watanzania wote. Na mali yote ya umma ilikuwa ni mali ya serikali. Hivi leo mambo sivyo yalivyo. Kuna kikundi cha watu wachache wanaojifanya wao ndio wanaomiliki mali zote za Watanzania sio kwa kuzitunza kwa faida ya Watanzania wote bali kwa kuzitumia na kuzifuja kwa manufaa yao wenyewe.
Katika hali kama hii, katiba mpya, pamoja na mambo mengine lazima ieleze kinagaubaga kwamba ipo haja ya kutathmini upya mali asili, madini, mafuta na rasilimali nyingine upya na thamani hiyo iwe ni mtaji na mali ya wananchi wa eneo husika na siyo ya kundi la wajanja wachache ndani au nje ya serikali kwa niaba ya wnaasiasa na viongozi fulani.
Laiti ardhi na mali asili kwenye maeneo yanakochimbwa madini na vitu vingine vya thamani leo ingefanyika kwa haki na usahihi hakuna mkazi wa maeneo hayo leo angelikuwa ni maskini na baadhi yao wangelikuw ana hisa nono katika makampuni yaliyopo hivi leo. Ujinga, uoga na kutokujua kwa wanavijiji haki zao kumechangia hili. Na ndio maana baadhi yetu tuna kampeni za kutaka kuona madaraka zaidi kwa mikoa, wilaya, tarafa, kata na vijiji ili viongozi wa juu wa taifa wasitumie mianya iliyopo kunyonya na kuwadhulumu watu wa maeneo fulani nchini.
Hatua za mwanzo kufanyika
Makampuni yaliyopewa migodi sawa na bure yanatambua ukweli huu, kwamba yanatunyonya tena kwa ile mbaya sana. Na baadhi yao wameanza kuzinduka na kuanza kuwagawia Watanzania kama mababu zao walivyofanya huko nyuma, shanga, vioo, nyembe na vipande vya nguo ili sisi kwa ujinga wetu tuendelee kuwaachia kuokota almasi na dhahabu yetu sisi tukiona hicho wanachotudanganya nacho kwamba eti kina thamani. Ninaamini Watanzania wa leo, hata wale wasiokwenda shule, sio wajinga kiasi hicho. Watanzania hawawezi kabisa kudanganyika kwa barabara, maji, shule na vitu kama hivyo ambavyo serikali yao kutokana na kodi wanayotoa na kama viongozi wangelipunguza mishahara na posho zao kwa asilimi hamsini tu wangelivipata.
Wanavijiji wawatafute watoto wao waliosoma sheria, jeolojia na menejimenti kuja kusimamia vuguvugu la kudai haki ya asili na kutajirika na madini na maliasili katika eneo lao.
Kikundi cha kuelimisha, kuelewesha na kuhamasisha kudai haki na utajiri kiandaliwe mapema iwezakanavyo na kazi yake kubwa ikiwa ni kuwafanya wanajamii wote kuwa kitu kimoja katika madai yao ya kutajirika kutokana na madini au maliasili zao na sio mgeni au wageni tu kunufaika na mali zetu, wakati wao tayari ni matajiri wa kutupwa, eti tu kwa kuwa kuna viongozi na wanasiasa wetu fulani, wananufaika na uwekezaji huo. Kitu kama hiki kinaendana kinyume kabisa na maadili aliyotuachia baba wa taifa pamoja na katiba yetu hii chakavu tuliyonayo leo.
Ni vizuri pia kwa viongozi wa jamii kusaidiwa na vyama visivyo vya kiserikali kwenda kwenye nchi ambazo tayari wananchi wake wananufaika na madini na mali asili zao mbalimbali kama vile Argentina, Bolivia, Peru na kwingineko.
Baada ya watu kueleweshwa na kuelimishwa kwamba wana nafasi bado ya kuwa matajiri na kuwa na hisa katika makampuni ya migodi kitakachofuatia
ni kampeni ya nyumba kwa nyumba ili kuhakikisha kwamba kila mpenda mabadiliko na maendeleo anakuwa ni sehemu ya vuguvugu na kila mtu kukubali kwanza kula shubiri kabla asali haijapatikana.
Baada ya kila nyuma na wakazi wake kulielewa na kulikubali hili kazi inayofuatia ni kuwa na mikutano ya mtaa, kata, tarafa, wilaya na mkoa ifanyike ili kuwafahamisha viongozi sababu, malengo na madhumuni ya vuguvugu la kurejeshewa haki na utajiri wa maeneo ya wazawa yaliyoachiwa wawekezaji kimakosa au kiujanja na baadhi ya wanasiasa na viongozi nchini.
Zoezi hili litapima viongozi mbalimbali kama wanasimama kuwatetea wananchi na maslahi yao au viongozi hao ni vibarakala wa serikali na vyama vya kisiasa na hawana habari kabisa sio tu na kesho ya wananchi husika bali hata leo yao pia hawana habari nayo.
-mikutano ya kuelimisha uongozi wa taifa
Hii ina maana mbunge, mkuu wa wilaya, mkuu wa mkoa ni lazima asimame na kuhesabiwa. Hesabu hii ndiyo itakayoamua kama nchi inafaa kuwa na viongozi wa kuteuliwa au wa kuchaguiwa na wananchi wa eneo husika. Maana unaweza kukuta wananchi sio tu wananyonywa mali asili na rasilimali zao nyingine na serikali kuu na viongozi wake, lakini pia wanabebeshwa mizigo wasiyostahili kubeba.
Masharti muhimu:
Ili kazi hii ya kudai haki na utajiri tokana na maliasili za wananchi ifanikiwe yapo masharti kadhaa:
Kwanza, zoezi zima lazima liendeshwe kwa nguvu za umma chini ya usimamizi ya watoto na wajukuu wa jamii husika waliosomea masuala ya sheria, madini, siasa na utawala, menejimenti, sayansi ya maamuzi, teknohama, fedha na uwekezaji na kadhalika.
Thamani ya mapato kutokana na uchimbaji dhahabu ifanyike kulingana na mapato yatakayopatikana tokana na uchimbaji na uuzaji dhahabu toka mgodi uanzwe kuchimbwa hadi dhahabu kumalizika kuchimbwa. Hii ina maana kama dhahabu imeanza kuchimbwa mwaka 1997 na itamalizika 2047, hii ni sawa na mapato ya miaka 50 na hesabu hii ndiyo itakayogawanywa kuwalipa fidia wanavijiji husika kama wabia pamoja na mwekezaji, serikali kuu, serikali ya mkoa, serikali ya wilya na wanaharakati watakaochangia kufanikisha jambo hili.
Ni lazima baada ya hpo kugawana faida sawa na wawekezaji katika uchimbaji dhahabu na madini kama hayo, na pale kampuni inaposhaurika ni vyema zaidi wananchi wa eneo husika na sio viongozi wasiohusika na eneo hilo kupewa hisa katika kampuni inayoshughulika na uchimbaji wa madini husika.
Uchimbaji dhahabu usilete madhara kwa wanadamu au mifugo, na kampuni au mtu yeyote anayesababisha madhara au vifo vya binadamu au wanayma kutokana na uchimbaji wa madini laima ahukumiwe kwa mujibu wa sheria za mauaji zilizopo hivi sasa.
Ni lazima wanavijiji ambao maeneo yao yalikwishataifishwa na kubinafsishiwa wawekezaji, walipwe fedha wanayostahili na kama fedha hiyo ililiwa na wakubwa basi irudishwe au mwekezaji alipe upya wanavijiji.
Wanasheria wanaojitolea kwa gharama ndogo wasimamie zoezi zima la ulipwaji upya wanavijiji. Wanasheria hawa wachangie pia kupatikana wawekezaji mbadala kutoka Brazili, Uchina, Vietnam, Korea, India, Urussi na kwingineko kule ambako kutawapatia wananchi wawekezaji watakaowanufaisha na kuwatajirisha wao pia kuliko wawekezaji hawa wa kutoka Kanada, Marekani na Afrika kusini waliopo hivi leo na wanaosadikiwa kula na kulindwa na wale walioko madarakani.
Wanavijiji wapewe hisa katika migodi au kampuni za dhahabu na madini mengine kwenye maeneo yote ambako migodi imeanzishwa na wao ndiko kulikokuwa na makazi yao ya awali toka walipozaliwa hadi kuhamishwa kwa mabavu na bila fidia au kwa kulipwa fidia sawa na mzaha!
Makosa hayo ni pamoja na kufanya maisha na makazi ya wazawa wa maeneo husika kama vile hayana thamani kabisa; hawana urithi katika eneo husika wa madini na mali asili yake; kuwa serikali kuu ndiyo yenye sauti ya mwisho kuhusu maeneo ya wakazi na wenyeji husika; kwamba kuna watu waliopewa chochote kwa jina lolote lile ili kupata mikataba ambayo inawaruhusu kuchimba na kuchukua madini yetu sawa na bure; na kwamba baada ya Watanzania kuwa masikini kwa zaidi ya karibia miaka hamsini toka wawe huru; uwekezaji na ubinafsishaji huu kwa wageni ni hakikisho rasmi kwamba wataendelea kuwa masikini kwa miaka hamsini zaidi ijayo kama sio miaka 100 na zaidi.
Hata hivyo, wahusika wakuu ikiwemo kampuni moja maarufu na yenye jina kubwa duniani na iliyo na mirija katika makontinenti na nchi kadhaa ni kampuni iliyojenga sifa ya kuwatumia viongozi mbumbumbu, waroho na wasio na uchungu na watu wao na maendeleo yao ili kuwekeza kwenye nchi hizo na kuendeleza himaya na utajiri wake katika migodi, uchimabaji na uuzaji madini wakati mwingine katika nafasi ya ukiritmba na faida za kutisha.
Tanzania chini ya uongozi ulioridhika, kutoshekana na unaoamini kwamba Watanzania wengi wanaishi kwa zaidi ya miaka 1,000 hawana haraka kabisa na kulitazama upya jambo hili na kuchukua hatua mwafaka kwa wakati mwafaka. Na hili linafanyika wakati kuna ripoti zisizokanushika kwamba kuna mamia kama sio maelfu ya binadamu na wanyama katika maeneo fulani wanadhurika na wengine hata kufa kutokana na uchimbaji madini wa kampuni hii na nyingine kama hizo ambao zimepewa migodi kama zawadi na viongozi wetu.
Wakati tunaadhimisha miaka 12 ya kifo cha Baba wa Taifa ni wakati mzuri kutafakari kwanini mzee hakuwa na haraka na shughuli za uchimbaji madini. Na kwanini alikuwa mstari wa mbele kuanzisha Kitivo cha Jeolojia pale Mlimani na kisha kuhamasisha nchi zingine za Afrika Mashariki ili Tanzania iwe kituo kikuu cha utafiti wa madini Afrika Mashariki na kati. Juhudi ambazo kwa sababu moja au nyingine zimekwamishwa mahala fulani na leo tunaambiwa eti sababu moja ya kuruhusu uwekezaji sawa na bure eti ni kwa sababu hatuna vifaa wala wataalamu wanaoweza kutuwezesha sisi wenyewe kuchimba madini yetu. Jambo kama hili sio tu ni vigumu kueleweka na kuaminika bali linaonyesha kwamba tuliowapa kazi ya uongozi hawaongozi bali wanacheza na nchi na maisha yetu kutokana na sababu wanazozijua wao wenyewe.
Hata hivyo, nchi za Argentina, Bolivia, Ecuador na Peru zinatuonesha kwamba wananchi wanaweza kuikataa mikataba dhalimu iliyopitishwa kisiri na kiwiziwizi na walioko madarakani na kudai mikataba mipya itakayokuwa na manufaa na maslahi kwa wazawa wa maeneo husika na nchi nzima kwa ujumla.
Kwa wale waliotazama hali ilivyokuwa huko Argentina na jinsi Waargentina walivyosimama kidedea na kuifosi Barricks kubadili mikataba yake ya kidhalimu (Al Jazeera, Oktoba 14, 2011) atakuwa bila shaka amefaidika kwa mengi ikiwemo hatua kikundi cha kijamii kinachohitaji kupitia ili kuhakikisha mapinduzi haya ya kukabili makampuni ya kimataifa yenye tabia za kitapeli na kidhalimu kutokana na kuwatumia viongozi wenye ubinafsi na wanaojali maslahi ya kikundi kimoja katika nchi na wasioona mbali na mbele kwenye nchi masikini kama Tanzania.
Ingawa mikataba ya kuuza au kukodisha migodi kwa wageni imeshasainiwa na wageni wanaendelea kufaidika na dhahabu na madini yetu mengine bado hatujachelewa kabisa kuibadili hali hii. Tunaweza sisi wananchi, tukisaidiwa na wanasheria wetu na vyama vya siasa vyenye viongozi wenye uchungu na dhiki na umaskini wa Watanzania kuidhibiti hali hii na fumba na kufumbua tukajikuta tuna uchimbaji madini nchi wenye manufaa na tija kwa Watanzania walioko kwenye maeneo yaliko machimbo hayo na sisi tunaoishi mbali na maeneo hayo.
Kwa maneno mengine ni ujinga kukata tamaa kwamba kitu kilichoko katika ardhi yetu sisi wenyewe Watanzania hakiwezi kututoa kwenye umaskini wetu, lakini eti kinaweza kwenda kuwapa utajiri wawekezaji waliowekwa na viongozi wasiowatakia mema wananchi wa nchi hii utajiri mara mia au elfu katika kipindi cha miaka michache tu. Na kwamba pamoja na kuishi katika umasikini kwa zaidi ya miaka 50 kabla ya uchimbaji madini, tunaweza tena kwa roho mbaya na ubinafsi wa viongozi wetu kuendelea kuishi kwa miaka zaidi ya 50 kama sio 100 kama masikini wa kutupwa katika nchi yetu.
Ipo bado nafasi ya Watanzania kuwawajibisha viongozi wao na wale waliokula na kufaidika na uwekezaji wa wale wanaochma madini na mafuta nchini mwetu leo. Na sio kunufaika tu, bali hata kutajirika na wale waliohamishwa katika maeneo yanakochimbwa madini na mafuta kuwa na hisa katika makampuni yanayofanya shughuli hizo katika maeneo yao ya kuzaliwa ambayo leo wamefukuzwa na kujikuta hawana tena makwao.
Huu ni wakati mzuri sana wa kutumia mchakato wa katiba mpya kuijulisha bila uoga wala kificho serikali kwamba mali asili na
madini ni ya wakazi wa eneo, tarafa, wilaya na mkoa husika, kwanza kabla ya yote ni mali ya wakazi hao na sio mali ya serikali wala chama chochote cha kisiasa hapa nchini. Sio haki na ni dhuluma iliyopitukia mipaka kwa kiongozi yeyote aliyeko Dodoma au Dar es salaam au popote pale alipo kunufaika na madini ya Bulyanhulu, Merelani, Geita, North Mara na kwingineko wakati mkazi na mzawa wa eneo husika anahukumiwa kulalia utajiri na kuamkia ukata na kufa masikini baada ya kufagiwa toka eneo husika.
Endapo kuna wanasiasa au viongozi yeyote walionufaika kwa kutoa kibali cha umilikaji eneo, uchimbaji na uuzaji madini nje wanastahili kujiwajibisha wao wenyewe kabla hawajawajibishwa na nguvu ya umma.
Tulivyozoea huko nyuma, eti, serikali ilijichukulia kama baba na mama wa Watanzania wote. Na mali yote ya umma ilikuwa ni mali ya serikali. Hivi leo mambo sivyo yalivyo. Kuna kikundi cha watu wachache wanaojifanya wao ndio wanaomiliki mali zote za Watanzania sio kwa kuzitunza kwa faida ya Watanzania wote bali kwa kuzitumia na kuzifuja kwa manufaa yao wenyewe.
Katika hali kama hii, katiba mpya, pamoja na mambo mengine lazima ieleze kinagaubaga kwamba ipo haja ya kutathmini upya mali asili, madini, mafuta na rasilimali nyingine upya na thamani hiyo iwe ni mtaji na mali ya wananchi wa eneo husika na siyo ya kundi la wajanja wachache ndani au nje ya serikali kwa niaba ya wnaasiasa na viongozi fulani.
Laiti ardhi na mali asili kwenye maeneo yanakochimbwa madini na vitu vingine vya thamani leo ingefanyika kwa haki na usahihi hakuna mkazi wa maeneo hayo leo angelikuwa ni maskini na baadhi yao wangelikuw ana hisa nono katika makampuni yaliyopo hivi leo. Ujinga, uoga na kutokujua kwa wanavijiji haki zao kumechangia hili. Na ndio maana baadhi yetu tuna kampeni za kutaka kuona madaraka zaidi kwa mikoa, wilaya, tarafa, kata na vijiji ili viongozi wa juu wa taifa wasitumie mianya iliyopo kunyonya na kuwadhulumu watu wa maeneo fulani nchini.
Hatua za mwanzo kufanyika
Makampuni yaliyopewa migodi sawa na bure yanatambua ukweli huu, kwamba yanatunyonya tena kwa ile mbaya sana. Na baadhi yao wameanza kuzinduka na kuanza kuwagawia Watanzania kama mababu zao walivyofanya huko nyuma, shanga, vioo, nyembe na vipande vya nguo ili sisi kwa ujinga wetu tuendelee kuwaachia kuokota almasi na dhahabu yetu sisi tukiona hicho wanachotudanganya nacho kwamba eti kina thamani. Ninaamini Watanzania wa leo, hata wale wasiokwenda shule, sio wajinga kiasi hicho. Watanzania hawawezi kabisa kudanganyika kwa barabara, maji, shule na vitu kama hivyo ambavyo serikali yao kutokana na kodi wanayotoa na kama viongozi wangelipunguza mishahara na posho zao kwa asilimi hamsini tu wangelivipata.
Wanavijiji wawatafute watoto wao waliosoma sheria, jeolojia na menejimenti kuja kusimamia vuguvugu la kudai haki ya asili na kutajirika na madini na maliasili katika eneo lao.
Kikundi cha kuelimisha, kuelewesha na kuhamasisha kudai haki na utajiri kiandaliwe mapema iwezakanavyo na kazi yake kubwa ikiwa ni kuwafanya wanajamii wote kuwa kitu kimoja katika madai yao ya kutajirika kutokana na madini au maliasili zao na sio mgeni au wageni tu kunufaika na mali zetu, wakati wao tayari ni matajiri wa kutupwa, eti tu kwa kuwa kuna viongozi na wanasiasa wetu fulani, wananufaika na uwekezaji huo. Kitu kama hiki kinaendana kinyume kabisa na maadili aliyotuachia baba wa taifa pamoja na katiba yetu hii chakavu tuliyonayo leo.
Ni vizuri pia kwa viongozi wa jamii kusaidiwa na vyama visivyo vya kiserikali kwenda kwenye nchi ambazo tayari wananchi wake wananufaika na madini na mali asili zao mbalimbali kama vile Argentina, Bolivia, Peru na kwingineko.
Baada ya watu kueleweshwa na kuelimishwa kwamba wana nafasi bado ya kuwa matajiri na kuwa na hisa katika makampuni ya migodi kitakachofuatia
ni kampeni ya nyumba kwa nyumba ili kuhakikisha kwamba kila mpenda mabadiliko na maendeleo anakuwa ni sehemu ya vuguvugu na kila mtu kukubali kwanza kula shubiri kabla asali haijapatikana.
Baada ya kila nyuma na wakazi wake kulielewa na kulikubali hili kazi inayofuatia ni kuwa na mikutano ya mtaa, kata, tarafa, wilaya na mkoa ifanyike ili kuwafahamisha viongozi sababu, malengo na madhumuni ya vuguvugu la kurejeshewa haki na utajiri wa maeneo ya wazawa yaliyoachiwa wawekezaji kimakosa au kiujanja na baadhi ya wanasiasa na viongozi nchini.
Zoezi hili litapima viongozi mbalimbali kama wanasimama kuwatetea wananchi na maslahi yao au viongozi hao ni vibarakala wa serikali na vyama vya kisiasa na hawana habari kabisa sio tu na kesho ya wananchi husika bali hata leo yao pia hawana habari nayo.
-mikutano ya kuelimisha uongozi wa taifa
Hii ina maana mbunge, mkuu wa wilaya, mkuu wa mkoa ni lazima asimame na kuhesabiwa. Hesabu hii ndiyo itakayoamua kama nchi inafaa kuwa na viongozi wa kuteuliwa au wa kuchaguiwa na wananchi wa eneo husika. Maana unaweza kukuta wananchi sio tu wananyonywa mali asili na rasilimali zao nyingine na serikali kuu na viongozi wake, lakini pia wanabebeshwa mizigo wasiyostahili kubeba.
Masharti muhimu:
Ili kazi hii ya kudai haki na utajiri tokana na maliasili za wananchi ifanikiwe yapo masharti kadhaa:
Kwanza, zoezi zima lazima liendeshwe kwa nguvu za umma chini ya usimamizi ya watoto na wajukuu wa jamii husika waliosomea masuala ya sheria, madini, siasa na utawala, menejimenti, sayansi ya maamuzi, teknohama, fedha na uwekezaji na kadhalika.
Thamani ya mapato kutokana na uchimbaji dhahabu ifanyike kulingana na mapato yatakayopatikana tokana na uchimbaji na uuzaji dhahabu toka mgodi uanzwe kuchimbwa hadi dhahabu kumalizika kuchimbwa. Hii ina maana kama dhahabu imeanza kuchimbwa mwaka 1997 na itamalizika 2047, hii ni sawa na mapato ya miaka 50 na hesabu hii ndiyo itakayogawanywa kuwalipa fidia wanavijiji husika kama wabia pamoja na mwekezaji, serikali kuu, serikali ya mkoa, serikali ya wilya na wanaharakati watakaochangia kufanikisha jambo hili.
Ni lazima baada ya hpo kugawana faida sawa na wawekezaji katika uchimbaji dhahabu na madini kama hayo, na pale kampuni inaposhaurika ni vyema zaidi wananchi wa eneo husika na sio viongozi wasiohusika na eneo hilo kupewa hisa katika kampuni inayoshughulika na uchimbaji wa madini husika.
Uchimbaji dhahabu usilete madhara kwa wanadamu au mifugo, na kampuni au mtu yeyote anayesababisha madhara au vifo vya binadamu au wanayma kutokana na uchimbaji wa madini laima ahukumiwe kwa mujibu wa sheria za mauaji zilizopo hivi sasa.
Ni lazima wanavijiji ambao maeneo yao yalikwishataifishwa na kubinafsishiwa wawekezaji, walipwe fedha wanayostahili na kama fedha hiyo ililiwa na wakubwa basi irudishwe au mwekezaji alipe upya wanavijiji.
Wanasheria wanaojitolea kwa gharama ndogo wasimamie zoezi zima la ulipwaji upya wanavijiji. Wanasheria hawa wachangie pia kupatikana wawekezaji mbadala kutoka Brazili, Uchina, Vietnam, Korea, India, Urussi na kwingineko kule ambako kutawapatia wananchi wawekezaji watakaowanufaisha na kuwatajirisha wao pia kuliko wawekezaji hawa wa kutoka Kanada, Marekani na Afrika kusini waliopo hivi leo na wanaosadikiwa kula na kulindwa na wale walioko madarakani.
Wanavijiji wapewe hisa katika migodi au kampuni za dhahabu na madini mengine kwenye maeneo yote ambako migodi imeanzishwa na wao ndiko kulikokuwa na makazi yao ya awali toka walipozaliwa hadi kuhamishwa kwa mabavu na bila fidia au kwa kulipwa fidia sawa na mzaha!
Sunday, October 2, 2011
Huwezi kupambana na soko huru, kubali yaishe....
MANENO kama magendo, uvushaji mali mipakani, njia za panya, rushwa, ujangili, uhujumu uchumi ni maneno ya wanasiasa na mangimeza uchwara ambao wameshindwa kuukubali utandawazi na kwenda na wakati kwa kuilalia sekta moja ya uchumi na kuinufaisha zaidi sekta nyingine.
Penda usipende ukishaamua kufuata soko huru, ni ujinga kutaka kupambana na soko hilo kwani lina nguvu zake zisizoonekana na hizo ndizo zinazofuatwa na sio kauli za wanasiasa.
Safari, kauli na maneno ya wanasiasa yanayotolewa hivi sasa ni jitihada za kujikosha na kujisafisha baada ya kushindwa kufanya kazi wanayostahili kuifanya na badala yake kurukia yale yanayostahili kufanywa na soko bila ya kushinikikizwa na mtu.
Kwa mfano tunaona maamuzi ya EWURA yanavyochangia zaidi kunganya watu badala ya kunufaisha umma kwa sababu taasisi hiyo inataka kuingilia moja kwa moja maamuzi ya soko badala ya kuandaa na kuendeleza mazingira ambayo yatafanya sekta husika kufanya maamuzi yanayofaa kutokana na ujenzi wa ushindani na kuongeza sauti ya walaji nchini.
Sukari ni bidhaa inayotokana na zao la miwa. Miwa hii inapochakatwa ndipo sukari huzalishwa. Inavyoelekea ni rahisi sana kuachia soko huru kufanya kazi pale uuzaji miwa kwa wenye viwanda unapohusika, lakini ni rahisi kuingilia soko huru pale uuzaji sukari unapowanufaisha zaidi wenye viwanda na wafanyabiashara kuliko wananchi. Huu ni walakini wa mipango na sera. Na mipango na sera havifanywi kwa kushtukia bali ni vitu vinavyochukua muda.
Nilishawahi kuzungumzia jambo hili katika kesi ya saruji. Ghafla saruji ya Tanzania ilijikuta ina soko zuri nchi jirani. Kama ilivyo kawaida wanasiasa walichoona ni kuzuia saruji isiuzwe nje. NIkadai hilo ni kosa. Nikashauri kwamba, Malawi na Afrika Kusini na nchi za mbali zilikuwa na sukari nzuri tu iliyokuwa ikiuzwa kwa bei nafuu kuliko yetu, hivyo sisi tukubali kuuza yetu kwa bei ya juu kwa majirani na sisi tununue saruji ya bei rahisi toka nje. Hii ni akili ya kuzaliwa ya kibiashara na sio jambo kubwa kiasi hicho.
Ninarudia tena ni makosa kuingilia soko ila tu kama tunataka kuonesha unafiki wa kisiasa na machozi ya mamba eti tunawapenda sana Watanzania.
Kama tunawapenda Watanzania tatizo sio bei ya sukari, bali ni gharama za uendeshaji viwanda vya sukari na mashamba ya miwa. Mipango na sera za kuwapenda Watanzania zilikuwa zinatakiwa kuanzia huko kwa kuhakikisha kuwa bei ya dizeli, gesi na umeme, gharama za usafirishaji, nauli, upatikanaji umeme na mipango mibadala kiuchumi inakuwepo kwa wakati na hatufanyi kazi zetu kama vile zimamoto.
Nimewahi kuongelea pia juu ya ukubwa wa nchi hii ambao umeegemea zaidi kunufaisha mkoa wa Dar es salaam na wakazi wa Dar es salaam kuliko watu wa sehemu nyingine yoyote nchini. Kwa sababu hiyo bei za Dar es salaam ni rahisi kuliko za Ujiji, Tunduma, Mtwara, Peramiho, Bukoba, Holili, Namanga, Mwanza na Tarime.
Hali hii ya unafuu kwa Dsm na ughali kwa mikoa iliyo pembezoni ni kosa la kimipango na kisera linaloendelea kufanywa na serikali na chama tawala kwa kushindwa kutimiza ahadi na nadhiri yake ya kuufanya Dodoma kuwa mji mkuu wa nchi na vilevile kukaidi ushauri wa baba wa Taifa wa kupeleka madaraka mikoani au angalau kwenye ngazi ya kanda.
Makao makuu ya serikali yangelikuwa ni Dodoma ni dhahiri jiji la Dar es salaam lingebaki la kibiashara na hivyo kunufaika zaidi kibiashara na sio pia kisiasa na kiutawala kwa ofisi nyingi za kisiasa na zile za kiserikali kuwa na makao yake makuu mkoani hapa. Mikoa pembezoni ingelinufaika sio haba na kile Dar inachonufaika nacho leo, na hivyo wananchi wake kuwa na nafuu kubwa zaidi maishani.
Madaraka mikoani yangeruhusu mikoa iliyoko pembezoni moja kwa moja kufanya biashara na nchi jirani na kunufaika kijamii na kiuchumi kuliko ilivyo hivi sasa. Hakuna haki yoyote kuwazuia wazalishaji wa kitu chochote hapa nchini kupata bei nzuri soko la dunia au masoko ya nchi jirani. Hiyo siyo kazi ya wazalishaji wahusika, kupata vitu vya bei nafuu ni kazi ya serikali na sio lazima iwalazimishe wazalishaji wauze kwa bei serikali inayotaka. Wakijaribu kufanya hivyo kwenye sekta ya viwanda, hakuna (kama kweli bado nchi ina viwanda) kiwanda kitakachokubali na kubakia kuzalisha hapa nchini. Hii ni amri ya soko huru. Na soko huru sio tu katika bidhaa za viwanda bali pia katika mazao ya kilimo ambayo pengine ni muhimu zaidi kuliko kwa maisha na uhai kuliko bidhaa za viwandani.
Aidha, wakati umefika kuipa sekta ya kilimo uhuru ambao tayari sekta ya biashara na viwanda unayo, kama kweli tunataka kuona mapinduzi ya kilimo yakizuka nchini.
Tuliwahi kuongelea huko nyuma juu ya kuzifanya balozi zetu za nje kuwa ni balozi za kiuchumi na kimkakati. Huu ni wakati muafaka balozi zetu kuwa na watu wanaofuatilia masoko na pale inapoonekana mazao na bidhaa zetu yana bei nzuri nchi za nje basi tuuze, na sisi kama walivyo seremala badala ya kukaa kwenye viti tukae kwenye mbao tukijua kwamba kwa kufanya hivyo tunaweza kuja kuwa na samani bora zaidi siku zijazo.
Afrika ina kasoro moja kubwa. Na hii siyo nyingine ila ni kule kuongoza nchi na kuishi kama vile mambo 'yatajiseti' yenyewe, na wahusika wakaacha kuwa na mipango na mikakati hai ambayo inaweza kuleta utofauti mkubwa katika mustakabali wa nchi na watu wake. Hii ni lazima iwe ni visheni ya muda mrefu na sio mpango wa papo kwa hapo.
Ukichangia na kasoro mbalimbali katika mifumo, miundo, uratibu, udhibiti na utekelezaji ni rahisi kuona kwanini wanasiasa Afrika huona kuwa kuingilia soko huru ni njia ya mkato katika kufanikisha malengo yao ya kisiasa hata kama yale ya muda mrefu kiuchumi yanaharibika.
Fedha ambazo sasa serikali za mikoa/mitaa inazibeba katika vita visivyo na tija dhidi ya wauza sukari nje, ni bora zitumike kutatua matatizo ya wakazi wa mkoa husika kuliko kufujwa kama zinavyofujwa.
Ni vita isiyo na tija maana kimahesabu katika suala zima la magendo mipakani changamoto sio kuzuia tu bidhaa isivuke mpaka bali kubwa zaidi ni kuona hali, silaha za Kisaikolojia na maisha ya wale unaotaka washiriki katika vita hivyo. Ni dhahiri vita dhidi ya magendo ya sukari mipakani tayari vimekwishashindwa hata kabla havijaanza kwa sababu mlolongo mzima wa wale wanaotakiwa kuzuia sukari kuhusu nje kwa bahati mbaya ni orodha ya watu wenye njaa na kiu kali ya hali bora ya maisha na ambao hivi sasa wanaona kifo kwao ni karibu zaidi kuliko malengo mbalimbali waliyojiwekea kimaisha.
Ni polisi gani atakataa milioni 20 achilia mbali milioni 40 huko mpakani; ni ofisa uhamiaji gani atakataa milioni 100 katika mipaka yetu na kuna kioingozi gani mwenye uthubutu wa kukataa zaidi ya hizo katika mikoa yetu inayoongozwa na viongozi ambao hawakuchaguliwa bali wanateuliwa na wakubwa na aghalabu sio wazawa wa mikoa husika na hawana mapenzi wala uchungu na mkoa au wilaya wanaoyoisimamia!
Vita dhidi ya magendo kwa kutumia watu wenye dhiki, njaa, ukata na mishahara duni ni muhali kufanikiwa. Kinachoweza kufanikiwa hapa ni mipango na sera zinazoendana na soko huru na sio vinginevyo. Maana mwisho wa yote, badala ya wafanyabiashara tu kuwa ndio wanaonufaika basi unafaidisha pia wengine kiulaini kama vile watumishi vyombo vya ulinzi, maofisa kodi, maofisa uhamiaji na watu kama hao kwa hasara ya nchi nzima na wananchi wote kwa ujumla.
Penda usipende ukishaamua kufuata soko huru, ni ujinga kutaka kupambana na soko hilo kwani lina nguvu zake zisizoonekana na hizo ndizo zinazofuatwa na sio kauli za wanasiasa.
Safari, kauli na maneno ya wanasiasa yanayotolewa hivi sasa ni jitihada za kujikosha na kujisafisha baada ya kushindwa kufanya kazi wanayostahili kuifanya na badala yake kurukia yale yanayostahili kufanywa na soko bila ya kushinikikizwa na mtu.
Kwa mfano tunaona maamuzi ya EWURA yanavyochangia zaidi kunganya watu badala ya kunufaisha umma kwa sababu taasisi hiyo inataka kuingilia moja kwa moja maamuzi ya soko badala ya kuandaa na kuendeleza mazingira ambayo yatafanya sekta husika kufanya maamuzi yanayofaa kutokana na ujenzi wa ushindani na kuongeza sauti ya walaji nchini.
Sukari ni bidhaa inayotokana na zao la miwa. Miwa hii inapochakatwa ndipo sukari huzalishwa. Inavyoelekea ni rahisi sana kuachia soko huru kufanya kazi pale uuzaji miwa kwa wenye viwanda unapohusika, lakini ni rahisi kuingilia soko huru pale uuzaji sukari unapowanufaisha zaidi wenye viwanda na wafanyabiashara kuliko wananchi. Huu ni walakini wa mipango na sera. Na mipango na sera havifanywi kwa kushtukia bali ni vitu vinavyochukua muda.
Nilishawahi kuzungumzia jambo hili katika kesi ya saruji. Ghafla saruji ya Tanzania ilijikuta ina soko zuri nchi jirani. Kama ilivyo kawaida wanasiasa walichoona ni kuzuia saruji isiuzwe nje. NIkadai hilo ni kosa. Nikashauri kwamba, Malawi na Afrika Kusini na nchi za mbali zilikuwa na sukari nzuri tu iliyokuwa ikiuzwa kwa bei nafuu kuliko yetu, hivyo sisi tukubali kuuza yetu kwa bei ya juu kwa majirani na sisi tununue saruji ya bei rahisi toka nje. Hii ni akili ya kuzaliwa ya kibiashara na sio jambo kubwa kiasi hicho.
Ninarudia tena ni makosa kuingilia soko ila tu kama tunataka kuonesha unafiki wa kisiasa na machozi ya mamba eti tunawapenda sana Watanzania.
Kama tunawapenda Watanzania tatizo sio bei ya sukari, bali ni gharama za uendeshaji viwanda vya sukari na mashamba ya miwa. Mipango na sera za kuwapenda Watanzania zilikuwa zinatakiwa kuanzia huko kwa kuhakikisha kuwa bei ya dizeli, gesi na umeme, gharama za usafirishaji, nauli, upatikanaji umeme na mipango mibadala kiuchumi inakuwepo kwa wakati na hatufanyi kazi zetu kama vile zimamoto.
Nimewahi kuongelea pia juu ya ukubwa wa nchi hii ambao umeegemea zaidi kunufaisha mkoa wa Dar es salaam na wakazi wa Dar es salaam kuliko watu wa sehemu nyingine yoyote nchini. Kwa sababu hiyo bei za Dar es salaam ni rahisi kuliko za Ujiji, Tunduma, Mtwara, Peramiho, Bukoba, Holili, Namanga, Mwanza na Tarime.
Hali hii ya unafuu kwa Dsm na ughali kwa mikoa iliyo pembezoni ni kosa la kimipango na kisera linaloendelea kufanywa na serikali na chama tawala kwa kushindwa kutimiza ahadi na nadhiri yake ya kuufanya Dodoma kuwa mji mkuu wa nchi na vilevile kukaidi ushauri wa baba wa Taifa wa kupeleka madaraka mikoani au angalau kwenye ngazi ya kanda.
Makao makuu ya serikali yangelikuwa ni Dodoma ni dhahiri jiji la Dar es salaam lingebaki la kibiashara na hivyo kunufaika zaidi kibiashara na sio pia kisiasa na kiutawala kwa ofisi nyingi za kisiasa na zile za kiserikali kuwa na makao yake makuu mkoani hapa. Mikoa pembezoni ingelinufaika sio haba na kile Dar inachonufaika nacho leo, na hivyo wananchi wake kuwa na nafuu kubwa zaidi maishani.
Madaraka mikoani yangeruhusu mikoa iliyoko pembezoni moja kwa moja kufanya biashara na nchi jirani na kunufaika kijamii na kiuchumi kuliko ilivyo hivi sasa. Hakuna haki yoyote kuwazuia wazalishaji wa kitu chochote hapa nchini kupata bei nzuri soko la dunia au masoko ya nchi jirani. Hiyo siyo kazi ya wazalishaji wahusika, kupata vitu vya bei nafuu ni kazi ya serikali na sio lazima iwalazimishe wazalishaji wauze kwa bei serikali inayotaka. Wakijaribu kufanya hivyo kwenye sekta ya viwanda, hakuna (kama kweli bado nchi ina viwanda) kiwanda kitakachokubali na kubakia kuzalisha hapa nchini. Hii ni amri ya soko huru. Na soko huru sio tu katika bidhaa za viwanda bali pia katika mazao ya kilimo ambayo pengine ni muhimu zaidi kuliko kwa maisha na uhai kuliko bidhaa za viwandani.
Aidha, wakati umefika kuipa sekta ya kilimo uhuru ambao tayari sekta ya biashara na viwanda unayo, kama kweli tunataka kuona mapinduzi ya kilimo yakizuka nchini.
Tuliwahi kuongelea huko nyuma juu ya kuzifanya balozi zetu za nje kuwa ni balozi za kiuchumi na kimkakati. Huu ni wakati muafaka balozi zetu kuwa na watu wanaofuatilia masoko na pale inapoonekana mazao na bidhaa zetu yana bei nzuri nchi za nje basi tuuze, na sisi kama walivyo seremala badala ya kukaa kwenye viti tukae kwenye mbao tukijua kwamba kwa kufanya hivyo tunaweza kuja kuwa na samani bora zaidi siku zijazo.
Afrika ina kasoro moja kubwa. Na hii siyo nyingine ila ni kule kuongoza nchi na kuishi kama vile mambo 'yatajiseti' yenyewe, na wahusika wakaacha kuwa na mipango na mikakati hai ambayo inaweza kuleta utofauti mkubwa katika mustakabali wa nchi na watu wake. Hii ni lazima iwe ni visheni ya muda mrefu na sio mpango wa papo kwa hapo.
Ukichangia na kasoro mbalimbali katika mifumo, miundo, uratibu, udhibiti na utekelezaji ni rahisi kuona kwanini wanasiasa Afrika huona kuwa kuingilia soko huru ni njia ya mkato katika kufanikisha malengo yao ya kisiasa hata kama yale ya muda mrefu kiuchumi yanaharibika.
Fedha ambazo sasa serikali za mikoa/mitaa inazibeba katika vita visivyo na tija dhidi ya wauza sukari nje, ni bora zitumike kutatua matatizo ya wakazi wa mkoa husika kuliko kufujwa kama zinavyofujwa.
Ni vita isiyo na tija maana kimahesabu katika suala zima la magendo mipakani changamoto sio kuzuia tu bidhaa isivuke mpaka bali kubwa zaidi ni kuona hali, silaha za Kisaikolojia na maisha ya wale unaotaka washiriki katika vita hivyo. Ni dhahiri vita dhidi ya magendo ya sukari mipakani tayari vimekwishashindwa hata kabla havijaanza kwa sababu mlolongo mzima wa wale wanaotakiwa kuzuia sukari kuhusu nje kwa bahati mbaya ni orodha ya watu wenye njaa na kiu kali ya hali bora ya maisha na ambao hivi sasa wanaona kifo kwao ni karibu zaidi kuliko malengo mbalimbali waliyojiwekea kimaisha.
Ni polisi gani atakataa milioni 20 achilia mbali milioni 40 huko mpakani; ni ofisa uhamiaji gani atakataa milioni 100 katika mipaka yetu na kuna kioingozi gani mwenye uthubutu wa kukataa zaidi ya hizo katika mikoa yetu inayoongozwa na viongozi ambao hawakuchaguliwa bali wanateuliwa na wakubwa na aghalabu sio wazawa wa mikoa husika na hawana mapenzi wala uchungu na mkoa au wilaya wanaoyoisimamia!
Vita dhidi ya magendo kwa kutumia watu wenye dhiki, njaa, ukata na mishahara duni ni muhali kufanikiwa. Kinachoweza kufanikiwa hapa ni mipango na sera zinazoendana na soko huru na sio vinginevyo. Maana mwisho wa yote, badala ya wafanyabiashara tu kuwa ndio wanaonufaika basi unafaidisha pia wengine kiulaini kama vile watumishi vyombo vya ulinzi, maofisa kodi, maofisa uhamiaji na watu kama hao kwa hasara ya nchi nzima na wananchi wote kwa ujumla.
Sunday, July 24, 2011
Tatizo la umeme lisipoeleweka, ufumbuzi wake ni ndoto...
INAVYOELEKEA bado tatizo la umeme linaloikumba Tanzania kwa hivi sasa halijaweleka na wote, yaani, viongozi na wananchi. Katika hali kama hii ni vigumu kuona mwanga upande wa pili wa pango, hususan, kuhusiana na uwezekano wa suala hilo kupata ufumbuzi bila kuchelewa mambo yakaharibika zaidi kuliko ilivyo sasa, kisiasa na kiuchumi.
Maana tatizo letu kama nchi nyingi za Kiafrika ni lile la kushindwa kuwa na miundo na mifumo inayofanya kazi kwa sababu mbalimbali zikiwemo zile za nchi kuongozwa kwa kufuata mipango, ahadi na misaada kutoka nje. Na kushindwa kabisa kujikwanyua toka kwenye makucha ya ubepari mamboleo, matapeli wa kimataifa na mabwana wa watwana. Uongozi wowote unaojenga tabia ya ombaomba, hujenga nchi ya ombaomba. Nyumba au uongozi wowote unaojivuna na unaothamini watu wake kikwelikweli hukataa kujenga tabia ya ombaomba. Watazame ombaomba mitaani Dar es salaam na familia zao ujiulize kama watu hawa kweli wanaweza kuja kubadilika baadaye. Haiwezekani. Badala yake ,hujenga tabia ya kupenda kujitegemea, kukinaishwa na kusaidiwa na kujivunia kama wenzetu wa Korea ya Kaskazini walivyofanya kunako miaka ya 1950 pale walipotengeneza trekta lao wenyewe la kwanza na badala ya kwenda mbele, gia zote zikawa ni za rivasi tu.
Kiongozi yeyote anayewadharau raia wake: kwa kuwaita wavivu, wezi, wategaji, wababaishaji atambue sio raia wake wenye tatizo bali ni yeye mwenye tatizo. Kwa kifupi, mdharau chake na kuthamini wengine na vya wengine hawezi kamwe kuwa kiongozi wa kutumaniwa wala kutegemewa kuleta mabadiliko ya kimsingi katika jamii husika. China au Korea Kusini au Brazl au India au Malaysia -ingelifanya hivyo, isingekua hapo ilipo leo.
Kuwathamini kupindukia watu toka nje na kutowathmini ipasavyo raia wako mwenyewe ni mwanzo wa jengo la nchi lisilo na msingi madhubuti.
Haya ni mambo yaliyotufikisha hapa tulipo ambapo leo pamoja na kuwa na wasomi wa masuala ya umeme na nishati, hawatumiki kwa ajili hiyo, na wanaofanya maamuzi juu ya masulala hayo ni wanasiasa ambao bila shaka ni mbumbumbu katika masuala hayo na uelewa wao unategemea maelezo wanayopata kutoka kwa wanaojua wanachokizungumza.
Aidha, kutokana na hayo hapo juu imekuwa vigumu kwetu kupambanua kati ya yale ambayo tunatakiwa tuyafanye sisi wenyewe ima-fa-ima na yale ambayo kwa sababu fulani fulani tunalazimika kuomba msaada au ushirikiano toka kwa wengine.
Hakuna asiyetambua kwamba, ili tuendelee nchi yetu inahitaji : chakula, maji; hewa safi; mazinigira salama; afya bora na usalama kwa watu wetu; umeme au nishati mbadala; reli ya kisasa; barabara zinazopitika bila usumbufu wakati wote; makazi bora kwa watu; usafiri wa anga na majini; masoko yanayofikika ndani na nje ya nchi; ushauri mzuri kwa waliotutangulia; utafiti na kuyaelezea kwa urahisi masuala mbalimbali ili yaeleweke na wengi nchini na elimu inayosaidia kutatua matatizo yetu au kutumia fursa za maendeleo zilizopo ndani ya mipaka yetu na nje ya mipaka yetu.
Tujihusishe na hili suala la umeme tu na hayo mengine tuyaache hadi wakati mwingine. Inshallah. Kuna vitu ambavyo 'piga-ua' ni lazima Watanzania waiunde au watengeneze wao wenyewe kwa kutumia watu wetu waliosoma na wasiosoma ili mradi ni wabunifu, watundu na wanaoweza kujaribu bila kukatishwa tamaa na kushindwa katika maisha yao yote. Hata wakishindwa mara ngapi! Na mimi siamini kama tukiwatumia wasomi wetu, wataalamu wetu, mameneja wetu, wanajeshi wetu na vijana wetu kikamilifu tuna sababu ya kushindwa zaidi ya mara mbili tatu tu! Tunashindwa kwa sababu hatuwatumii watu wetu ipasavyo! Tunashindwa kwa sababu wanasiasa wetu wamejifanya pia wao ndio wataalamu na magwiji wa uchumi na maendeleo ya jamii.
Lakini kama tutawatumia maprofesa wetu wa vyuo vikuu na wanafunzi wao katika taaluma ya umeme na nishati sio tu tunaweza kupata ufumbuzi wa muda mfupi bali wa kudumu wa matatizo yetu.
Ni kitu cha kuhuzunisha kuwa pengine kutokana na viongozi wetu wa vyuo vikuu kujikita zaidi kwenye siasa badala ya uchumi na uzalishaji mali, mahala kama Chuo Kikuu cha Dar es salaam, chenye idara ya Uhandisi wa umeme hakina mifano yoyote inayofanya kazi kama vile mashamba ya upepo wa umeme au ya solar energy au uzalishaji umeme kwa njia nyingine mikoani - na inayoweza kulipiwa na kufadhalilwa na kupanuliwa kukidhi mahitaji yetu ya umeme.
Msiba mmoja mkubwa kwa taifa letu ni lile la kuwa na elimu na wasomi wanaojengwa ili na wao kutegemea vitu na mitambo inayozalishwa nje kwa maendeleo ya watu na nchi yetu.
Ni kwa njia hii tu ndiyo tutaweza kupata maendeleo ya kweli, ya kudumu na endelevu na sio kwa kutegemea kila kitu kitoke kwa wengine.
Vitu hivyo ni pamoja na mashine na mitambo kwa ajili ya uzalishaji umeme; utekaji, uvutaji na usmbazaji na umwagiliaji maji; uchimbaji madini; ujenzi wa bandari; ujenzi wa reli; ujenzi wa viwanja vya ndege; ujenzi wa barabara; ujenzi wa madaraja; miundombinu ya mawasiliano; na zana au vifaa mbalimbali vinavyohitajika katika ujenzi wa majengo na makazi katika nchi.
Msingi wa nchi yoyote usipoanzia katika mambo hayo hapo juu, nchi haiwezi kamwe kuuacha umaskini, achilia kuwa na maendeleo endelevu. Mpango na mkakati wowote unaoshindwa kuibua mambo haya, kisha kuyatafakari, kuyainisha na kuyapa kipaumbele katika maendeleo ya nchi ni mpango au mkakati unaofaa kutupwa jalalani pindi unapogundulika kwamba upo na unagharamiwa na kodi za wananchi. Ni mpango unaoihukumu nchi kubaki kwenye makucha ya wakoloni, mabepari na mabeberu kwa faida zao na wala sio kwa faida ya nchi na watu wake. Ni mapango unaowalazimisha watu wa nchi fulani wawe ombaomba, huku rasilimali za nchi zikichotwa kwenda kuwafanya watoa sadaka matajiri na matajiri zaidi. Ni mpango na mkakati unaomfanya raia wa nchi hii kuwa mtumwa wa wakoloni wa zamani na vibarakala wao na utandawazi na mumiani wake.
Kwa maneno mengine matatizo yetu mengi, likiwemo hilo la umeme ni matatizo yanayoweza kupatiwa ufumbuzi wa haraka na kudumu kwa kutumia vyema rasilimali watu yetu na rasimali watu toka nje pamoja na matumizi sahihi ya rasilimali zetu nyingine.
Hili linaweza kufaulu tu katika nchi ambayo haijvunii na haiwalindi mafisadi kama sehemu ya uongozi wake; inayotambua maendeleo yetu kama rasilimali zetu zinatumika vizuri, yanaweza kugharamiwa na watakaopata ujuzi na uzoefu katika mipango yetu mbalimbali ya maendeleo nchini, wakati watakapokwenda kuwafanyia Waafrika wengine kazi kama hii. Fisadi wa Kitanzania, ni mwizi anayejiibia shati lake mwenyewe. Fisadi wa kimataifa, haibi cha ndani, hukwapua cha nje kuja kuwafaa wenzake walio nyumbani na sio vinginevyo. Na uwezo wa kutajirika kwa kutumia rasilimali za wengine, ikiwa ni pamoja na umeme, kutokana na nchi zinazotuzunguka Watanzania tunao, isipokuwa hatuna uongozi unaoona wala kuelewa hili.
Vilevile, hili huweza kufanyika tu katika nchi ambayo chama tawala hakiendeshi nchi kana kwamba ni wabunge wake tu na wanachama wake wenye uwezo wa kuwa mawaziri, wakuu wa mikoa, wakuu wa wilaya, makatibu wakuu, wakurugenzi, mamaneja, majaji, mabalozi na wafanyakazi nchi za nje na wasimamizi wa taasisi mbalimbali. Bali kinaendesha nchi kwa kutumia akili, uwezo na michango ya Watanzania wote bila kujali ni wafuasi wa chama tawala au la.
Miaka hamsini baada ya Uhuru dunia imeipa fursa kubwa nchi yetu ya kuchagua na kuwakaribisha wataalamu tofauti toka sehemu mbalimbali duniani wenye ujuzi na uzoefu wa kila aina kuanzia watengnenezaji baiskeli hadi waunda satelaiti na roketi. Hawa ni binadamu wenzetu amabo leo ni 'jobless' pamoja na utaalamu au elimu na uzoefu wao, walioko huko Marekani, Ulaya Magharibi, Ulaya Mashariki, Marekani ya Kusini na Asia. Watu ambao tukiwapatia nyumba, gari na mshahara wa kukidhi mahitaji yao ya msingi wapo tayari kuja nchini hapa kusaidiana na sisi kuifanya nchi yetu iendelee kwa kasi na haraka zaidi. Kinachotakiwa ni kutambua hili na kujipanga kulishughulikia kwa namna ambayo litakuwa ni la faida kwetu sote, kwao na sisi kadhalika. Ni rahisi, kulizungumza hili kwa maneno, lakini ukweli ni kwmba kwa uoga, uziwi na upofu wa viongozi wetu hususan kuhusiana na yale yanayoandikwa na magazeti ni GUMU KAMA GAMBA LA KOBE.
Ila kwa bahati nzuri, kutokana na kukua kwa demokrasia nchini hapa upo uwezekano kwamba hili likifumbiwa macho na watawala, haliwezi kuachwa kuokotwa na wapinzani na wanaharakati wengine wenye mapenzi ya dhati ya nchi yao na uchungu na umasikini wa wananchi wenzao.
Katika miaka hii ambayo hali ya hewa inaendelea kubadilika na hatuna ahadi wala uhakika na mvua na kwa hiyo maji yanayotiririka katika mito na mabwawa tuliyoandaa kuzalisha umeme ni makosa makubwa kuendelea kutegemea umeme wa tabaini zinazoendeshwa na maji.
Hali yetu kama nchi sasa ni afadhali ukilinganisha na Somalia. Lakini upo uwezekano mkubwa wa ukame ulioikumba nchi hii iliyo kaskazini ya Tanzania na Kenya pia kuikumba nchi yetu.
Kutokana na ukweli huu, wale wanaoshika nafasi za uongozi nchini wanapaswa kuona mbali na mbele zaidi kuliko mwananchi wa kawaida.
Tatizo letu kwa hiyo siyo tu tatizo la ukame na kukosa mvua na maji ya kuzalisha umeme bali pia ni upungufu wa mipango na mikakati ya upatikanaji nishati ya uhakika na isiyoathirika na hali ya hewa kwa kadri inavyobadilika.
Tatizo pacha ni lile la serikali kudharau na kupuuza ushauri wa watu mbalimbali kuhusiana na muundo, kazi na nafasi ya shirka la umeme la taifa (TANESCO) katika kutafuta jawabu kamili na la kuridhisha la tatizo la umeme nchini.Shirika ambalo hivi leo limebatizwa na kuitwa 'TANZANIA ELELCTRIC SUFFOCATION COMPANY'- Ni dhahiri kwamba shirika ambalo miaka 50 baada ya uhuru limeweza kuwapatia asilimia 5 tu ya Watanzania umeme halina akili wala uwezo wa kufanya makubwa zaidi ya hayo ambayo tayari limekwishayafanya. Limefikia upeo wa uwezo na ubunifu wake.
Uendeshaji wa mashirika ya umma umefanana na ule wa mzazi ambaye alimshonea mwanaye suti akiwa na miaka 10 na leo mtoto huyo ambaye ana miaka 20 eti anatakiwa kuvaa suti ileile aliyoivaa akiwa na miaka 10. Watanzania tulikuwa milioni 9 mwaka 1960. Tuliyoyafanya wakati huo hayawezi kufanywa miaka hamsini baadaye na tukiwa takriban Watanzania milioni hamsini.
Baadhi ya watu wameshawahi shirika hilo livunjwe katika sehemu nne. Uzalishaji umeme, usambazaji umeme, utengenezaji vifaa vya umeme na uunganishaji na uhudumiaji miundo-mbinu ya umeme. Na sio lazima kufanya kazi zote hizi, bali shirika/serikali iruhusu Watanzania binafsi, wanajamii na wawekezaji kuendesha shughuli hizo kwa ufanisi na ufanifu zaidi.
Wapo pia waliopendekeza kwamba kila mkoa uwe na shirika lake la umeme, badala ya kuwa na shirika la umeme la taifa, kwa kutumia rasilimali za mkoa na ubia na wawekezaji wa ndani na nje. Hawa waliamini katika falsafa ya Schumacher kwamba 'Kidogo ni kizuri na chema zaidi,' au kwa Kiingereza: 'Small is Beautiful.' Kilal mkoa ungelitafuta chanzo chake binafsi cha uzalishaji umeme bila ya kutegemea tu maji. Hili lingeliendana pia na kifungu cha katiba kinachohusiana na kuwepo na ulinganifu katika maendeleo ya taifa-kitu ambacho kimeshindikana kabisa katika sekta hii ya nishati.
Niliposikiliza mahojiano ya Mh. Jakaya Kikwete na BBC akiwa ziarani Afrika Kusini sikuweza kuacha kuona kwamba majibu yake hayakuwa yenye kuonesha imani na matumaini kwamba tatizo la umeme liko ndani ya mikono ya Watanzania . Kilichojitokeza ni kwamba ni serikali ndiyo tu iliyokuwa ikitarajiwa kulitatua tatizo hilo. Aidha, serikali ilikuwa inapaswa kulipa fedha zote za ununuzi wa mitambo ya uzalishaji umeme papo kwa hapo. Kitu ambacho sio sahihi.
Ninaamini, Watanzania wakihamasishwa kama walivyokatwa kodi na haki zao mbalimbali ili kuanzisha mashirika ya umma (yaliyokuja kubinafsishwa bila wao kulipwa chochote) wana sababu, uwezo na nia ya kuchangia kumaliza tatizo la umeme lakini kwa sharti kuwa wanakuwa nao ni wamiliki wa mashirika yatakayoanzishwa kama sehemu ya ufumbuzi wa tatizo hili.
Vilevile, watengenezaji wa mitambo ya umeme wako tayari kukodisha mitambo yao na vile vile kuuza mitambo hiyo kwa mtu kulipia kidogo kidogo hadi deni liishe.
Hata hivyo kinachoonekan hapa ni kuwa mtazamo wa ndani kwa suala hili haupo na badala yake tuna mtazamo wa nje tu. Ikiwa ni pamoja na kuamini kuwa ni lazima tupate msaada au tukope kutoka nje ili tatizo la umeme liishe hapa nchini. Au wakati mwingine, pengine ni ujanja wa kununua vikubwa vikubwa kwa gharama kubwa ili watu wapate chambele au teni pasenti yao.
Sikubaliani kabisa na wale wanaoamini kwamba tatizo la umeme limesababishwa na ufisadi na eti kuna wauza majenereta walioihona serikali ili biashara yao ya majenereta ichanganye vilivyo. Japo kuwa majenereta yanauzwa kwa fujo hivi leo, lakini adha na gharama za uendeshaji majenereta ikiwemo kwa taasisi za serikali pia, kama vile gharama za dizeli au petroli; kelele; uchafu wa mazingira; nguvu kazi ya ziada katika kuzihudumia
ni mambo yanayoitia hoja hiyo hapo juu mashakani.
Uwekezaji katika sekta hii ya umeme unawezekana kabisa kutokea ndani ya nchi. Kwa maana kwamba, kama serikali ilivyoanzisha mashirika kwa kutumia kodi za wananchi upo uwezekano wa wananchi na wawekezaji kuchangia asilimia fulani na wawekezaji wa nje wakachangia asilimia fulani. Inapendekezwa ili makampuni ya umeme yawe ni ya Watanzania basi Watanzania wamiliki asilimia 51-60 na wawekezaji toka kwingineko asilimia 40-49.
Ufumbuzi wa tatizo la umeme, hali kadhalika, utakuwa mgumu bila kufahamu mchango wa siasa katika udhairu, kudumaa na kuserereka kwa TANESCO pamoja na misaada yote ambayo shirika hili limekuwa likipata toka kwa wafadhili wa nje na malipo ya gharama kubwa za umeme kuliko nchi nyingine yoyote Afrika. Wapo wanaodai kwamba shirika hilo liligeuzwa shamba la bibi na baadhi ya wanasiasa. Kwa maneno machache, shirika hilo, halijawahi kuendeshwa kibiashara bila kuingiliwa na wanasiasa. Pamoja na mifano mingi ya uwezo mdogo wa mameneja wa Kitanzania kusimamia miradi mikubwa hazijafanyika jitihada za dhati kumpata meneja toka nje mwenye uwezo na dhati ya kutusaidia Watanzania tuondokane na tatizo hili la umeme. Netsolution, kwa kiasi kikubwa, ilikuwa ni 'dili' lililonufaisha watu binafsi na sio nchi na watu wake.
Vilevile, wanasiasa Tanzania wamejenga tabia ya kuingilia kila fani na kazi nchini na kujifanya wao ni wataalamu zaidi kuliko wataalamu wenyewe. Toka mgao huu wa umeme pamoja na kuwa na vyuo vikuu vinavyotoa shahada mbalimbali za masuala ya umeme hapajawahikuendeshwa warsha au kongamano au angalau semina yoyote iliyowashsirikisha ili michango yao kuhusu ufumbuzi wa tatizo la umeme nchini lipatikane. Hii ni kasoro kubwa sana nchi mwetu, na isipoangaliwa itatuumiza katika kila sekta na nyanja ya maendeleo kwa miaka mingi ijayo.
Kama walivyo wanafunzi wa masomo mengine, wanafunzi wa shahada za uhandisi Tanzania hawapewi fursa za kutosha kutumia elimu yao kwa utafiti na uvumbuzi kwa majibu ya matatizo yetu mbalimbali. Bajeti yetu katika kuchochea utafiti ni ndogo mno, na sidhani kuna bajeti yoyote ya kuhamasisha ubunifu na uvumbuzi nchini miongoni mwa wasomi na wasiokuwa wasomi.
Wakati vijana wa Kenya wanagundua njia mbalimbali za kuzalisha umeme ikiwemo wa kutumia magurudumu ya baiskeli, umeme kwa upepe na sasa umeme kwa chupa ya cocacola na maji, vijana wa Kitanzania wamezungushiwa kitanzi shingoni mwao kinachowatia uoga katika kuanzisha au kuunda kitu chochote kinachoweza kuwa na manufaa kwa jamii yao. Na sio suala la ujinga au kutokujua. Ni kwamba wazazi wao na serikali yao haijakaa mkao wa kudai na kupata kutoka kwa kizazi hiki kipya zaidi ya muziki wa kuiga toka Marekani au kuvaa katakei!
Kati ya vijana wasiosoma sana ni wale ambao wameshawahi kuunda redio, kompyuta, gari, ndege, helikopta, transmita za redio na kadhalika. Lakini kwa kuwa baba na mama zao sio watu wakubwa, vijana hawa wameishia kutishiwa na vyombo vya dola hadi kujenga uoga mkubwa wa kuwa wabunifu na wavumbuzi wa kitu chochote katika maisha yao yaliyobakia. Ni nani anayekosa hapa. Tanzania au mtoto anayehusika?
Hebu, chunguza wewe mwenyewe katika nchi ambayo magazeti yametoa habari za watoto au vijana waliovumbua vitu mbalimbali, je, leo hao watoto wako wapi. Wamesaidiwa au wamehujumiwa, kwa kuwa tu ni watoto wa watu wasiokuwa na uwezo?
Nchi zetu za Kiafrika zimejenga utaratibu unaowafanya wananchi waamini kwamba bila serikali matatizo yao hayawezi kutatuliwa. Serikali inaonekana kujua kila kitu,kuwa na fedha zote duniani na kuwa bila mkono au mguu wa serikali hakuna anayeweza kusogea kwenda popote. Na serikali kwa upande wake inaelekea kuamini na kudhani ndiyo peke yake yenye majibu ya matatizo yote ya kiuchumi, kijamii, kisiasa, kiutamaduni na kiteknolojia. Kitu ambacho si kweli.
Guru wa Menejimenti, Profesa Peter Drucker anasema meneja mzuri na anayefanya kazi kwelikweli, hafanyi kazi yoyote. Ndivyo ilivyo pia kwa serikali nzuri na inayofanya kazi kwelikweli. Haifanyi kazi. Tunaposema haifanyi kazi hatuna maana haifanyi chochote au inategea tu. La hasha. Meneja na serikali bora na mfano wa kuigwa hufnaya kazi kwa kupitia watu, idara na taasisi nyingine. Unapoingilia kufanya kazi za watu wengine, idara na taasisi nyingine badla aya wao kuzifanya wenyewe kuna uwezekano mkubwa wa wewe kuvuruga kazi hizo au kutokuwa na tija linganifu wala ufanifu na ufanisi. Ni vizuri viongozi na mameneja wetu walielewe hili na wajipime na kuona kama kweli wanafanya kile ambacho kiongozi au meneja anachotakiwa kukifanya na sio kufanya anayoweza kufanya karani au tarishi. Kama sio waziri au mbunge au mkuu wa mkoa kama sio mkuu wa wilaya.
Tujiulize ni nini nafasi ya jamii katika ufumbuzi wa tatizo la umeme nchini Tanzania. Hivi leo, Benki ya dunia inamwaga misaada kwa ajili ya uanzishwaji wa miradi mbalimbali ya kijamii, jambo linaloashiria uwezekano wa kushirikiana na benki hiyo kuziwezesha jamii mbalimbali kuja na mawazo na mapendekezo kuhusiana na jinsi wanajamii wenyewe wanavyoweza kuchangia katika uzalishaji umeme nchini bila ya kutegemea sana wawekezaji toka nje. Maana wawekezaji hawaji kujenga miundombinu bali kuwekeza katika biashara au uzalishaji mali kwenye eneo walilojikita. Mjenzi wa miundombinu yetu ni lazima awe Mtanzania mwenyewe, mwanajamii katika jamii husika.
Wanajamii wa maeneo mbalimbali nchini hivi leo wanasita kujiunga na shughuli yoyote inayonukia ujamaaujamaa au ushirka ushrika kwani dhana hizo zilichakachuliwa vibaya mno na viongozi waliokuwa chini ya Mwalimu Nyerere. Ni yeye tu inaelekea alikuwa na nia safi na nzuri ya kubadili maisha ya Watanzania na sio wengine, na kama walikuwepo walikuwa wachache sana na walisakamwa kupita kiasi na mafisadi na walilia ubepari wa wakati huo.
Ni vyema pia kuzijua njia mbalimbali za kuzalisha umeme. Kisha kuainisha ni ipi au zipi ambazo zinaweza katika muda mfupi kutupa nafuu katika tatizo hili na zile ambazo zinahitaji muda na uwekezaji mkubwa zaidi.
Ziko njia mbalimbali za kuzalsha umeme zinazojulikana kufikia sasa. Njia hizo ni pamoja na mchakato wa nyuklia; samadi na takataka mbalimbali; mvuke; mashamba ya umeme wa solar; mashamba ya umeme wa upepo; mafuta ya petroli au dizeli na maji.
Tanzania inasemekana haijafikia hali ya kujitosheleza kiuwezo na kiusalama kuzalisha umeme kwa mchakato wa uranium ijapo tumejaliwa madini hayo. Kwa hiyo, hii sio njia ya kutusaidia katika siku za karibu.
Umeme kwa maji ndio huo ambao unatuongezea umaskini, maafa na dhiki zisizokweisha.
Nao huu unaweza kurudia hali yake ya kawaida endapo mipango yetu ya uoteshai miti, utunzaji mazingira na vilivyomo na hususan kwenye maeneo ya vyanzo vya maji milimani au chini ardhini itafanikishwa.
Uzalishaji umeme kwa kutumia samadi na takataka mbalimbali; upepo; mafuta ya petroli au dizeli ndio njia zinazoweza kuchangia haraka zaidi kumaliza tatizo hili.
Kwa jiji kama Dar es salaam uzalishaji umeme kwa kutumia takataka ni kitu kinachowezekana. Na njia hii itaua ndege wawili kwa jiwe moja. Kwanza, utaongeza megawati za umeme kwenye mtandoa wa umeme na pili utafanya jiji hili kuwa safi daima.
Mashamba ya umeme wa solar na upepo kwenye mikoa yenye jua na upepo wa kutosha yanaweza kuchangia gridi ya taifa kwa megawati kadhaa.
Kwenye miji na wilaya ambazo zina upepo wa kutosha ni dhahiri tukishirikiana na nchi kama Denmark na Netherlands tunaweza kupata 'shortcut' za kupata mitambo na vifaa vinavyohitaji na kuzalisha umeme chini ya mwaka mmoja.
Umeme wa jenereta zinazotuchafulia hali ya hewa, mazingira na kutupigia makelele unastahili kudhibitiwa na kuvumuliwa tu kutokana na ukweli kuwa hakuna ujanja mwingine.
Mitaani ili tusichafue zaidi hali ya hewa ni vyema maduka au makampuni kadhaa yakaungana na kununua jenereta kubwa zinazoweza kutosheleza maduka au makampuni yote yaliyo sehemu hiyo badala ya kila mmoja kuwa na kijenereta chake na hivyo kusababisha uchafuzi mkubwa wa mazingira kwa moshi, kelele na hewa ya carbon monoxide.
Inafaa pia kuuliza kama nchi zilizotuzunguka, yaani, Msumbiji, Malawi, Zambia, Kongo Kinshasa, Rwanda (ambayo imefanya kazi nzuri sana katika upatikanaji umeme kwa watu wake), Burundi, Uganda na Kenya zina hali gani kiumeme na tunaweza kushirikiana nazo vipi ili tuzalishe umeme kwa pamoja utakaotusaidia sote kupunguza au kumaliza kabisa tatizo letu la umeme.
Maana tatizo letu kama nchi nyingi za Kiafrika ni lile la kushindwa kuwa na miundo na mifumo inayofanya kazi kwa sababu mbalimbali zikiwemo zile za nchi kuongozwa kwa kufuata mipango, ahadi na misaada kutoka nje. Na kushindwa kabisa kujikwanyua toka kwenye makucha ya ubepari mamboleo, matapeli wa kimataifa na mabwana wa watwana. Uongozi wowote unaojenga tabia ya ombaomba, hujenga nchi ya ombaomba. Nyumba au uongozi wowote unaojivuna na unaothamini watu wake kikwelikweli hukataa kujenga tabia ya ombaomba. Watazame ombaomba mitaani Dar es salaam na familia zao ujiulize kama watu hawa kweli wanaweza kuja kubadilika baadaye. Haiwezekani. Badala yake ,hujenga tabia ya kupenda kujitegemea, kukinaishwa na kusaidiwa na kujivunia kama wenzetu wa Korea ya Kaskazini walivyofanya kunako miaka ya 1950 pale walipotengeneza trekta lao wenyewe la kwanza na badala ya kwenda mbele, gia zote zikawa ni za rivasi tu.
Kiongozi yeyote anayewadharau raia wake: kwa kuwaita wavivu, wezi, wategaji, wababaishaji atambue sio raia wake wenye tatizo bali ni yeye mwenye tatizo. Kwa kifupi, mdharau chake na kuthamini wengine na vya wengine hawezi kamwe kuwa kiongozi wa kutumaniwa wala kutegemewa kuleta mabadiliko ya kimsingi katika jamii husika. China au Korea Kusini au Brazl au India au Malaysia -ingelifanya hivyo, isingekua hapo ilipo leo.
Kuwathamini kupindukia watu toka nje na kutowathmini ipasavyo raia wako mwenyewe ni mwanzo wa jengo la nchi lisilo na msingi madhubuti.
Haya ni mambo yaliyotufikisha hapa tulipo ambapo leo pamoja na kuwa na wasomi wa masuala ya umeme na nishati, hawatumiki kwa ajili hiyo, na wanaofanya maamuzi juu ya masulala hayo ni wanasiasa ambao bila shaka ni mbumbumbu katika masuala hayo na uelewa wao unategemea maelezo wanayopata kutoka kwa wanaojua wanachokizungumza.
Aidha, kutokana na hayo hapo juu imekuwa vigumu kwetu kupambanua kati ya yale ambayo tunatakiwa tuyafanye sisi wenyewe ima-fa-ima na yale ambayo kwa sababu fulani fulani tunalazimika kuomba msaada au ushirikiano toka kwa wengine.
Hakuna asiyetambua kwamba, ili tuendelee nchi yetu inahitaji : chakula, maji; hewa safi; mazinigira salama; afya bora na usalama kwa watu wetu; umeme au nishati mbadala; reli ya kisasa; barabara zinazopitika bila usumbufu wakati wote; makazi bora kwa watu; usafiri wa anga na majini; masoko yanayofikika ndani na nje ya nchi; ushauri mzuri kwa waliotutangulia; utafiti na kuyaelezea kwa urahisi masuala mbalimbali ili yaeleweke na wengi nchini na elimu inayosaidia kutatua matatizo yetu au kutumia fursa za maendeleo zilizopo ndani ya mipaka yetu na nje ya mipaka yetu.
Tujihusishe na hili suala la umeme tu na hayo mengine tuyaache hadi wakati mwingine. Inshallah. Kuna vitu ambavyo 'piga-ua' ni lazima Watanzania waiunde au watengeneze wao wenyewe kwa kutumia watu wetu waliosoma na wasiosoma ili mradi ni wabunifu, watundu na wanaoweza kujaribu bila kukatishwa tamaa na kushindwa katika maisha yao yote. Hata wakishindwa mara ngapi! Na mimi siamini kama tukiwatumia wasomi wetu, wataalamu wetu, mameneja wetu, wanajeshi wetu na vijana wetu kikamilifu tuna sababu ya kushindwa zaidi ya mara mbili tatu tu! Tunashindwa kwa sababu hatuwatumii watu wetu ipasavyo! Tunashindwa kwa sababu wanasiasa wetu wamejifanya pia wao ndio wataalamu na magwiji wa uchumi na maendeleo ya jamii.
Lakini kama tutawatumia maprofesa wetu wa vyuo vikuu na wanafunzi wao katika taaluma ya umeme na nishati sio tu tunaweza kupata ufumbuzi wa muda mfupi bali wa kudumu wa matatizo yetu.
Ni kitu cha kuhuzunisha kuwa pengine kutokana na viongozi wetu wa vyuo vikuu kujikita zaidi kwenye siasa badala ya uchumi na uzalishaji mali, mahala kama Chuo Kikuu cha Dar es salaam, chenye idara ya Uhandisi wa umeme hakina mifano yoyote inayofanya kazi kama vile mashamba ya upepo wa umeme au ya solar energy au uzalishaji umeme kwa njia nyingine mikoani - na inayoweza kulipiwa na kufadhalilwa na kupanuliwa kukidhi mahitaji yetu ya umeme.
Msiba mmoja mkubwa kwa taifa letu ni lile la kuwa na elimu na wasomi wanaojengwa ili na wao kutegemea vitu na mitambo inayozalishwa nje kwa maendeleo ya watu na nchi yetu.
Ni kwa njia hii tu ndiyo tutaweza kupata maendeleo ya kweli, ya kudumu na endelevu na sio kwa kutegemea kila kitu kitoke kwa wengine.
Vitu hivyo ni pamoja na mashine na mitambo kwa ajili ya uzalishaji umeme; utekaji, uvutaji na usmbazaji na umwagiliaji maji; uchimbaji madini; ujenzi wa bandari; ujenzi wa reli; ujenzi wa viwanja vya ndege; ujenzi wa barabara; ujenzi wa madaraja; miundombinu ya mawasiliano; na zana au vifaa mbalimbali vinavyohitajika katika ujenzi wa majengo na makazi katika nchi.
Msingi wa nchi yoyote usipoanzia katika mambo hayo hapo juu, nchi haiwezi kamwe kuuacha umaskini, achilia kuwa na maendeleo endelevu. Mpango na mkakati wowote unaoshindwa kuibua mambo haya, kisha kuyatafakari, kuyainisha na kuyapa kipaumbele katika maendeleo ya nchi ni mpango au mkakati unaofaa kutupwa jalalani pindi unapogundulika kwamba upo na unagharamiwa na kodi za wananchi. Ni mpango unaoihukumu nchi kubaki kwenye makucha ya wakoloni, mabepari na mabeberu kwa faida zao na wala sio kwa faida ya nchi na watu wake. Ni mapango unaowalazimisha watu wa nchi fulani wawe ombaomba, huku rasilimali za nchi zikichotwa kwenda kuwafanya watoa sadaka matajiri na matajiri zaidi. Ni mpango na mkakati unaomfanya raia wa nchi hii kuwa mtumwa wa wakoloni wa zamani na vibarakala wao na utandawazi na mumiani wake.
Kwa maneno mengine matatizo yetu mengi, likiwemo hilo la umeme ni matatizo yanayoweza kupatiwa ufumbuzi wa haraka na kudumu kwa kutumia vyema rasilimali watu yetu na rasimali watu toka nje pamoja na matumizi sahihi ya rasilimali zetu nyingine.
Hili linaweza kufaulu tu katika nchi ambayo haijvunii na haiwalindi mafisadi kama sehemu ya uongozi wake; inayotambua maendeleo yetu kama rasilimali zetu zinatumika vizuri, yanaweza kugharamiwa na watakaopata ujuzi na uzoefu katika mipango yetu mbalimbali ya maendeleo nchini, wakati watakapokwenda kuwafanyia Waafrika wengine kazi kama hii. Fisadi wa Kitanzania, ni mwizi anayejiibia shati lake mwenyewe. Fisadi wa kimataifa, haibi cha ndani, hukwapua cha nje kuja kuwafaa wenzake walio nyumbani na sio vinginevyo. Na uwezo wa kutajirika kwa kutumia rasilimali za wengine, ikiwa ni pamoja na umeme, kutokana na nchi zinazotuzunguka Watanzania tunao, isipokuwa hatuna uongozi unaoona wala kuelewa hili.
Vilevile, hili huweza kufanyika tu katika nchi ambayo chama tawala hakiendeshi nchi kana kwamba ni wabunge wake tu na wanachama wake wenye uwezo wa kuwa mawaziri, wakuu wa mikoa, wakuu wa wilaya, makatibu wakuu, wakurugenzi, mamaneja, majaji, mabalozi na wafanyakazi nchi za nje na wasimamizi wa taasisi mbalimbali. Bali kinaendesha nchi kwa kutumia akili, uwezo na michango ya Watanzania wote bila kujali ni wafuasi wa chama tawala au la.
Miaka hamsini baada ya Uhuru dunia imeipa fursa kubwa nchi yetu ya kuchagua na kuwakaribisha wataalamu tofauti toka sehemu mbalimbali duniani wenye ujuzi na uzoefu wa kila aina kuanzia watengnenezaji baiskeli hadi waunda satelaiti na roketi. Hawa ni binadamu wenzetu amabo leo ni 'jobless' pamoja na utaalamu au elimu na uzoefu wao, walioko huko Marekani, Ulaya Magharibi, Ulaya Mashariki, Marekani ya Kusini na Asia. Watu ambao tukiwapatia nyumba, gari na mshahara wa kukidhi mahitaji yao ya msingi wapo tayari kuja nchini hapa kusaidiana na sisi kuifanya nchi yetu iendelee kwa kasi na haraka zaidi. Kinachotakiwa ni kutambua hili na kujipanga kulishughulikia kwa namna ambayo litakuwa ni la faida kwetu sote, kwao na sisi kadhalika. Ni rahisi, kulizungumza hili kwa maneno, lakini ukweli ni kwmba kwa uoga, uziwi na upofu wa viongozi wetu hususan kuhusiana na yale yanayoandikwa na magazeti ni GUMU KAMA GAMBA LA KOBE.
Ila kwa bahati nzuri, kutokana na kukua kwa demokrasia nchini hapa upo uwezekano kwamba hili likifumbiwa macho na watawala, haliwezi kuachwa kuokotwa na wapinzani na wanaharakati wengine wenye mapenzi ya dhati ya nchi yao na uchungu na umasikini wa wananchi wenzao.
Katika miaka hii ambayo hali ya hewa inaendelea kubadilika na hatuna ahadi wala uhakika na mvua na kwa hiyo maji yanayotiririka katika mito na mabwawa tuliyoandaa kuzalisha umeme ni makosa makubwa kuendelea kutegemea umeme wa tabaini zinazoendeshwa na maji.
Hali yetu kama nchi sasa ni afadhali ukilinganisha na Somalia. Lakini upo uwezekano mkubwa wa ukame ulioikumba nchi hii iliyo kaskazini ya Tanzania na Kenya pia kuikumba nchi yetu.
Kutokana na ukweli huu, wale wanaoshika nafasi za uongozi nchini wanapaswa kuona mbali na mbele zaidi kuliko mwananchi wa kawaida.
Tatizo letu kwa hiyo siyo tu tatizo la ukame na kukosa mvua na maji ya kuzalisha umeme bali pia ni upungufu wa mipango na mikakati ya upatikanaji nishati ya uhakika na isiyoathirika na hali ya hewa kwa kadri inavyobadilika.
Tatizo pacha ni lile la serikali kudharau na kupuuza ushauri wa watu mbalimbali kuhusiana na muundo, kazi na nafasi ya shirka la umeme la taifa (TANESCO) katika kutafuta jawabu kamili na la kuridhisha la tatizo la umeme nchini.Shirika ambalo hivi leo limebatizwa na kuitwa 'TANZANIA ELELCTRIC SUFFOCATION COMPANY'- Ni dhahiri kwamba shirika ambalo miaka 50 baada ya uhuru limeweza kuwapatia asilimia 5 tu ya Watanzania umeme halina akili wala uwezo wa kufanya makubwa zaidi ya hayo ambayo tayari limekwishayafanya. Limefikia upeo wa uwezo na ubunifu wake.
Uendeshaji wa mashirika ya umma umefanana na ule wa mzazi ambaye alimshonea mwanaye suti akiwa na miaka 10 na leo mtoto huyo ambaye ana miaka 20 eti anatakiwa kuvaa suti ileile aliyoivaa akiwa na miaka 10. Watanzania tulikuwa milioni 9 mwaka 1960. Tuliyoyafanya wakati huo hayawezi kufanywa miaka hamsini baadaye na tukiwa takriban Watanzania milioni hamsini.
Baadhi ya watu wameshawahi shirika hilo livunjwe katika sehemu nne. Uzalishaji umeme, usambazaji umeme, utengenezaji vifaa vya umeme na uunganishaji na uhudumiaji miundo-mbinu ya umeme. Na sio lazima kufanya kazi zote hizi, bali shirika/serikali iruhusu Watanzania binafsi, wanajamii na wawekezaji kuendesha shughuli hizo kwa ufanisi na ufanifu zaidi.
Wapo pia waliopendekeza kwamba kila mkoa uwe na shirika lake la umeme, badala ya kuwa na shirika la umeme la taifa, kwa kutumia rasilimali za mkoa na ubia na wawekezaji wa ndani na nje. Hawa waliamini katika falsafa ya Schumacher kwamba 'Kidogo ni kizuri na chema zaidi,' au kwa Kiingereza: 'Small is Beautiful.' Kilal mkoa ungelitafuta chanzo chake binafsi cha uzalishaji umeme bila ya kutegemea tu maji. Hili lingeliendana pia na kifungu cha katiba kinachohusiana na kuwepo na ulinganifu katika maendeleo ya taifa-kitu ambacho kimeshindikana kabisa katika sekta hii ya nishati.
Niliposikiliza mahojiano ya Mh. Jakaya Kikwete na BBC akiwa ziarani Afrika Kusini sikuweza kuacha kuona kwamba majibu yake hayakuwa yenye kuonesha imani na matumaini kwamba tatizo la umeme liko ndani ya mikono ya Watanzania . Kilichojitokeza ni kwamba ni serikali ndiyo tu iliyokuwa ikitarajiwa kulitatua tatizo hilo. Aidha, serikali ilikuwa inapaswa kulipa fedha zote za ununuzi wa mitambo ya uzalishaji umeme papo kwa hapo. Kitu ambacho sio sahihi.
Ninaamini, Watanzania wakihamasishwa kama walivyokatwa kodi na haki zao mbalimbali ili kuanzisha mashirika ya umma (yaliyokuja kubinafsishwa bila wao kulipwa chochote) wana sababu, uwezo na nia ya kuchangia kumaliza tatizo la umeme lakini kwa sharti kuwa wanakuwa nao ni wamiliki wa mashirika yatakayoanzishwa kama sehemu ya ufumbuzi wa tatizo hili.
Vilevile, watengenezaji wa mitambo ya umeme wako tayari kukodisha mitambo yao na vile vile kuuza mitambo hiyo kwa mtu kulipia kidogo kidogo hadi deni liishe.
Hata hivyo kinachoonekan hapa ni kuwa mtazamo wa ndani kwa suala hili haupo na badala yake tuna mtazamo wa nje tu. Ikiwa ni pamoja na kuamini kuwa ni lazima tupate msaada au tukope kutoka nje ili tatizo la umeme liishe hapa nchini. Au wakati mwingine, pengine ni ujanja wa kununua vikubwa vikubwa kwa gharama kubwa ili watu wapate chambele au teni pasenti yao.
Sikubaliani kabisa na wale wanaoamini kwamba tatizo la umeme limesababishwa na ufisadi na eti kuna wauza majenereta walioihona serikali ili biashara yao ya majenereta ichanganye vilivyo. Japo kuwa majenereta yanauzwa kwa fujo hivi leo, lakini adha na gharama za uendeshaji majenereta ikiwemo kwa taasisi za serikali pia, kama vile gharama za dizeli au petroli; kelele; uchafu wa mazingira; nguvu kazi ya ziada katika kuzihudumia
ni mambo yanayoitia hoja hiyo hapo juu mashakani.
Uwekezaji katika sekta hii ya umeme unawezekana kabisa kutokea ndani ya nchi. Kwa maana kwamba, kama serikali ilivyoanzisha mashirika kwa kutumia kodi za wananchi upo uwezekano wa wananchi na wawekezaji kuchangia asilimia fulani na wawekezaji wa nje wakachangia asilimia fulani. Inapendekezwa ili makampuni ya umeme yawe ni ya Watanzania basi Watanzania wamiliki asilimia 51-60 na wawekezaji toka kwingineko asilimia 40-49.
Ufumbuzi wa tatizo la umeme, hali kadhalika, utakuwa mgumu bila kufahamu mchango wa siasa katika udhairu, kudumaa na kuserereka kwa TANESCO pamoja na misaada yote ambayo shirika hili limekuwa likipata toka kwa wafadhili wa nje na malipo ya gharama kubwa za umeme kuliko nchi nyingine yoyote Afrika. Wapo wanaodai kwamba shirika hilo liligeuzwa shamba la bibi na baadhi ya wanasiasa. Kwa maneno machache, shirika hilo, halijawahi kuendeshwa kibiashara bila kuingiliwa na wanasiasa. Pamoja na mifano mingi ya uwezo mdogo wa mameneja wa Kitanzania kusimamia miradi mikubwa hazijafanyika jitihada za dhati kumpata meneja toka nje mwenye uwezo na dhati ya kutusaidia Watanzania tuondokane na tatizo hili la umeme. Netsolution, kwa kiasi kikubwa, ilikuwa ni 'dili' lililonufaisha watu binafsi na sio nchi na watu wake.
Vilevile, wanasiasa Tanzania wamejenga tabia ya kuingilia kila fani na kazi nchini na kujifanya wao ni wataalamu zaidi kuliko wataalamu wenyewe. Toka mgao huu wa umeme pamoja na kuwa na vyuo vikuu vinavyotoa shahada mbalimbali za masuala ya umeme hapajawahikuendeshwa warsha au kongamano au angalau semina yoyote iliyowashsirikisha ili michango yao kuhusu ufumbuzi wa tatizo la umeme nchini lipatikane. Hii ni kasoro kubwa sana nchi mwetu, na isipoangaliwa itatuumiza katika kila sekta na nyanja ya maendeleo kwa miaka mingi ijayo.
Kama walivyo wanafunzi wa masomo mengine, wanafunzi wa shahada za uhandisi Tanzania hawapewi fursa za kutosha kutumia elimu yao kwa utafiti na uvumbuzi kwa majibu ya matatizo yetu mbalimbali. Bajeti yetu katika kuchochea utafiti ni ndogo mno, na sidhani kuna bajeti yoyote ya kuhamasisha ubunifu na uvumbuzi nchini miongoni mwa wasomi na wasiokuwa wasomi.
Wakati vijana wa Kenya wanagundua njia mbalimbali za kuzalisha umeme ikiwemo wa kutumia magurudumu ya baiskeli, umeme kwa upepe na sasa umeme kwa chupa ya cocacola na maji, vijana wa Kitanzania wamezungushiwa kitanzi shingoni mwao kinachowatia uoga katika kuanzisha au kuunda kitu chochote kinachoweza kuwa na manufaa kwa jamii yao. Na sio suala la ujinga au kutokujua. Ni kwamba wazazi wao na serikali yao haijakaa mkao wa kudai na kupata kutoka kwa kizazi hiki kipya zaidi ya muziki wa kuiga toka Marekani au kuvaa katakei!
Kati ya vijana wasiosoma sana ni wale ambao wameshawahi kuunda redio, kompyuta, gari, ndege, helikopta, transmita za redio na kadhalika. Lakini kwa kuwa baba na mama zao sio watu wakubwa, vijana hawa wameishia kutishiwa na vyombo vya dola hadi kujenga uoga mkubwa wa kuwa wabunifu na wavumbuzi wa kitu chochote katika maisha yao yaliyobakia. Ni nani anayekosa hapa. Tanzania au mtoto anayehusika?
Hebu, chunguza wewe mwenyewe katika nchi ambayo magazeti yametoa habari za watoto au vijana waliovumbua vitu mbalimbali, je, leo hao watoto wako wapi. Wamesaidiwa au wamehujumiwa, kwa kuwa tu ni watoto wa watu wasiokuwa na uwezo?
Nchi zetu za Kiafrika zimejenga utaratibu unaowafanya wananchi waamini kwamba bila serikali matatizo yao hayawezi kutatuliwa. Serikali inaonekana kujua kila kitu,kuwa na fedha zote duniani na kuwa bila mkono au mguu wa serikali hakuna anayeweza kusogea kwenda popote. Na serikali kwa upande wake inaelekea kuamini na kudhani ndiyo peke yake yenye majibu ya matatizo yote ya kiuchumi, kijamii, kisiasa, kiutamaduni na kiteknolojia. Kitu ambacho si kweli.
Guru wa Menejimenti, Profesa Peter Drucker anasema meneja mzuri na anayefanya kazi kwelikweli, hafanyi kazi yoyote. Ndivyo ilivyo pia kwa serikali nzuri na inayofanya kazi kwelikweli. Haifanyi kazi. Tunaposema haifanyi kazi hatuna maana haifanyi chochote au inategea tu. La hasha. Meneja na serikali bora na mfano wa kuigwa hufnaya kazi kwa kupitia watu, idara na taasisi nyingine. Unapoingilia kufanya kazi za watu wengine, idara na taasisi nyingine badla aya wao kuzifanya wenyewe kuna uwezekano mkubwa wa wewe kuvuruga kazi hizo au kutokuwa na tija linganifu wala ufanifu na ufanisi. Ni vizuri viongozi na mameneja wetu walielewe hili na wajipime na kuona kama kweli wanafanya kile ambacho kiongozi au meneja anachotakiwa kukifanya na sio kufanya anayoweza kufanya karani au tarishi. Kama sio waziri au mbunge au mkuu wa mkoa kama sio mkuu wa wilaya.
Tujiulize ni nini nafasi ya jamii katika ufumbuzi wa tatizo la umeme nchini Tanzania. Hivi leo, Benki ya dunia inamwaga misaada kwa ajili ya uanzishwaji wa miradi mbalimbali ya kijamii, jambo linaloashiria uwezekano wa kushirikiana na benki hiyo kuziwezesha jamii mbalimbali kuja na mawazo na mapendekezo kuhusiana na jinsi wanajamii wenyewe wanavyoweza kuchangia katika uzalishaji umeme nchini bila ya kutegemea sana wawekezaji toka nje. Maana wawekezaji hawaji kujenga miundombinu bali kuwekeza katika biashara au uzalishaji mali kwenye eneo walilojikita. Mjenzi wa miundombinu yetu ni lazima awe Mtanzania mwenyewe, mwanajamii katika jamii husika.
Wanajamii wa maeneo mbalimbali nchini hivi leo wanasita kujiunga na shughuli yoyote inayonukia ujamaaujamaa au ushirka ushrika kwani dhana hizo zilichakachuliwa vibaya mno na viongozi waliokuwa chini ya Mwalimu Nyerere. Ni yeye tu inaelekea alikuwa na nia safi na nzuri ya kubadili maisha ya Watanzania na sio wengine, na kama walikuwepo walikuwa wachache sana na walisakamwa kupita kiasi na mafisadi na walilia ubepari wa wakati huo.
Ni vyema pia kuzijua njia mbalimbali za kuzalisha umeme. Kisha kuainisha ni ipi au zipi ambazo zinaweza katika muda mfupi kutupa nafuu katika tatizo hili na zile ambazo zinahitaji muda na uwekezaji mkubwa zaidi.
Ziko njia mbalimbali za kuzalsha umeme zinazojulikana kufikia sasa. Njia hizo ni pamoja na mchakato wa nyuklia; samadi na takataka mbalimbali; mvuke; mashamba ya umeme wa solar; mashamba ya umeme wa upepo; mafuta ya petroli au dizeli na maji.
Tanzania inasemekana haijafikia hali ya kujitosheleza kiuwezo na kiusalama kuzalisha umeme kwa mchakato wa uranium ijapo tumejaliwa madini hayo. Kwa hiyo, hii sio njia ya kutusaidia katika siku za karibu.
Umeme kwa maji ndio huo ambao unatuongezea umaskini, maafa na dhiki zisizokweisha.
Nao huu unaweza kurudia hali yake ya kawaida endapo mipango yetu ya uoteshai miti, utunzaji mazingira na vilivyomo na hususan kwenye maeneo ya vyanzo vya maji milimani au chini ardhini itafanikishwa.
Uzalishaji umeme kwa kutumia samadi na takataka mbalimbali; upepo; mafuta ya petroli au dizeli ndio njia zinazoweza kuchangia haraka zaidi kumaliza tatizo hili.
Kwa jiji kama Dar es salaam uzalishaji umeme kwa kutumia takataka ni kitu kinachowezekana. Na njia hii itaua ndege wawili kwa jiwe moja. Kwanza, utaongeza megawati za umeme kwenye mtandoa wa umeme na pili utafanya jiji hili kuwa safi daima.
Mashamba ya umeme wa solar na upepo kwenye mikoa yenye jua na upepo wa kutosha yanaweza kuchangia gridi ya taifa kwa megawati kadhaa.
Kwenye miji na wilaya ambazo zina upepo wa kutosha ni dhahiri tukishirikiana na nchi kama Denmark na Netherlands tunaweza kupata 'shortcut' za kupata mitambo na vifaa vinavyohitaji na kuzalisha umeme chini ya mwaka mmoja.
Umeme wa jenereta zinazotuchafulia hali ya hewa, mazingira na kutupigia makelele unastahili kudhibitiwa na kuvumuliwa tu kutokana na ukweli kuwa hakuna ujanja mwingine.
Mitaani ili tusichafue zaidi hali ya hewa ni vyema maduka au makampuni kadhaa yakaungana na kununua jenereta kubwa zinazoweza kutosheleza maduka au makampuni yote yaliyo sehemu hiyo badala ya kila mmoja kuwa na kijenereta chake na hivyo kusababisha uchafuzi mkubwa wa mazingira kwa moshi, kelele na hewa ya carbon monoxide.
Inafaa pia kuuliza kama nchi zilizotuzunguka, yaani, Msumbiji, Malawi, Zambia, Kongo Kinshasa, Rwanda (ambayo imefanya kazi nzuri sana katika upatikanaji umeme kwa watu wake), Burundi, Uganda na Kenya zina hali gani kiumeme na tunaweza kushirikiana nazo vipi ili tuzalishe umeme kwa pamoja utakaotusaidia sote kupunguza au kumaliza kabisa tatizo letu la umeme.
Sunday, March 27, 2011
Ajali, fidia na Mtanzania
Ajali, fidia na Mtanzania
NI wakati kama huu wa ajali ndipo Watanzania wengi wanapotambua kwamba sio tu hawana kinga dhidi ya ajali lakini pia baada ya ajali kutokea wanaweza wasipate msaada wa maana kuendelea na maisha yao.
Watetezi wa umma, hata hivyo, huu ndio wakati wa kuingilia kati na kujaribu kuubadili mfumo uliopo ili uangalie pia maslahi ya wanyonge na wasio nacho katika jamii.
Wenye nacho na walioko madarakani hawana sababu ya kuwapenda wanaotetea maslahi ya walio wengi. Lakini vile vile watetezi wa umma hawana sababu ya kuwaogopa wenye nacho na walioko madarakani katika kutetea haki za wanyonge. Huu ni wito na sio kazi ya kutafuta cheo au ukubwa au utajiri.
Mfumo uliopo
Mfumo wa bima na fidia uliopo hivi sasa umejengwa katika mihimili ya kuwasaidia walionacho na wakubwa.
Mnyonge hana nafasi katika mfumo huu. Ukitaka ushahidi nenda kawahoji walioathirika na ajali kama zile za MV Bukoba, ajali mbalimbali za mabasi na majini nchini kwa miaka tuseme saba tu iliyopita. Kadhalika kawahoji watu wa Merelani kwa matukio mawili matatu na usikie fidia waliyopata.
Ukitoka hapo kaangalie upande wa pili na mahesabu ya mashirika ya bima kuhusu ajali zilizowahusu walionacho na wenye nchi.
Baada ya maswali na udadisi huo utagundua kuwa mfumo wa bima na fidia upo kwa ajili ya tabaka fulani tu katika jamii na sio kwa umma wote.
Swali linakuja. Je, huu ndio mfumo nchi kama yetu yenye asili ya kijamaa unaostahili kuwa nao? Kweli kuna sababu ya kuruhusu mfumo huu uendelee au kwa maneno mengine kwanini mfumo huu bado unalindwa? Je, maslahi ya wengi yakiangaliwa yale ya wachache yatapotea?
Kama mabadiliko yanahitajika, je, nchi hii inahitaji mfumo gani wa bima na fidia kwa faida ya umma?
Mashirika ya umma na fidia
Eti kwa kuwa TANESCO, DAWASA, TRC, ATC na mashirika mengine enzi hizo yalikuwa ya umma ilikuwa haiyumkiniki mtu kufidiwa kitu.
Si mnakumbuka wale ambao friji, TV, redio na vyombo vyenu vingine vya nyumbani vilivyoharibiwa na umeme wa TANESCO? Wangapi kati yenu walilipwa fidia?
Treni hadi leo ikisababisha ajali hata kama ni kwa uzembe wa shirika husika eti ni wewe mpita njia ndiye unayewajibika na sio wao. Makubwa haya jama.
Pamoja na haya yote ni kwamba hakuna shirika linalowajibishwa hapa nchini hivi sasa kwa kushindwa kutimiza upande wake wa mkataba iwe ni kutoa huduma au kuuza bidhaa mbovu kwa wananchi.
Mtanzania kwa kifupi hana haki kabisa dhidi ya mashirika yanayotakiwa kumpatia bidhaa au huduma. Yakimpatia huduma au bidhaa safi na bora sawa. Yakitoa huduma ovyo na bidhaa zilizooza sawa! Hataweza kuyashtaki na kuambulia chochote katika mfumo uliopo.
Sheria na udhibiti wa uzembe
Ieleweke kuwa kazi mojawapo ya sheria na katiba ya nchi yoyote ile ni kulinda raia na mali zao. Sheria na katiba inayoshindwa kufanya hili inakuwa na walakini.
Vyombo vya sheria vina jukumu sio tu la kuona kuna sheria fulani lakini kuhakikisha kuwa sheria hizo zinakwenda na wakati na zinatimiza yale ambayo katika macho ya jamii ni haki na wajibu.
Mojawapo kati ya mambo hayo ni kuona kuwa raia na wasio raia wanapata fidia maridhawa pale wanapofikwa na janga lolote nyumbani, kazini au safarini. Jingine ni kuhakikisha kuwa sheria inatumika kama kinga dhidi ya ulegevu na uzembe unaoweza kusababisha kifo au mtu kuwa kilema maisha yake yote.
Kifo kinapomkuta, kwa mfano, msafiri wa treni ina maana kuna familia na hasa watoto watakaokosa baba au mama. Je, ni nani atawalea hawa? Sheria ina haki kunyamaza kuhusu hili?
Jamaa huyo huyo anaweza akawa pia alikuwa akitegemewa na wazazi wake-baba, mama na pengine kwa mila zetu za Kiafrika-babu na bibi. Na pengine baba huyo ndio wale jamaa waliostaafishwa na jumuia ya Afrika Mashariki na kulipwa sh. 320 kama mafao. Ni nani atawatunza wazee hawa? Sheria inaliona hili?
Katika kujadili masuala kama haya ni wazi kuwa hatma ya yote itaonekana kuwa Tanzania haina mfumo wa bima na fidia unaoweza kuwalinda Watanzania walio wengi wakati wa maafa ya aina yoyote ile.
Kwa mantiki hii kazi iliyobaki ni kwa vyombo vya sheria vikipata changamoto kutoka vikundi vya hiari na taasisi nyingine zinazotetea maslahi ya wanyonge kuhakikisha nchi inakuwa na sheria zitakazowesha kuwa na jamii na uchumi usiotetereshwa na maafa na majanga.
Aidha ni muhimu kuwa na mfumo unaolinda nchi na watu wake dhidi ya uzembe wa wenye mali.
Kwa mfano, hivi kuna ugumu gani kuwa na sheria itakayotaka familia ifidiwe shilingi milioni 5 -10 kwa kupoteza jamaa yao? Fidia ya milioni 1-2 kwa mtu kuvunjika mguu?
Je, kwa namna hii kuna dereva, meneja au mwenye gari au chombo cha usafiri atakayecheza na maisha ya watu.
Kwa mantiki hii kama inaonekana uzembe ulifanyika na kisha kusababisha ajali basi fidia inaweza kuwa mara mbili au zaidi ya hapo.
Fidia ni njia pekee inayoweza kuwasaidia watoto na wajukuu wanaobaki bila mtafuta riziki wake. Fidia ni njia pekee inayoweza kuwasaidia wazazi waliozeeka wanaoachwa bila mtu wa kuwasaidia.
Fidia ni njia pekee inayoweza kumsaidia mtu anayefanywa kilema katika ajali fulani aweze kujitegemea kimaisha. Kukiwa na mfumo wa bima na fidia unaowezesha hayo hapo juu ni dhahiri kuwa nchi itanufaika pia kiuchumi.
Kutokana na kuzungusha upya pato la nchi linalokwenda aghalabu zaidi kwa wachache basi kunakuwa na msukumo mkubwa zaidi wa uzalishaji mali utakaonufaisha sehemu mpya na sio zile za asili tu.
Ulaya, Marekani na fidia
Ingawa Tanzania haiwezi kuwa kama Marekani na Ulaya katika masuala ya bima na fidia ni muhimu hata hivyo kujifunza falsafa iliyowafanya waheshimu na kuendeleza mfumo wa sheria unaowanufaisha watu wanaoathirika kwa maafa mbalimbali.
Anayeumia kidole kazini, kwa mfano, huko Ulaya au Marekani anaweza akajikuta ametajirika fumba na kufumbua.
Watoto na wazazi wanaowategemea wengine huwa hawaambulii patupu wanapompoteza mtafutaji wao katika ajali iliyosababishwa na uzembe wa wengine na pengine hata maafa yalio nje ya kazi za binadamu. Kwa mfano moto unaochanja mbuga huko Texas hivi sasa. Hakuna aliyeusababisha lakini wote waliopoteza makazi yao huko wanaweza kuja kufidiwa kwa namna moja au nyingine.
Huu ni mfumo kwa kweli unaowapa watu imani na nchi yao, wananchi wenzao na serikali yao. Nadharia yake sio ngeni katika masikio yetu. Miaka kadhaa iliyopita Mwalimu J.K. Nyerere katika Ujamaa wa Kiafrika alilizungumzia hili.
Kama jamii ya wakati huo iliweza kumpa msaada mtu na kumwezesha kurejea maisha yake ya zamani kwa kiasi fulani kwanini leo nchi na taasisi zake za fedha ishindwe kuiga mfano huu unaotokana na mila na utamaduni wetu?
Bima ya umma
Ni dhahiri kuwa hakuna mwenye basi, mwenye meli au ndege atakayesumbuliwa na suala hili la bima na fidia kwa wanaofikwa na balaa wakisafiri katika vyombo vyao.
Huu ndio ukweli wa binadamu na mali yake. Hujali mali yake zaidi kuliko maisha ya watu wengine. Kama ndivyo, je, sio jukumu la serikali ya watu kuingilia kati hapa.
Ninapendekeza kuwa kwa kila abiria anayesafiri na basi, meli, ndege serikali itoze sh. 100 tu kuanzisha mfuko wa Bima dhidi ya ajali za vyombo vya usafiri.
Tusiwasumbue wenye vyombo vya usafiri katika hili. Njia rahisi ni kukadiria kuwa kwa mwezi chombo fulani, mathalan, treni ya TRC inabeba abiria elfu ishirini na TRC wanastahili kulipa shilingi laki mbili kwa mwezi. Iwe vivyo hivyo kwa mabasi na ndege.
Wakati wa fidia mwenye chombo atalipa nusu ya fidia na nusu iliyobaki italipwa na mfuko huu kwa fidia yoyote itakayoamuliwa. Kazi kwenu wawakilishi wa umma Dodoma kuchambua pendekezo hili.
Tume za maafa na faida zake
Vyombo vya habari ndani na nje za nchi inaelekea havioni umuhimu wa Tume zinazoanzishwa kuchunguza maafa kama haya ya juzi na jana. Yaani Merelani na Dodoma. Kwa upande mwingine, hata hivyo, kama Tume ya Ajali ya Treni Dodoma itashughulikia na masuala yatakayochangia pia kuubadili mfumo wa bima na fidia kama njia ya kudhibiti ajali zinazotokana na uzembe ingefaa iungwe mkono. Vinginevyo, fedha itakayoliwa na wajumbe hao wapewe wafiwa na mejeruhi.
NI wakati kama huu wa ajali ndipo Watanzania wengi wanapotambua kwamba sio tu hawana kinga dhidi ya ajali lakini pia baada ya ajali kutokea wanaweza wasipate msaada wa maana kuendelea na maisha yao.
Watetezi wa umma, hata hivyo, huu ndio wakati wa kuingilia kati na kujaribu kuubadili mfumo uliopo ili uangalie pia maslahi ya wanyonge na wasio nacho katika jamii.
Wenye nacho na walioko madarakani hawana sababu ya kuwapenda wanaotetea maslahi ya walio wengi. Lakini vile vile watetezi wa umma hawana sababu ya kuwaogopa wenye nacho na walioko madarakani katika kutetea haki za wanyonge. Huu ni wito na sio kazi ya kutafuta cheo au ukubwa au utajiri.
Mfumo uliopo
Mfumo wa bima na fidia uliopo hivi sasa umejengwa katika mihimili ya kuwasaidia walionacho na wakubwa.
Mnyonge hana nafasi katika mfumo huu. Ukitaka ushahidi nenda kawahoji walioathirika na ajali kama zile za MV Bukoba, ajali mbalimbali za mabasi na majini nchini kwa miaka tuseme saba tu iliyopita. Kadhalika kawahoji watu wa Merelani kwa matukio mawili matatu na usikie fidia waliyopata.
Ukitoka hapo kaangalie upande wa pili na mahesabu ya mashirika ya bima kuhusu ajali zilizowahusu walionacho na wenye nchi.
Baada ya maswali na udadisi huo utagundua kuwa mfumo wa bima na fidia upo kwa ajili ya tabaka fulani tu katika jamii na sio kwa umma wote.
Swali linakuja. Je, huu ndio mfumo nchi kama yetu yenye asili ya kijamaa unaostahili kuwa nao? Kweli kuna sababu ya kuruhusu mfumo huu uendelee au kwa maneno mengine kwanini mfumo huu bado unalindwa? Je, maslahi ya wengi yakiangaliwa yale ya wachache yatapotea?
Kama mabadiliko yanahitajika, je, nchi hii inahitaji mfumo gani wa bima na fidia kwa faida ya umma?
Mashirika ya umma na fidia
Eti kwa kuwa TANESCO, DAWASA, TRC, ATC na mashirika mengine enzi hizo yalikuwa ya umma ilikuwa haiyumkiniki mtu kufidiwa kitu.
Si mnakumbuka wale ambao friji, TV, redio na vyombo vyenu vingine vya nyumbani vilivyoharibiwa na umeme wa TANESCO? Wangapi kati yenu walilipwa fidia?
Treni hadi leo ikisababisha ajali hata kama ni kwa uzembe wa shirika husika eti ni wewe mpita njia ndiye unayewajibika na sio wao. Makubwa haya jama.
Pamoja na haya yote ni kwamba hakuna shirika linalowajibishwa hapa nchini hivi sasa kwa kushindwa kutimiza upande wake wa mkataba iwe ni kutoa huduma au kuuza bidhaa mbovu kwa wananchi.
Mtanzania kwa kifupi hana haki kabisa dhidi ya mashirika yanayotakiwa kumpatia bidhaa au huduma. Yakimpatia huduma au bidhaa safi na bora sawa. Yakitoa huduma ovyo na bidhaa zilizooza sawa! Hataweza kuyashtaki na kuambulia chochote katika mfumo uliopo.
Sheria na udhibiti wa uzembe
Ieleweke kuwa kazi mojawapo ya sheria na katiba ya nchi yoyote ile ni kulinda raia na mali zao. Sheria na katiba inayoshindwa kufanya hili inakuwa na walakini.
Vyombo vya sheria vina jukumu sio tu la kuona kuna sheria fulani lakini kuhakikisha kuwa sheria hizo zinakwenda na wakati na zinatimiza yale ambayo katika macho ya jamii ni haki na wajibu.
Mojawapo kati ya mambo hayo ni kuona kuwa raia na wasio raia wanapata fidia maridhawa pale wanapofikwa na janga lolote nyumbani, kazini au safarini. Jingine ni kuhakikisha kuwa sheria inatumika kama kinga dhidi ya ulegevu na uzembe unaoweza kusababisha kifo au mtu kuwa kilema maisha yake yote.
Kifo kinapomkuta, kwa mfano, msafiri wa treni ina maana kuna familia na hasa watoto watakaokosa baba au mama. Je, ni nani atawalea hawa? Sheria ina haki kunyamaza kuhusu hili?
Jamaa huyo huyo anaweza akawa pia alikuwa akitegemewa na wazazi wake-baba, mama na pengine kwa mila zetu za Kiafrika-babu na bibi. Na pengine baba huyo ndio wale jamaa waliostaafishwa na jumuia ya Afrika Mashariki na kulipwa sh. 320 kama mafao. Ni nani atawatunza wazee hawa? Sheria inaliona hili?
Katika kujadili masuala kama haya ni wazi kuwa hatma ya yote itaonekana kuwa Tanzania haina mfumo wa bima na fidia unaoweza kuwalinda Watanzania walio wengi wakati wa maafa ya aina yoyote ile.
Kwa mantiki hii kazi iliyobaki ni kwa vyombo vya sheria vikipata changamoto kutoka vikundi vya hiari na taasisi nyingine zinazotetea maslahi ya wanyonge kuhakikisha nchi inakuwa na sheria zitakazowesha kuwa na jamii na uchumi usiotetereshwa na maafa na majanga.
Aidha ni muhimu kuwa na mfumo unaolinda nchi na watu wake dhidi ya uzembe wa wenye mali.
Kwa mfano, hivi kuna ugumu gani kuwa na sheria itakayotaka familia ifidiwe shilingi milioni 5 -10 kwa kupoteza jamaa yao? Fidia ya milioni 1-2 kwa mtu kuvunjika mguu?
Je, kwa namna hii kuna dereva, meneja au mwenye gari au chombo cha usafiri atakayecheza na maisha ya watu.
Kwa mantiki hii kama inaonekana uzembe ulifanyika na kisha kusababisha ajali basi fidia inaweza kuwa mara mbili au zaidi ya hapo.
Fidia ni njia pekee inayoweza kuwasaidia watoto na wajukuu wanaobaki bila mtafuta riziki wake. Fidia ni njia pekee inayoweza kuwasaidia wazazi waliozeeka wanaoachwa bila mtu wa kuwasaidia.
Fidia ni njia pekee inayoweza kumsaidia mtu anayefanywa kilema katika ajali fulani aweze kujitegemea kimaisha. Kukiwa na mfumo wa bima na fidia unaowezesha hayo hapo juu ni dhahiri kuwa nchi itanufaika pia kiuchumi.
Kutokana na kuzungusha upya pato la nchi linalokwenda aghalabu zaidi kwa wachache basi kunakuwa na msukumo mkubwa zaidi wa uzalishaji mali utakaonufaisha sehemu mpya na sio zile za asili tu.
Ulaya, Marekani na fidia
Ingawa Tanzania haiwezi kuwa kama Marekani na Ulaya katika masuala ya bima na fidia ni muhimu hata hivyo kujifunza falsafa iliyowafanya waheshimu na kuendeleza mfumo wa sheria unaowanufaisha watu wanaoathirika kwa maafa mbalimbali.
Anayeumia kidole kazini, kwa mfano, huko Ulaya au Marekani anaweza akajikuta ametajirika fumba na kufumbua.
Watoto na wazazi wanaowategemea wengine huwa hawaambulii patupu wanapompoteza mtafutaji wao katika ajali iliyosababishwa na uzembe wa wengine na pengine hata maafa yalio nje ya kazi za binadamu. Kwa mfano moto unaochanja mbuga huko Texas hivi sasa. Hakuna aliyeusababisha lakini wote waliopoteza makazi yao huko wanaweza kuja kufidiwa kwa namna moja au nyingine.
Huu ni mfumo kwa kweli unaowapa watu imani na nchi yao, wananchi wenzao na serikali yao. Nadharia yake sio ngeni katika masikio yetu. Miaka kadhaa iliyopita Mwalimu J.K. Nyerere katika Ujamaa wa Kiafrika alilizungumzia hili.
Kama jamii ya wakati huo iliweza kumpa msaada mtu na kumwezesha kurejea maisha yake ya zamani kwa kiasi fulani kwanini leo nchi na taasisi zake za fedha ishindwe kuiga mfano huu unaotokana na mila na utamaduni wetu?
Bima ya umma
Ni dhahiri kuwa hakuna mwenye basi, mwenye meli au ndege atakayesumbuliwa na suala hili la bima na fidia kwa wanaofikwa na balaa wakisafiri katika vyombo vyao.
Huu ndio ukweli wa binadamu na mali yake. Hujali mali yake zaidi kuliko maisha ya watu wengine. Kama ndivyo, je, sio jukumu la serikali ya watu kuingilia kati hapa.
Ninapendekeza kuwa kwa kila abiria anayesafiri na basi, meli, ndege serikali itoze sh. 100 tu kuanzisha mfuko wa Bima dhidi ya ajali za vyombo vya usafiri.
Tusiwasumbue wenye vyombo vya usafiri katika hili. Njia rahisi ni kukadiria kuwa kwa mwezi chombo fulani, mathalan, treni ya TRC inabeba abiria elfu ishirini na TRC wanastahili kulipa shilingi laki mbili kwa mwezi. Iwe vivyo hivyo kwa mabasi na ndege.
Wakati wa fidia mwenye chombo atalipa nusu ya fidia na nusu iliyobaki italipwa na mfuko huu kwa fidia yoyote itakayoamuliwa. Kazi kwenu wawakilishi wa umma Dodoma kuchambua pendekezo hili.
Tume za maafa na faida zake
Vyombo vya habari ndani na nje za nchi inaelekea havioni umuhimu wa Tume zinazoanzishwa kuchunguza maafa kama haya ya juzi na jana. Yaani Merelani na Dodoma. Kwa upande mwingine, hata hivyo, kama Tume ya Ajali ya Treni Dodoma itashughulikia na masuala yatakayochangia pia kuubadili mfumo wa bima na fidia kama njia ya kudhibiti ajali zinazotokana na uzembe ingefaa iungwe mkono. Vinginevyo, fedha itakayoliwa na wajumbe hao wapewe wafiwa na mejeruhi.
Haki kulindwa na mahakama ya Afrika, Dunia?
Sio watu wengi wanaojua kuwa iwapo umefuata taratibu zote za mahakama katika nchi yako na hukuridhika na maamuzi ya mahakama basi unaweza kukata rufaa kwenye kamati maalum ya Umoja wa Afrika inayoshugulikia masuala ya haki za binadamu.
Kamati au tume hiyo hivi sasa iko mbioni kufanywa mahakama kama viongozi wa Afrika wataridhia suala hili kwenye mkutano wa kilele ujao kunako mwezi Juni.
Kwa mfano mjane anayeamini kuwa kanyimwa haki za kurithi mali aliyochuma na mumewe na akapeleka kesi mahakamani lakini ikatupwa nje; akakata rufaa mahakama kuu akashindwa; akakata rufaa tena mahakama ya rufaa na bado akashindwa bado atakuwa na nafasi kama hiyo tena kwenye mahakama hiyo ya Afrika.
Uanzishwaji wa Mahakama Kuu ya Afrika unakwenda sambamba na uanzishwaji wa mahakama ya Umoja wa Mataifa ambayo malengo yake bado yana shabaha ya kufanikisha vita vya haki ya binadamu duniani.
Kwa bahati mbaya sio wengi wanaojua juu ya kile kinachoendelea duniani katika ujenzi wa taasisi na taratibu zitakazohakikisha kuwa haki na usawa mbele ya vyombo vya sheria inakuwa ni ndoto ya kweli kwa kila mtu popote pale alipo duniani.
Hali ilivyo sasa ni kuwa anaweza kuibuka mtu mahala popote pale duniani na kwa kutumia nafasi yake ya uongozi; mipaka ya kile anachoita taifa lake huru; na kwa ushirikiano na wajanja wachache akafanya uhuni mkubwa katika nchi yake ikiwamo kudhulumu watu mali zao; kujitajirisha kwa wizi au rushwa; na hata kuiuza nchi yake na raia katika nchi yake na dunia nzima kwa ujumla isiwe na lolote la kufanya kumkomesha mtu huyo.
Isitoshe yapo matukio kadhaa katika nchi mbalimbali za Kiafrika hivi sasa kuonesha kuwa baadhi ya wale walioko madarakani wanadiriki kuficha au kufukia vitendo viovu, dhuluma, uonevu au vitendo vingine vya ukiukwaji wa haki za binadamu katika milki yao.
Kwa kuwa na Mahakama Kuu ya Afrika na Dunia na pengine mahakama za rufani katika ngazi hizo pia kutaimarisha uhuru wa mahakama za nchi moja moja na kuboresha haki na usawa kwa raia wa nchi husika.
Inavyoonekana ni kuwa dunia imeona udhaifu wa taasisi za kimataifa ambazo zinakosa meno ya kikatiba na kisheria.
Hali hii imesababisha kwa baadhi ya nchi mahakimu na majaji kuonekana wanawajibika kwa viongozi waliowateua na hivyo kuzifanya mahakama kutokuwa huru.
Ubinafsi pia umejitokeza katika vyombo vya sheria kufikia kiwango cha mwenye fedha kununua haki dhidi ya mnyonge anayestahili haki hiyo.
Maadili yameshuka katika baadhi ya nchi na rushwa sio kitu kigeni katika vyombo vingi vya sheria karibu katika kila nchi Afrika. Mahakama ya Afrika na dunia zitarudisha heshima ya mahakimu na majaji popote pale kwani wale wanaokiuka maadili wataadhiriwa na ngazi za juu.
Uzuri wa Mahakama ya Afrika ni kuwa itakuwa na majaji toka nchi mbalimbali za Kiafrika na pengine hata kutoka nje ya Afrika (kutegemeana na aina ya kesi na uzoefu wa majaji husika). Kitakachopambana katika duru hizi ni ubingwa wa kuitafsiri sheria kwa mujibu wa sheria na mikataba ya kimataifa kwa lengo la kuhakikisha Waafrika wote wanakuwa sawa mbele ya sheria hizo na mwenye haki ndiye anayestahili kunufaika na sio vinginevyo.
Haki za binadamu
Waafrika na wasio Waafrika kwa muda mrefu wamekuwa wakililaumu bara hili kwa kushindwa kuheshimu haki za binadamu.
Vyombo vya dola, yaani polisi, magereza na upelelezi aghalabu vinalaumiwa kwa kukiuka haki za binadamu.
Mathalani, hali ya magereza ya Afrika ukifananisha na yale ya Ulaya au Marekani ni ya kusikitisha na kutisha. Upo uwezekano mkubwa kuwa mahakama ya Afrika itashughulikia suala hili kikamilifu zaidi kuliko mahakama za nchi moja moja ambazo zinaelekea kuistahi au kuihurumia serikali ya nchi husika.
Wenye fedha au madaraka vijijini, kwenye kata, wilaya hadi ngazi za mikoa kwenye nchi mbalimbali wamekuwa wakikiuka haki za binadamu kwa kutumia nafasi zao kunyamazisha vitendo vyao ambavyo sasa vinaweza kumulikwa na kurunzi la mahakama ya Afrika na Dunia.
Demokrasia
Kwa kuwa kumekosekana chombo sahihi cha kushughulikia kutafsiri sheria na katiba katika nchi zetu hivi sasa viongozi walioko madarakani wamepora jukumu hilo na kuanza kutafsiri sheria hizo kwa mujibu wa uelewa wao na kile wanachokiamini wao kuwa ndio haki.
Mahakama Kuu ya Afrika itachangia sio kwa kiasi kidogo kutafsiri demokrasia na nafasi yake katika sheria na katiba mbalimbali za nchi zetu.
Kwa mantiki hii hapatakuwa na seti kadhaa za tafsiri kutegemeana na wale walioko madarakani na kile wanachokitaka wao.
Fujo na matatizo mengine yanayosababishwa na ukiukwaji wa misingi ya demokrasi sasa vinaweza kupata ufumbuzi wa kudumu kwa kuwa na Mahakama ya Afrika na Dunia na jopo la majaji kushughulikia kesi za demokrasia na uchaguzi.
Uwazi na rushwa
Mikataba mingi ya kibiashara ndani na nje ya nchi mbalimbali za Kiafrika inaghubikwa na giza la usiri na kinachofanyika huku kinajulikana na M…. na wahusika.
Mahakama ya Afrika na dunia itamulika masuala yote ambayo ni vivutio dhahiri vya rushwa kama vinafanyika bila uwazi.
Suala la uwazi limekuwa gumu sana kwa viongozi wa Afrika hasa pale maslahi binafsi na yale ya kutaka kuhakikisha chama tawala kinabakia madarakani baada ya kipindi cha utawala wake kwisha. Fedha inahitajika na kiongozi mwenyewe ili aweze kuwa na maisha mazuri baada ya kuondoka madarakani lakini vile vile fedha inahitajika ili kuhakikisha chama kinabakia tena madarakani kipindi kijacho.
Uwazi unakuwa kikwazo mbele ya masaula hayo hapo juu. Na kiongozi hata awe na nia nzuri namna gani kitendo cha kuleta uwazi katika uongozi wake anajikuta katika matatizo makubwa ndani ya chama chake na katika serikali yake.
Hata iundwe tume gani ikifikia kwenye hatua ya uwazi mwanga wa tume hiyo hufifia na kisha kufa kabisa.
Hatuwezi kutegemea viongozi wetu wajikosoe wenyewe; haiwezekani viongozi wetu kujitathmini wao wenywe; na haiwezekani viongozi wetu kujiadhibu wao wenyewe. Ni kwa mantiki hii taasisi ya kimataifa yenye uwezo wa kuwawajibisha hata viongozi au hata kuonesha tu kuwa wana makosa au aibu wanazoficha itasaidia kuongeza hadhi ya utawala katika Afrika.
Utawala bora
Utawala bora hauwezi kuja Afrika bila kuwa na chombo cha juu kinachoweza kukosoa taasisi zetu za ndani.
Mazoea, kutokujua na ukomo wa uwezo wa watendaji katika ngazi mbalimbali siku zote vitachangia kuwa na serikali dhaifu zisizowajibika kwa wananchi.
Hali ilivyo sasa karibu Afrika yote ni ile inayoonesha kuwa watawala ni mabwana na wananchi ni watwana.
Hali hii haiwezi kuruhusiwa kuendelea kama kweli tunataka kuwakomboa watu wetu kijamii, kiuchumi na kimawazo.
Ni pale tu wananchi wetu watakapokuwa na kauli na uwezo wa kuwawajibisha viongozi wao ndio maendeleo ya kweli yataanza kuonekana Afrika.
Mahakama Kuu ya Afrika itaweza pia kuchangia kwa kiasi kikubwa katika kuleta utawala bora Afrika kwa kusikiliza kilio cha wale wanaoamini kuwa kijiji, mji, wilaya au mkoa au nchi yao haifuati utawala wa sheria wala katiba iliyopo haikidhi haki za chini na za juu za wananchi katika nchi husika.
Msingi wa UA
Mahakama ya Afrika itakuwa jiwe la msingi la Umoja wa Afrika. Misingi mingine ni pamoja na haki ya wananchi kusafiri, kuishi na kufanya kazi popote Afrika; jeshi moja la Afrika; bunge la Afrika ambavyo ni vitu pekee vitakavyoweza kufanikisha kuwa na serikali moja ya Afrika.
Yapo mambo mengine muhimu ya kuzingatiwa na hasa unapoelewa kuwa nchi za Kiafrika hazifanani na kila moja ina historia yake na matatizo yake kutokana na sababu za kisiasa, kijamii na mazingira.
Hata hivyo, misingi hiyo hapo juu inaweza kuwa mwanzo wa kufanikisha kuondoa matatizo ya kila nchi kwani utawala wa sheria na taratibu zinazokubalika zina nguvu na uwezo wa kurahisisha maazimio na mipango mingine kwa kila nchi.
Taasisi zingine ziige mfano
Umoja wa Afrika utaendelea kuwa ndoto kama Waafrika watategemea viongozi wao tu ndio watakaoufanikisha.
Kinachotakiwa hivi sasa ni kwa makundi mbalimbali hapa Afrika kama vile waandishi wa habari, walimu, madaktari, manesi, watumishi wa serikali, maprofesa, wahandisi, wahasibu, vijana, wazee, wanawake na kadhalika kuunda taasisi zao chini ya Umoja wa Afrika na kuanza kuandaa ajenda mbalimbali zitakazoongoza Afrika kule wao na wenzao wote wanakotaka iende.
Heshima na usawa
Umoja na maendeleo ya Afrika lazima ujengwe katika misingi ya usawa na heshima kwa wote.
Bila shaka mahakama ya Afrika itatoa msukumo unaotakiwa katika kuhakikisha kuwa kila nchi inazingatia kuwepo sio tu kwa haki bali usawa na heshima kwa kila mwananchi kama nguzo za kusimamisha mkusanyiko wa watu mkubwa kuliko ule wa utaifa mmoja mmoja kwa nchi mbalimbali za Kiafrika.
Afrika ina nafasi chungu nzima za kujifunza kutoka mabara mengine jinsi ya kufanikisha kuwepo kwa umoja wa Afrika utakaochangia tu sio kuondoa umaskini bali pia kujenga mkusanyiko wa watu utakaopewa usawa na heshima toka popote pale duniani.
Itakuwa ni kitendo cha faraja kama viongozi wetu wataunga mkono kwa hali na mali mpango wa uanzishaji wa mahakama kamili ya Afrika na ile ya dunia.
Kamati au tume hiyo hivi sasa iko mbioni kufanywa mahakama kama viongozi wa Afrika wataridhia suala hili kwenye mkutano wa kilele ujao kunako mwezi Juni.
Kwa mfano mjane anayeamini kuwa kanyimwa haki za kurithi mali aliyochuma na mumewe na akapeleka kesi mahakamani lakini ikatupwa nje; akakata rufaa mahakama kuu akashindwa; akakata rufaa tena mahakama ya rufaa na bado akashindwa bado atakuwa na nafasi kama hiyo tena kwenye mahakama hiyo ya Afrika.
Uanzishwaji wa Mahakama Kuu ya Afrika unakwenda sambamba na uanzishwaji wa mahakama ya Umoja wa Mataifa ambayo malengo yake bado yana shabaha ya kufanikisha vita vya haki ya binadamu duniani.
Kwa bahati mbaya sio wengi wanaojua juu ya kile kinachoendelea duniani katika ujenzi wa taasisi na taratibu zitakazohakikisha kuwa haki na usawa mbele ya vyombo vya sheria inakuwa ni ndoto ya kweli kwa kila mtu popote pale alipo duniani.
Hali ilivyo sasa ni kuwa anaweza kuibuka mtu mahala popote pale duniani na kwa kutumia nafasi yake ya uongozi; mipaka ya kile anachoita taifa lake huru; na kwa ushirikiano na wajanja wachache akafanya uhuni mkubwa katika nchi yake ikiwamo kudhulumu watu mali zao; kujitajirisha kwa wizi au rushwa; na hata kuiuza nchi yake na raia katika nchi yake na dunia nzima kwa ujumla isiwe na lolote la kufanya kumkomesha mtu huyo.
Isitoshe yapo matukio kadhaa katika nchi mbalimbali za Kiafrika hivi sasa kuonesha kuwa baadhi ya wale walioko madarakani wanadiriki kuficha au kufukia vitendo viovu, dhuluma, uonevu au vitendo vingine vya ukiukwaji wa haki za binadamu katika milki yao.
Kwa kuwa na Mahakama Kuu ya Afrika na Dunia na pengine mahakama za rufani katika ngazi hizo pia kutaimarisha uhuru wa mahakama za nchi moja moja na kuboresha haki na usawa kwa raia wa nchi husika.
Inavyoonekana ni kuwa dunia imeona udhaifu wa taasisi za kimataifa ambazo zinakosa meno ya kikatiba na kisheria.
Hali hii imesababisha kwa baadhi ya nchi mahakimu na majaji kuonekana wanawajibika kwa viongozi waliowateua na hivyo kuzifanya mahakama kutokuwa huru.
Ubinafsi pia umejitokeza katika vyombo vya sheria kufikia kiwango cha mwenye fedha kununua haki dhidi ya mnyonge anayestahili haki hiyo.
Maadili yameshuka katika baadhi ya nchi na rushwa sio kitu kigeni katika vyombo vingi vya sheria karibu katika kila nchi Afrika. Mahakama ya Afrika na dunia zitarudisha heshima ya mahakimu na majaji popote pale kwani wale wanaokiuka maadili wataadhiriwa na ngazi za juu.
Uzuri wa Mahakama ya Afrika ni kuwa itakuwa na majaji toka nchi mbalimbali za Kiafrika na pengine hata kutoka nje ya Afrika (kutegemeana na aina ya kesi na uzoefu wa majaji husika). Kitakachopambana katika duru hizi ni ubingwa wa kuitafsiri sheria kwa mujibu wa sheria na mikataba ya kimataifa kwa lengo la kuhakikisha Waafrika wote wanakuwa sawa mbele ya sheria hizo na mwenye haki ndiye anayestahili kunufaika na sio vinginevyo.
Haki za binadamu
Waafrika na wasio Waafrika kwa muda mrefu wamekuwa wakililaumu bara hili kwa kushindwa kuheshimu haki za binadamu.
Vyombo vya dola, yaani polisi, magereza na upelelezi aghalabu vinalaumiwa kwa kukiuka haki za binadamu.
Mathalani, hali ya magereza ya Afrika ukifananisha na yale ya Ulaya au Marekani ni ya kusikitisha na kutisha. Upo uwezekano mkubwa kuwa mahakama ya Afrika itashughulikia suala hili kikamilifu zaidi kuliko mahakama za nchi moja moja ambazo zinaelekea kuistahi au kuihurumia serikali ya nchi husika.
Wenye fedha au madaraka vijijini, kwenye kata, wilaya hadi ngazi za mikoa kwenye nchi mbalimbali wamekuwa wakikiuka haki za binadamu kwa kutumia nafasi zao kunyamazisha vitendo vyao ambavyo sasa vinaweza kumulikwa na kurunzi la mahakama ya Afrika na Dunia.
Demokrasia
Kwa kuwa kumekosekana chombo sahihi cha kushughulikia kutafsiri sheria na katiba katika nchi zetu hivi sasa viongozi walioko madarakani wamepora jukumu hilo na kuanza kutafsiri sheria hizo kwa mujibu wa uelewa wao na kile wanachokiamini wao kuwa ndio haki.
Mahakama Kuu ya Afrika itachangia sio kwa kiasi kidogo kutafsiri demokrasia na nafasi yake katika sheria na katiba mbalimbali za nchi zetu.
Kwa mantiki hii hapatakuwa na seti kadhaa za tafsiri kutegemeana na wale walioko madarakani na kile wanachokitaka wao.
Fujo na matatizo mengine yanayosababishwa na ukiukwaji wa misingi ya demokrasi sasa vinaweza kupata ufumbuzi wa kudumu kwa kuwa na Mahakama ya Afrika na Dunia na jopo la majaji kushughulikia kesi za demokrasia na uchaguzi.
Uwazi na rushwa
Mikataba mingi ya kibiashara ndani na nje ya nchi mbalimbali za Kiafrika inaghubikwa na giza la usiri na kinachofanyika huku kinajulikana na M…. na wahusika.
Mahakama ya Afrika na dunia itamulika masuala yote ambayo ni vivutio dhahiri vya rushwa kama vinafanyika bila uwazi.
Suala la uwazi limekuwa gumu sana kwa viongozi wa Afrika hasa pale maslahi binafsi na yale ya kutaka kuhakikisha chama tawala kinabakia madarakani baada ya kipindi cha utawala wake kwisha. Fedha inahitajika na kiongozi mwenyewe ili aweze kuwa na maisha mazuri baada ya kuondoka madarakani lakini vile vile fedha inahitajika ili kuhakikisha chama kinabakia tena madarakani kipindi kijacho.
Uwazi unakuwa kikwazo mbele ya masaula hayo hapo juu. Na kiongozi hata awe na nia nzuri namna gani kitendo cha kuleta uwazi katika uongozi wake anajikuta katika matatizo makubwa ndani ya chama chake na katika serikali yake.
Hata iundwe tume gani ikifikia kwenye hatua ya uwazi mwanga wa tume hiyo hufifia na kisha kufa kabisa.
Hatuwezi kutegemea viongozi wetu wajikosoe wenyewe; haiwezekani viongozi wetu kujitathmini wao wenywe; na haiwezekani viongozi wetu kujiadhibu wao wenyewe. Ni kwa mantiki hii taasisi ya kimataifa yenye uwezo wa kuwawajibisha hata viongozi au hata kuonesha tu kuwa wana makosa au aibu wanazoficha itasaidia kuongeza hadhi ya utawala katika Afrika.
Utawala bora
Utawala bora hauwezi kuja Afrika bila kuwa na chombo cha juu kinachoweza kukosoa taasisi zetu za ndani.
Mazoea, kutokujua na ukomo wa uwezo wa watendaji katika ngazi mbalimbali siku zote vitachangia kuwa na serikali dhaifu zisizowajibika kwa wananchi.
Hali ilivyo sasa karibu Afrika yote ni ile inayoonesha kuwa watawala ni mabwana na wananchi ni watwana.
Hali hii haiwezi kuruhusiwa kuendelea kama kweli tunataka kuwakomboa watu wetu kijamii, kiuchumi na kimawazo.
Ni pale tu wananchi wetu watakapokuwa na kauli na uwezo wa kuwawajibisha viongozi wao ndio maendeleo ya kweli yataanza kuonekana Afrika.
Mahakama Kuu ya Afrika itaweza pia kuchangia kwa kiasi kikubwa katika kuleta utawala bora Afrika kwa kusikiliza kilio cha wale wanaoamini kuwa kijiji, mji, wilaya au mkoa au nchi yao haifuati utawala wa sheria wala katiba iliyopo haikidhi haki za chini na za juu za wananchi katika nchi husika.
Msingi wa UA
Mahakama ya Afrika itakuwa jiwe la msingi la Umoja wa Afrika. Misingi mingine ni pamoja na haki ya wananchi kusafiri, kuishi na kufanya kazi popote Afrika; jeshi moja la Afrika; bunge la Afrika ambavyo ni vitu pekee vitakavyoweza kufanikisha kuwa na serikali moja ya Afrika.
Yapo mambo mengine muhimu ya kuzingatiwa na hasa unapoelewa kuwa nchi za Kiafrika hazifanani na kila moja ina historia yake na matatizo yake kutokana na sababu za kisiasa, kijamii na mazingira.
Hata hivyo, misingi hiyo hapo juu inaweza kuwa mwanzo wa kufanikisha kuondoa matatizo ya kila nchi kwani utawala wa sheria na taratibu zinazokubalika zina nguvu na uwezo wa kurahisisha maazimio na mipango mingine kwa kila nchi.
Taasisi zingine ziige mfano
Umoja wa Afrika utaendelea kuwa ndoto kama Waafrika watategemea viongozi wao tu ndio watakaoufanikisha.
Kinachotakiwa hivi sasa ni kwa makundi mbalimbali hapa Afrika kama vile waandishi wa habari, walimu, madaktari, manesi, watumishi wa serikali, maprofesa, wahandisi, wahasibu, vijana, wazee, wanawake na kadhalika kuunda taasisi zao chini ya Umoja wa Afrika na kuanza kuandaa ajenda mbalimbali zitakazoongoza Afrika kule wao na wenzao wote wanakotaka iende.
Heshima na usawa
Umoja na maendeleo ya Afrika lazima ujengwe katika misingi ya usawa na heshima kwa wote.
Bila shaka mahakama ya Afrika itatoa msukumo unaotakiwa katika kuhakikisha kuwa kila nchi inazingatia kuwepo sio tu kwa haki bali usawa na heshima kwa kila mwananchi kama nguzo za kusimamisha mkusanyiko wa watu mkubwa kuliko ule wa utaifa mmoja mmoja kwa nchi mbalimbali za Kiafrika.
Afrika ina nafasi chungu nzima za kujifunza kutoka mabara mengine jinsi ya kufanikisha kuwepo kwa umoja wa Afrika utakaochangia tu sio kuondoa umaskini bali pia kujenga mkusanyiko wa watu utakaopewa usawa na heshima toka popote pale duniani.
Itakuwa ni kitendo cha faraja kama viongozi wetu wataunga mkono kwa hali na mali mpango wa uanzishaji wa mahakama kamili ya Afrika na ile ya dunia.
Haki kulindwa na mahakama ya Afrika, Dunia?
Sio watu wengi wanaojua kuwa iwapo umefuata taratibu zote za mahakama katika nchi yako na hukuridhika na maamuzi ya mahakama basi unaweza kukata rufaa kwenye kamati maalum ya Umoja wa Afrika inayoshugulikia masuala ya haki za binadamu.
Kamati au tume hiyo hivi sasa iko mbioni kufanywa mahakama kama viongozi wa Afrika wataridhia suala hili kwenye mkutano wa kilele ujao kunako mwezi Juni.
Kwa mfano mjane anayeamini kuwa kanyimwa haki za kurithi mali aliyochuma na mumewe na akapeleka kesi mahakamani lakini ikatupwa nje; akakata rufaa mahakama kuu akashindwa; akakata rufaa tena mahakama ya rufaa na bado akashindwa bado atakuwa na nafasi kama hiyo tena kwenye mahakama hiyo ya Afrika.
Uanzishwaji wa Mahakama Kuu ya Afrika unakwenda sambamba na uanzishwaji wa mahakama ya Umoja wa Mataifa ambayo malengo yake bado yana shabaha ya kufanikisha vita vya haki ya binadamu duniani.
Kwa bahati mbaya sio wengi wanaojua juu ya kile kinachoendelea duniani katika ujenzi wa taasisi na taratibu zitakazohakikisha kuwa haki na usawa mbele ya vyombo vya sheria inakuwa ni ndoto ya kweli kwa kila mtu popote pale alipo duniani.
Hali ilivyo sasa ni kuwa anaweza kuibuka mtu mahala popote pale duniani na kwa kutumia nafasi yake ya uongozi; mipaka ya kile anachoita taifa lake huru; na kwa ushirikiano na wajanja wachache akafanya uhuni mkubwa katika nchi yake ikiwamo kudhulumu watu mali zao; kujitajirisha kwa wizi au rushwa; na hata kuiuza nchi yake na raia katika nchi yake na dunia nzima kwa ujumla isiwe na lolote la kufanya kumkomesha mtu huyo.
Isitoshe yapo matukio kadhaa katika nchi mbalimbali za Kiafrika hivi sasa kuonesha kuwa baadhi ya wale walioko madarakani wanadiriki kuficha au kufukia vitendo viovu, dhuluma, uonevu au vitendo vingine vya ukiukwaji wa haki za binadamu katika milki yao.
Kwa kuwa na Mahakama Kuu ya Afrika na Dunia na pengine mahakama za rufani katika ngazi hizo pia kutaimarisha uhuru wa mahakama za nchi moja moja na kuboresha haki na usawa kwa raia wa nchi husika.
Inavyoonekana ni kuwa dunia imeona udhaifu wa taasisi za kimataifa ambazo zinakosa meno ya kikatiba na kisheria.
Hali hii imesababisha kwa baadhi ya nchi mahakimu na majaji kuonekana wanawajibika kwa viongozi waliowateua na hivyo kuzifanya mahakama kutokuwa huru.
Ubinafsi pia umejitokeza katika vyombo vya sheria kufikia kiwango cha mwenye fedha kununua haki dhidi ya mnyonge anayestahili haki hiyo.
Maadili yameshuka katika baadhi ya nchi na rushwa sio kitu kigeni katika vyombo vingi vya sheria karibu katika kila nchi Afrika. Mahakama ya Afrika na dunia zitarudisha heshima ya mahakimu na majaji popote pale kwani wale wanaokiuka maadili wataadhiriwa na ngazi za juu.
Uzuri wa Mahakama ya Afrika ni kuwa itakuwa na majaji toka nchi mbalimbali za Kiafrika na pengine hata kutoka nje ya Afrika (kutegemeana na aina ya kesi na uzoefu wa majaji husika). Kitakachopambana katika duru hizi ni ubingwa wa kuitafsiri sheria kwa mujibu wa sheria na mikataba ya kimataifa kwa lengo la kuhakikisha Waafrika wote wanakuwa sawa mbele ya sheria hizo na mwenye haki ndiye anayestahili kunufaika na sio vinginevyo.
Haki za binadamu
Waafrika na wasio Waafrika kwa muda mrefu wamekuwa wakililaumu bara hili kwa kushindwa kuheshimu haki za binadamu.
Vyombo vya dola, yaani polisi, magereza na upelelezi aghalabu vinalaumiwa kwa kukiuka haki za binadamu.
Mathalani, hali ya magereza ya Afrika ukifananisha na yale ya Ulaya au Marekani ni ya kusikitisha na kutisha. Upo uwezekano mkubwa kuwa mahakama ya Afrika itashughulikia suala hili kikamilifu zaidi kuliko mahakama za nchi moja moja ambazo zinaelekea kuistahi au kuihurumia serikali ya nchi husika.
Wenye fedha au madaraka vijijini, kwenye kata, wilaya hadi ngazi za mikoa kwenye nchi mbalimbali wamekuwa wakikiuka haki za binadamu kwa kutumia nafasi zao kunyamazisha vitendo vyao ambavyo sasa vinaweza kumulikwa na kurunzi la mahakama ya Afrika na Dunia.
Demokrasia
Kwa kuwa kumekosekana chombo sahihi cha kushughulikia kutafsiri sheria na katiba katika nchi zetu hivi sasa viongozi walioko madarakani wamepora jukumu hilo na kuanza kutafsiri sheria hizo kwa mujibu wa uelewa wao na kile wanachokiamini wao kuwa ndio haki.
Mahakama Kuu ya Afrika itachangia sio kwa kiasi kidogo kutafsiri demokrasia na nafasi yake katika sheria na katiba mbalimbali za nchi zetu.
Kwa mantiki hii hapatakuwa na seti kadhaa za tafsiri kutegemeana na wale walioko madarakani na kile wanachokitaka wao.
Fujo na matatizo mengine yanayosababishwa na ukiukwaji wa misingi ya demokrasi sasa vinaweza kupata ufumbuzi wa kudumu kwa kuwa na Mahakama ya Afrika na Dunia na jopo la majaji kushughulikia kesi za demokrasia na uchaguzi.
Uwazi na rushwa
Mikataba mingi ya kibiashara ndani na nje ya nchi mbalimbali za Kiafrika inaghubikwa na giza la usiri na kinachofanyika huku kinajulikana na M…. na wahusika.
Mahakama ya Afrika na dunia itamulika masuala yote ambayo ni vivutio dhahiri vya rushwa kama vinafanyika bila uwazi.
Suala la uwazi limekuwa gumu sana kwa viongozi wa Afrika hasa pale maslahi binafsi na yale ya kutaka kuhakikisha chama tawala kinabakia madarakani baada ya kipindi cha utawala wake kwisha. Fedha inahitajika na kiongozi mwenyewe ili aweze kuwa na maisha mazuri baada ya kuondoka madarakani lakini vile vile fedha inahitajika ili kuhakikisha chama kinabakia tena madarakani kipindi kijacho.
Uwazi unakuwa kikwazo mbele ya masaula hayo hapo juu. Na kiongozi hata awe na nia nzuri namna gani kitendo cha kuleta uwazi katika uongozi wake anajikuta katika matatizo makubwa ndani ya chama chake na katika serikali yake.
Hata iundwe tume gani ikifikia kwenye hatua ya uwazi mwanga wa tume hiyo hufifia na kisha kufa kabisa.
Hatuwezi kutegemea viongozi wetu wajikosoe wenyewe; haiwezekani viongozi wetu kujitathmini wao wenywe; na haiwezekani viongozi wetu kujiadhibu wao wenyewe. Ni kwa mantiki hii taasisi ya kimataifa yenye uwezo wa kuwawajibisha hata viongozi au hata kuonesha tu kuwa wana makosa au aibu wanazoficha itasaidia kuongeza hadhi ya utawala katika Afrika.
Utawala bora
Utawala bora hauwezi kuja Afrika bila kuwa na chombo cha juu kinachoweza kukosoa taasisi zetu za ndani.
Mazoea, kutokujua na ukomo wa uwezo wa watendaji katika ngazi mbalimbali siku zote vitachangia kuwa na serikali dhaifu zisizowajibika kwa wananchi.
Hali ilivyo sasa karibu Afrika yote ni ile inayoonesha kuwa watawala ni mabwana na wananchi ni watwana.
Hali hii haiwezi kuruhusiwa kuendelea kama kweli tunataka kuwakomboa watu wetu kijamii, kiuchumi na kimawazo.
Ni pale tu wananchi wetu watakapokuwa na kauli na uwezo wa kuwawajibisha viongozi wao ndio maendeleo ya kweli yataanza kuonekana Afrika.
Mahakama Kuu ya Afrika itaweza pia kuchangia kwa kiasi kikubwa katika kuleta utawala bora Afrika kwa kusikiliza kilio cha wale wanaoamini kuwa kijiji, mji, wilaya au mkoa au nchi yao haifuati utawala wa sheria wala katiba iliyopo haikidhi haki za chini na za juu za wananchi katika nchi husika.
Msingi wa UA
Mahakama ya Afrika itakuwa jiwe la msingi la Umoja wa Afrika. Misingi mingine ni pamoja na haki ya wananchi kusafiri, kuishi na kufanya kazi popote Afrika; jeshi moja la Afrika; bunge la Afrika ambavyo ni vitu pekee vitakavyoweza kufanikisha kuwa na serikali moja ya Afrika.
Yapo mambo mengine muhimu ya kuzingatiwa na hasa unapoelewa kuwa nchi za Kiafrika hazifanani na kila moja ina historia yake na matatizo yake kutokana na sababu za kisiasa, kijamii na mazingira.
Hata hivyo, misingi hiyo hapo juu inaweza kuwa mwanzo wa kufanikisha kuondoa matatizo ya kila nchi kwani utawala wa sheria na taratibu zinazokubalika zina nguvu na uwezo wa kurahisisha maazimio na mipango mingine kwa kila nchi.
Taasisi zingine ziige mfano
Umoja wa Afrika utaendelea kuwa ndoto kama Waafrika watategemea viongozi wao tu ndio watakaoufanikisha.
Kinachotakiwa hivi sasa ni kwa makundi mbalimbali hapa Afrika kama vile waandishi wa habari, walimu, madaktari, manesi, watumishi wa serikali, maprofesa, wahandisi, wahasibu, vijana, wazee, wanawake na kadhalika kuunda taasisi zao chini ya Umoja wa Afrika na kuanza kuandaa ajenda mbalimbali zitakazoongoza Afrika kule wao na wenzao wote wanakotaka iende.
Heshima na usawa
Umoja na maendeleo ya Afrika lazima ujengwe katika misingi ya usawa na heshima kwa wote.
Bila shaka mahakama ya Afrika itatoa msukumo unaotakiwa katika kuhakikisha kuwa kila nchi inazingatia kuwepo sio tu kwa haki bali usawa na heshima kwa kila mwananchi kama nguzo za kusimamisha mkusanyiko wa watu mkubwa kuliko ule wa utaifa mmoja mmoja kwa nchi mbalimbali za Kiafrika.
Afrika ina nafasi chungu nzima za kujifunza kutoka mabara mengine jinsi ya kufanikisha kuwepo kwa umoja wa Afrika utakaochangia tu sio kuondoa umaskini bali pia kujenga mkusanyiko wa watu utakaopewa usawa na heshima toka popote pale duniani.
Itakuwa ni kitendo cha faraja kama viongozi wetu wataunga mkono kwa hali na mali mpango wa uanzishaji wa mahakama kamili ya Afrika na ile ya dunia.
Kamati au tume hiyo hivi sasa iko mbioni kufanywa mahakama kama viongozi wa Afrika wataridhia suala hili kwenye mkutano wa kilele ujao kunako mwezi Juni.
Kwa mfano mjane anayeamini kuwa kanyimwa haki za kurithi mali aliyochuma na mumewe na akapeleka kesi mahakamani lakini ikatupwa nje; akakata rufaa mahakama kuu akashindwa; akakata rufaa tena mahakama ya rufaa na bado akashindwa bado atakuwa na nafasi kama hiyo tena kwenye mahakama hiyo ya Afrika.
Uanzishwaji wa Mahakama Kuu ya Afrika unakwenda sambamba na uanzishwaji wa mahakama ya Umoja wa Mataifa ambayo malengo yake bado yana shabaha ya kufanikisha vita vya haki ya binadamu duniani.
Kwa bahati mbaya sio wengi wanaojua juu ya kile kinachoendelea duniani katika ujenzi wa taasisi na taratibu zitakazohakikisha kuwa haki na usawa mbele ya vyombo vya sheria inakuwa ni ndoto ya kweli kwa kila mtu popote pale alipo duniani.
Hali ilivyo sasa ni kuwa anaweza kuibuka mtu mahala popote pale duniani na kwa kutumia nafasi yake ya uongozi; mipaka ya kile anachoita taifa lake huru; na kwa ushirikiano na wajanja wachache akafanya uhuni mkubwa katika nchi yake ikiwamo kudhulumu watu mali zao; kujitajirisha kwa wizi au rushwa; na hata kuiuza nchi yake na raia katika nchi yake na dunia nzima kwa ujumla isiwe na lolote la kufanya kumkomesha mtu huyo.
Isitoshe yapo matukio kadhaa katika nchi mbalimbali za Kiafrika hivi sasa kuonesha kuwa baadhi ya wale walioko madarakani wanadiriki kuficha au kufukia vitendo viovu, dhuluma, uonevu au vitendo vingine vya ukiukwaji wa haki za binadamu katika milki yao.
Kwa kuwa na Mahakama Kuu ya Afrika na Dunia na pengine mahakama za rufani katika ngazi hizo pia kutaimarisha uhuru wa mahakama za nchi moja moja na kuboresha haki na usawa kwa raia wa nchi husika.
Inavyoonekana ni kuwa dunia imeona udhaifu wa taasisi za kimataifa ambazo zinakosa meno ya kikatiba na kisheria.
Hali hii imesababisha kwa baadhi ya nchi mahakimu na majaji kuonekana wanawajibika kwa viongozi waliowateua na hivyo kuzifanya mahakama kutokuwa huru.
Ubinafsi pia umejitokeza katika vyombo vya sheria kufikia kiwango cha mwenye fedha kununua haki dhidi ya mnyonge anayestahili haki hiyo.
Maadili yameshuka katika baadhi ya nchi na rushwa sio kitu kigeni katika vyombo vingi vya sheria karibu katika kila nchi Afrika. Mahakama ya Afrika na dunia zitarudisha heshima ya mahakimu na majaji popote pale kwani wale wanaokiuka maadili wataadhiriwa na ngazi za juu.
Uzuri wa Mahakama ya Afrika ni kuwa itakuwa na majaji toka nchi mbalimbali za Kiafrika na pengine hata kutoka nje ya Afrika (kutegemeana na aina ya kesi na uzoefu wa majaji husika). Kitakachopambana katika duru hizi ni ubingwa wa kuitafsiri sheria kwa mujibu wa sheria na mikataba ya kimataifa kwa lengo la kuhakikisha Waafrika wote wanakuwa sawa mbele ya sheria hizo na mwenye haki ndiye anayestahili kunufaika na sio vinginevyo.
Haki za binadamu
Waafrika na wasio Waafrika kwa muda mrefu wamekuwa wakililaumu bara hili kwa kushindwa kuheshimu haki za binadamu.
Vyombo vya dola, yaani polisi, magereza na upelelezi aghalabu vinalaumiwa kwa kukiuka haki za binadamu.
Mathalani, hali ya magereza ya Afrika ukifananisha na yale ya Ulaya au Marekani ni ya kusikitisha na kutisha. Upo uwezekano mkubwa kuwa mahakama ya Afrika itashughulikia suala hili kikamilifu zaidi kuliko mahakama za nchi moja moja ambazo zinaelekea kuistahi au kuihurumia serikali ya nchi husika.
Wenye fedha au madaraka vijijini, kwenye kata, wilaya hadi ngazi za mikoa kwenye nchi mbalimbali wamekuwa wakikiuka haki za binadamu kwa kutumia nafasi zao kunyamazisha vitendo vyao ambavyo sasa vinaweza kumulikwa na kurunzi la mahakama ya Afrika na Dunia.
Demokrasia
Kwa kuwa kumekosekana chombo sahihi cha kushughulikia kutafsiri sheria na katiba katika nchi zetu hivi sasa viongozi walioko madarakani wamepora jukumu hilo na kuanza kutafsiri sheria hizo kwa mujibu wa uelewa wao na kile wanachokiamini wao kuwa ndio haki.
Mahakama Kuu ya Afrika itachangia sio kwa kiasi kidogo kutafsiri demokrasia na nafasi yake katika sheria na katiba mbalimbali za nchi zetu.
Kwa mantiki hii hapatakuwa na seti kadhaa za tafsiri kutegemeana na wale walioko madarakani na kile wanachokitaka wao.
Fujo na matatizo mengine yanayosababishwa na ukiukwaji wa misingi ya demokrasi sasa vinaweza kupata ufumbuzi wa kudumu kwa kuwa na Mahakama ya Afrika na Dunia na jopo la majaji kushughulikia kesi za demokrasia na uchaguzi.
Uwazi na rushwa
Mikataba mingi ya kibiashara ndani na nje ya nchi mbalimbali za Kiafrika inaghubikwa na giza la usiri na kinachofanyika huku kinajulikana na M…. na wahusika.
Mahakama ya Afrika na dunia itamulika masuala yote ambayo ni vivutio dhahiri vya rushwa kama vinafanyika bila uwazi.
Suala la uwazi limekuwa gumu sana kwa viongozi wa Afrika hasa pale maslahi binafsi na yale ya kutaka kuhakikisha chama tawala kinabakia madarakani baada ya kipindi cha utawala wake kwisha. Fedha inahitajika na kiongozi mwenyewe ili aweze kuwa na maisha mazuri baada ya kuondoka madarakani lakini vile vile fedha inahitajika ili kuhakikisha chama kinabakia tena madarakani kipindi kijacho.
Uwazi unakuwa kikwazo mbele ya masaula hayo hapo juu. Na kiongozi hata awe na nia nzuri namna gani kitendo cha kuleta uwazi katika uongozi wake anajikuta katika matatizo makubwa ndani ya chama chake na katika serikali yake.
Hata iundwe tume gani ikifikia kwenye hatua ya uwazi mwanga wa tume hiyo hufifia na kisha kufa kabisa.
Hatuwezi kutegemea viongozi wetu wajikosoe wenyewe; haiwezekani viongozi wetu kujitathmini wao wenywe; na haiwezekani viongozi wetu kujiadhibu wao wenyewe. Ni kwa mantiki hii taasisi ya kimataifa yenye uwezo wa kuwawajibisha hata viongozi au hata kuonesha tu kuwa wana makosa au aibu wanazoficha itasaidia kuongeza hadhi ya utawala katika Afrika.
Utawala bora
Utawala bora hauwezi kuja Afrika bila kuwa na chombo cha juu kinachoweza kukosoa taasisi zetu za ndani.
Mazoea, kutokujua na ukomo wa uwezo wa watendaji katika ngazi mbalimbali siku zote vitachangia kuwa na serikali dhaifu zisizowajibika kwa wananchi.
Hali ilivyo sasa karibu Afrika yote ni ile inayoonesha kuwa watawala ni mabwana na wananchi ni watwana.
Hali hii haiwezi kuruhusiwa kuendelea kama kweli tunataka kuwakomboa watu wetu kijamii, kiuchumi na kimawazo.
Ni pale tu wananchi wetu watakapokuwa na kauli na uwezo wa kuwawajibisha viongozi wao ndio maendeleo ya kweli yataanza kuonekana Afrika.
Mahakama Kuu ya Afrika itaweza pia kuchangia kwa kiasi kikubwa katika kuleta utawala bora Afrika kwa kusikiliza kilio cha wale wanaoamini kuwa kijiji, mji, wilaya au mkoa au nchi yao haifuati utawala wa sheria wala katiba iliyopo haikidhi haki za chini na za juu za wananchi katika nchi husika.
Msingi wa UA
Mahakama ya Afrika itakuwa jiwe la msingi la Umoja wa Afrika. Misingi mingine ni pamoja na haki ya wananchi kusafiri, kuishi na kufanya kazi popote Afrika; jeshi moja la Afrika; bunge la Afrika ambavyo ni vitu pekee vitakavyoweza kufanikisha kuwa na serikali moja ya Afrika.
Yapo mambo mengine muhimu ya kuzingatiwa na hasa unapoelewa kuwa nchi za Kiafrika hazifanani na kila moja ina historia yake na matatizo yake kutokana na sababu za kisiasa, kijamii na mazingira.
Hata hivyo, misingi hiyo hapo juu inaweza kuwa mwanzo wa kufanikisha kuondoa matatizo ya kila nchi kwani utawala wa sheria na taratibu zinazokubalika zina nguvu na uwezo wa kurahisisha maazimio na mipango mingine kwa kila nchi.
Taasisi zingine ziige mfano
Umoja wa Afrika utaendelea kuwa ndoto kama Waafrika watategemea viongozi wao tu ndio watakaoufanikisha.
Kinachotakiwa hivi sasa ni kwa makundi mbalimbali hapa Afrika kama vile waandishi wa habari, walimu, madaktari, manesi, watumishi wa serikali, maprofesa, wahandisi, wahasibu, vijana, wazee, wanawake na kadhalika kuunda taasisi zao chini ya Umoja wa Afrika na kuanza kuandaa ajenda mbalimbali zitakazoongoza Afrika kule wao na wenzao wote wanakotaka iende.
Heshima na usawa
Umoja na maendeleo ya Afrika lazima ujengwe katika misingi ya usawa na heshima kwa wote.
Bila shaka mahakama ya Afrika itatoa msukumo unaotakiwa katika kuhakikisha kuwa kila nchi inazingatia kuwepo sio tu kwa haki bali usawa na heshima kwa kila mwananchi kama nguzo za kusimamisha mkusanyiko wa watu mkubwa kuliko ule wa utaifa mmoja mmoja kwa nchi mbalimbali za Kiafrika.
Afrika ina nafasi chungu nzima za kujifunza kutoka mabara mengine jinsi ya kufanikisha kuwepo kwa umoja wa Afrika utakaochangia tu sio kuondoa umaskini bali pia kujenga mkusanyiko wa watu utakaopewa usawa na heshima toka popote pale duniani.
Itakuwa ni kitendo cha faraja kama viongozi wetu wataunga mkono kwa hali na mali mpango wa uanzishaji wa mahakama kamili ya Afrika na ile ya dunia.
Matumizi duni ya Tovuti yanadumaza uchumi
Katika siku za hivi karibuni nimekuwa nikipata barua-pepe nyingi za watu wa nje wanaotaka kuja kutalii, kuwekeza au kufanya biashara na Tanzania.
Baadhi ya watu hao wala sio wageni ni Watanzania waliokaa nje muda mrefu au ambao wamechukua uraia wa nchi nyingine lakini hivi sasa wanataka kurejea baada ya kuvutiwa na mageuzi ya uchumi yanayoendelea nchini.
Baadhi ya maswali yao yamekuwa magumu kwangu kujibu na nikayaelekeza au nikawaelekeza wahusika kwa taasisi kama vile Wizara ya Mambo ya Nje, TCCIA, taasisi zinazohusika na utalii, Tanzania Investment Center na kadhalika.
Majibu ambayo watu waliowasiliana nami wananipa ni kuwa ama e-mail za wahusika hazifanyi kazi, nyingine zina virusi, na kwa kila hali hakuna anayewajibu wala kushughulikia shida zao.
Kwa mfano, kuna makampuni ya utalii nchini Venezuela na Brazil yaliyokuwa na watu wanaotaka kuja kutalii Tanzania. Hadi leo wanahaha kupata visa za kuja Tanzania.
Ubalozi wa karibu (naomba kusahihishwa) nadhani ni Washington lakini japo ubalozi huo una web-site na email wakala hao wanasema hakuna jibu walilolipata.
Anwani ya websaiti ya ubalozi huo ni http://www.tanzaniaembassy-us.org na kama sikosei email yao ni: balozi@tanzaniaembassy-us.org Wabrazili na Wavenezuela wanasema ni anwani bubu.
Katika websaiti hiyo pamoja na mambo mengine kuna nembo ya taifa, bendera inayopepea lakini inaelekea anwani ya barua pepe yao haipepei na kuna twiga anayekimbia na maneno -TANZANIA ON THE GO- lakini inaelekea kwa hakika sivyo bado Tanzania imelala katika kutumia mtandao ili kukuza uchumi wake kutokana na biashara nyingi ambazo hivi leo zinafanyika kwa kutumia email na internet.
Kuna bwana yuko Uarabuni anataka kuanza biashara ya kununua na kuuza mifugo na Tanzania. Inaelekea huyu kazaliwa hapa maana anazungumza Kiswahili fasaha. Nimejaribu kumuelekeza kwa wahusika lakini anasema hapati majibu anaomba mimi nimsaidie. Lakini ninadhani kuna walioajiriwa kufanya kazi hiyo au sio-pengine Wizara inayohusika inaweza kumsaidia kwa kuwasiliana nami.
Leo ninapoandika makala hii nina barua pepe zaidi ya kumi. Baadhi yake zinataka kununua korosho kutoka Tanzania; Huyu mwingine anataka kujua kama Bombay Bazar na Manek Traders ni kampuni halali na wanaweza kufanya biashara nazo; kuna kijana wa Kimarekani anasema mkimbiaji mbio aliyewika miaka kama 20 iliyopita hivi ni baba yake na anataka kuwasiliana naye (sijui kama ni kweli au uongo), hata hivyo mwanariadha aliyesoma Marekani na anajua ana mtoto huko awasiliane nami nimuunganishe na mwanae; kuna wanaotaka madini; kuna wanaotaka kuuza nguo ili mradi kuna fursa mbalimbali kwa Watanzania na taifa kuongeza kipato chake.
Labda hapa tuwaambie Watanzania wanaotaka biashara hizo au ambao wametajwa hapo juu wawasiliane nami kupitia anwani yangu ya sammy.makilla@columnist.com niwaunganishe na wahusika bila malipo yoyote.
Kwanini email & internet hazitumiki
Hali hii, hata hivyo, imenifanya nijiulize hivi kweli serikali, taasisi mbalimbali na makampuni yaliyoko kwenye mtandao yanautumia kikamilifu ili kuikwamua nchi kutokana na umaskini?
Kuna wizara ambazo katika miaka hii ya sayansi na teknolojia zinatakiwa kuwa na websaiti na watu wanaofuatilia email kwa saa ishirini na nne.
Tanzania haiko tena kwenye miaka ya kulala masaa 16 kila siku jamani. Hivi kweli tutaendelea kama zaidi ya asilimia 60 ya maisha yetu hapa duniani ni ya usingizini au kwenye anasa nyingine?
Kwa mfano websaiti ya Wizara ya Nje ya Afrika ya Kusini inayoitwa Department of Foreign Affairs inayopatikana kwenye http://www.dfa.gov.za Inafanya kazi masaa ishirini na nne.
Ukituma email wakati wowote unajibiwa katika muda usiozidi saa moja. Mnaona hayo na sisi bado tumelala.
Hao wawekezaji watatoka wapi kama wakituma email hakuna anayewajibu? Taasisi zinazohusika na biashara na huduma mbalimbali na hasa kama vile bodi ya utalii, makampuni ya utalii, mahoteli, vyombo vya usafiri na kadhalika navyo kwa namna moja au nyingine lazima ziwe na mtandao hai na unaofanya kazi ikiwezekana kwa saa ishirini na nne.
Dunia ilivyo ni kuwa Tanzania ikiwa ni usiku Marekani na Japani ni asubuhi au mchana.
Bado hatujaamka na kujua ukweli huu? Tusifikiri sisi tunapolala basi watu wote duniani wamelala. Wengine ndio kwanza wanakunywa chai, wengine wamo kwenye lanchi na wengine ndio kazi zimeanza tena.
Makala hii inakusudia kutoa wito kwa Watanzania kuamka na kuanza kuchangamkia matumizi ya email na internet kwa ukamilifu kwa sababu hii sasa ndio njia muhimu ya mawasiliano ya kibiashara pengine kuliko njia nyingine yoyote duniani.
Haifai kuwa na websaiti za mapambo. Websaiti lazima ziwe ni viungo hai vinavyoiunganisha nchi na watu wengine duniani ili biashara au shughuli fulani ifanyike kwa haraka na kwa ufanisi mkubwa zaidi.
Ni tatizo gani linakwamisha…
Wanaojua ni nini kinachokwamisha kwa mfano wizara muhimu kuwa na websaiti na webmasta na wasaidizi wake wanaofanya kazi kwa kupokezana kwa masaa ishirini na nne kila siku ni wizara zinazohusika.
Sababu zinaweza kuwa za kifedha, nguvu kazi, gharama za kuweka kiunganisho cha internet na kadhalika.
Lakini kama haya ni matatizo kwanini tusiyaongelee? Kwanini serikali isivutwe sikio na kuambiwa kuwa kuna tatizo kama hili? Lakini matatizo yote haya kwa upande wangu ninaona ni matatizo ya mficha maradhi tu.
Tatizo la fedha kwa mfano linaweza likawa la urongo na kweli. Maana nina hakika katika nchi nyingi kampuni zinazotoa huduma za mtandao ziko tayari kusaidia serikali na taasisi zote zile zinazotaka kukuza uchumi wa nchi tena wakati mwingine bure. Lakini watu hao wasipofuatwa wakaelezwa shida hii hakuna atakayejua kuwa tatizo ndio hilo la kifedha.
Kuhusu utaalamu hapa serikali lazima ielezwe ukweli kuwa inapaswa kutoa mchango mkubwa ili Tanzania iwe na wataalamu wa kompyuta na shughuli zinazoendana na teknolojia hii.
Na uzuri wa kuwekeza katika sekta hii ni kuwa wataalam wa mambo haya wana soko kubwa karibu kila sehemu duniani.
Nina hakika nchi ikiwa na nia tunaweza kutoa wataalamu wa kujitosheleza na ziada ambao watatuingizia fedha za kigeni kwa kwenda kufanya kazi nchi za nje. Hao wanaobaki nyumbani watatusaidia kuifanya Tanzania kuwa namba wani kikweli kweli katika teknolojia hii muhimu katika enzi za utandawazi na ushindani mkubwa wa kiuchumi.
Serikali inastahili pongezi kwa kurahisisha upatikanaji wa vifaa vya teknolojia hii kwa bei nafuu sana ukilinganisha na sehemu nyingine Afrika. Na hili ni muhimu liendelee ili kompyuta Tanzania zifike hadi vijijini. Kama wananchi wa Ruvuma vijijini wanaweza kufanya biashara na nchi za nje kupitia mtandao, kwanini vijiji vingine navyo visifanye hivyo?
Gharama za kuunganisha
Baadhi ya wizara na taasisi mbalimbali ninaamini zilianza vibaya kwa kutumia internet ya kupitia kwenye laini za simu.
Njia hii ni ghali sana. Njia bora zaidi ni kutumia kitu kinachoitwa ‘wireless’ au kuunganishwa na mtoa huduma bila haja ya kuwepo kwa simu.
Kwa hakika gharama za mwanzo za uunganishaji ni kubwa lakini baada ya hapo internet inakuwa kama ni bure. Wizara na taasisi zote zinazostahili kuwa na mtandao lazima zitumie wireless na sio vinginevyo.
Gharama hivi sasa zinafikia milioni tatu hivi kuunganishwa. Kwanini serikali na taasisi zinazohusika zisikae chini na kuona ni jinsi gani gharama hizi zinaweza kupunguzwa. Nina hakika gharama zikifika milioni moja sio tu makampuni bali hata watu binafsi wataweza kuwa na huduma hii muhimu katika miaka ya hivi sasa.
Kingine kilichobaki na ambacho nacho kina umuhimu sawa ni hili la kuona kuwa tunakuwa na wataalamu na mafundi wengi kadri iwezekanavyo katika nyanja za kompyuta na internet.
Na hapa serikali na wabia wengine washirikiane ili Tanzania iwe ni mfano wa kuigwa Afrika baada ya Afrika Kusini katika mambo ya internet na matumizi ya kompyuta kwa ujumla.
Baadhi ya watu hao wala sio wageni ni Watanzania waliokaa nje muda mrefu au ambao wamechukua uraia wa nchi nyingine lakini hivi sasa wanataka kurejea baada ya kuvutiwa na mageuzi ya uchumi yanayoendelea nchini.
Baadhi ya maswali yao yamekuwa magumu kwangu kujibu na nikayaelekeza au nikawaelekeza wahusika kwa taasisi kama vile Wizara ya Mambo ya Nje, TCCIA, taasisi zinazohusika na utalii, Tanzania Investment Center na kadhalika.
Majibu ambayo watu waliowasiliana nami wananipa ni kuwa ama e-mail za wahusika hazifanyi kazi, nyingine zina virusi, na kwa kila hali hakuna anayewajibu wala kushughulikia shida zao.
Kwa mfano, kuna makampuni ya utalii nchini Venezuela na Brazil yaliyokuwa na watu wanaotaka kuja kutalii Tanzania. Hadi leo wanahaha kupata visa za kuja Tanzania.
Ubalozi wa karibu (naomba kusahihishwa) nadhani ni Washington lakini japo ubalozi huo una web-site na email wakala hao wanasema hakuna jibu walilolipata.
Anwani ya websaiti ya ubalozi huo ni http://www.tanzaniaembassy-us.org na kama sikosei email yao ni: balozi@tanzaniaembassy-us.org Wabrazili na Wavenezuela wanasema ni anwani bubu.
Katika websaiti hiyo pamoja na mambo mengine kuna nembo ya taifa, bendera inayopepea lakini inaelekea anwani ya barua pepe yao haipepei na kuna twiga anayekimbia na maneno -TANZANIA ON THE GO- lakini inaelekea kwa hakika sivyo bado Tanzania imelala katika kutumia mtandao ili kukuza uchumi wake kutokana na biashara nyingi ambazo hivi leo zinafanyika kwa kutumia email na internet.
Kuna bwana yuko Uarabuni anataka kuanza biashara ya kununua na kuuza mifugo na Tanzania. Inaelekea huyu kazaliwa hapa maana anazungumza Kiswahili fasaha. Nimejaribu kumuelekeza kwa wahusika lakini anasema hapati majibu anaomba mimi nimsaidie. Lakini ninadhani kuna walioajiriwa kufanya kazi hiyo au sio-pengine Wizara inayohusika inaweza kumsaidia kwa kuwasiliana nami.
Leo ninapoandika makala hii nina barua pepe zaidi ya kumi. Baadhi yake zinataka kununua korosho kutoka Tanzania; Huyu mwingine anataka kujua kama Bombay Bazar na Manek Traders ni kampuni halali na wanaweza kufanya biashara nazo; kuna kijana wa Kimarekani anasema mkimbiaji mbio aliyewika miaka kama 20 iliyopita hivi ni baba yake na anataka kuwasiliana naye (sijui kama ni kweli au uongo), hata hivyo mwanariadha aliyesoma Marekani na anajua ana mtoto huko awasiliane nami nimuunganishe na mwanae; kuna wanaotaka madini; kuna wanaotaka kuuza nguo ili mradi kuna fursa mbalimbali kwa Watanzania na taifa kuongeza kipato chake.
Labda hapa tuwaambie Watanzania wanaotaka biashara hizo au ambao wametajwa hapo juu wawasiliane nami kupitia anwani yangu ya sammy.makilla@columnist.com niwaunganishe na wahusika bila malipo yoyote.
Kwanini email & internet hazitumiki
Hali hii, hata hivyo, imenifanya nijiulize hivi kweli serikali, taasisi mbalimbali na makampuni yaliyoko kwenye mtandao yanautumia kikamilifu ili kuikwamua nchi kutokana na umaskini?
Kuna wizara ambazo katika miaka hii ya sayansi na teknolojia zinatakiwa kuwa na websaiti na watu wanaofuatilia email kwa saa ishirini na nne.
Tanzania haiko tena kwenye miaka ya kulala masaa 16 kila siku jamani. Hivi kweli tutaendelea kama zaidi ya asilimia 60 ya maisha yetu hapa duniani ni ya usingizini au kwenye anasa nyingine?
Kwa mfano websaiti ya Wizara ya Nje ya Afrika ya Kusini inayoitwa Department of Foreign Affairs inayopatikana kwenye http://www.dfa.gov.za Inafanya kazi masaa ishirini na nne.
Ukituma email wakati wowote unajibiwa katika muda usiozidi saa moja. Mnaona hayo na sisi bado tumelala.
Hao wawekezaji watatoka wapi kama wakituma email hakuna anayewajibu? Taasisi zinazohusika na biashara na huduma mbalimbali na hasa kama vile bodi ya utalii, makampuni ya utalii, mahoteli, vyombo vya usafiri na kadhalika navyo kwa namna moja au nyingine lazima ziwe na mtandao hai na unaofanya kazi ikiwezekana kwa saa ishirini na nne.
Dunia ilivyo ni kuwa Tanzania ikiwa ni usiku Marekani na Japani ni asubuhi au mchana.
Bado hatujaamka na kujua ukweli huu? Tusifikiri sisi tunapolala basi watu wote duniani wamelala. Wengine ndio kwanza wanakunywa chai, wengine wamo kwenye lanchi na wengine ndio kazi zimeanza tena.
Makala hii inakusudia kutoa wito kwa Watanzania kuamka na kuanza kuchangamkia matumizi ya email na internet kwa ukamilifu kwa sababu hii sasa ndio njia muhimu ya mawasiliano ya kibiashara pengine kuliko njia nyingine yoyote duniani.
Haifai kuwa na websaiti za mapambo. Websaiti lazima ziwe ni viungo hai vinavyoiunganisha nchi na watu wengine duniani ili biashara au shughuli fulani ifanyike kwa haraka na kwa ufanisi mkubwa zaidi.
Ni tatizo gani linakwamisha…
Wanaojua ni nini kinachokwamisha kwa mfano wizara muhimu kuwa na websaiti na webmasta na wasaidizi wake wanaofanya kazi kwa kupokezana kwa masaa ishirini na nne kila siku ni wizara zinazohusika.
Sababu zinaweza kuwa za kifedha, nguvu kazi, gharama za kuweka kiunganisho cha internet na kadhalika.
Lakini kama haya ni matatizo kwanini tusiyaongelee? Kwanini serikali isivutwe sikio na kuambiwa kuwa kuna tatizo kama hili? Lakini matatizo yote haya kwa upande wangu ninaona ni matatizo ya mficha maradhi tu.
Tatizo la fedha kwa mfano linaweza likawa la urongo na kweli. Maana nina hakika katika nchi nyingi kampuni zinazotoa huduma za mtandao ziko tayari kusaidia serikali na taasisi zote zile zinazotaka kukuza uchumi wa nchi tena wakati mwingine bure. Lakini watu hao wasipofuatwa wakaelezwa shida hii hakuna atakayejua kuwa tatizo ndio hilo la kifedha.
Kuhusu utaalamu hapa serikali lazima ielezwe ukweli kuwa inapaswa kutoa mchango mkubwa ili Tanzania iwe na wataalamu wa kompyuta na shughuli zinazoendana na teknolojia hii.
Na uzuri wa kuwekeza katika sekta hii ni kuwa wataalam wa mambo haya wana soko kubwa karibu kila sehemu duniani.
Nina hakika nchi ikiwa na nia tunaweza kutoa wataalamu wa kujitosheleza na ziada ambao watatuingizia fedha za kigeni kwa kwenda kufanya kazi nchi za nje. Hao wanaobaki nyumbani watatusaidia kuifanya Tanzania kuwa namba wani kikweli kweli katika teknolojia hii muhimu katika enzi za utandawazi na ushindani mkubwa wa kiuchumi.
Serikali inastahili pongezi kwa kurahisisha upatikanaji wa vifaa vya teknolojia hii kwa bei nafuu sana ukilinganisha na sehemu nyingine Afrika. Na hili ni muhimu liendelee ili kompyuta Tanzania zifike hadi vijijini. Kama wananchi wa Ruvuma vijijini wanaweza kufanya biashara na nchi za nje kupitia mtandao, kwanini vijiji vingine navyo visifanye hivyo?
Gharama za kuunganisha
Baadhi ya wizara na taasisi mbalimbali ninaamini zilianza vibaya kwa kutumia internet ya kupitia kwenye laini za simu.
Njia hii ni ghali sana. Njia bora zaidi ni kutumia kitu kinachoitwa ‘wireless’ au kuunganishwa na mtoa huduma bila haja ya kuwepo kwa simu.
Kwa hakika gharama za mwanzo za uunganishaji ni kubwa lakini baada ya hapo internet inakuwa kama ni bure. Wizara na taasisi zote zinazostahili kuwa na mtandao lazima zitumie wireless na sio vinginevyo.
Gharama hivi sasa zinafikia milioni tatu hivi kuunganishwa. Kwanini serikali na taasisi zinazohusika zisikae chini na kuona ni jinsi gani gharama hizi zinaweza kupunguzwa. Nina hakika gharama zikifika milioni moja sio tu makampuni bali hata watu binafsi wataweza kuwa na huduma hii muhimu katika miaka ya hivi sasa.
Kingine kilichobaki na ambacho nacho kina umuhimu sawa ni hili la kuona kuwa tunakuwa na wataalamu na mafundi wengi kadri iwezekanavyo katika nyanja za kompyuta na internet.
Na hapa serikali na wabia wengine washirikiane ili Tanzania iwe ni mfano wa kuigwa Afrika baada ya Afrika Kusini katika mambo ya internet na matumizi ya kompyuta kwa ujumla.
Tutawashingilia wengine hadi lini?
Watanzania ni Waafrika na wiki hii wana kila sababu ya kuishangilia timu pekee ya Afrika iliyobaki katika kinyang’anyiro cha Kombe la Dunia huko Japan na Korea mwaka huu wa 2002.
Kwa kuwa Tanzania na Afrika Mashariki kwa ujumla hazikufuzu basi wawakilishi wetu sasa ni timu ya Taifa ya Senegal, nchi iliyoko huko Afrika Magharibi.
Historia ya Kombe la Dunia inaonesha Afrika Mashariki haijawahi kutoa timu yenye kiwango cha mpira wa Kombe la Dunia. Ni Afrika Kaskazini, Afrika Magharibi na Afrika ya Kati tu zinazochukua nafasi hizo mwaka nenda, mwaka rudi.
Swali hapa ni je, tutaendelea kuwashangilia wenzetu hawa mpaka lini? Nchi za Afrika Mashariki kila moja peke yake na zote kwa umoja wao haziwezi kuweka mkakati wa kuhakikisha zinasaidiana kuwa angalau na timu moja ya nchi hizi (pamoja na Rwanda na Burundi) kwenda Kombe la Dunia?
Njia ya mkato kwenda Kombe la Dunia
Njia ya mkato kwenda Kombe la Dunia ni kuhakikisha kuwa bara la Afrika na nchi ya Marekani (USA) zinagawanya katika sehemu tano tano (kutokana na nchi/majimbo yao).
Kila moja itoe timu 5 za Taifa (ili kuhakikisha uwakilishi unaoenda kwa uwiano wa idadi ya watu na nchi/majimbo). Afrika iwakilishwe na timu 10 kwa utaratibu wa Afrika Magharibi-timu 3; Afrika Kaskazini-timu 2; Afrika ya Kati –timu 2; Visiwa vya Afrika-timu 1; Afrika Mashariki-timu 1 na Afrika Kusini-timu 1.
Hili litakuwa ni jibu zuri kwa Ulaya ambayo inatoa timu nyingi zaidi kuliko wingi wa watu na ukubwa wa eneo hilo la dunia.
Marekani (USA) kwa kuwa ndiyo imeanza kuchangamkia mpira wa miguu itoe timu tano-kila moja toka Kaskazini, Kusini, Kati, Magharibi na Mashariki. Kwa kufanya hivi FIFA itachangia kasi ya kukubalika kwa soka huko Marekani na hivyo kuongeza utamu na sifa ya mchezo huu kuwa namba moja duniani.
Lakini kama nilivyosema hii ndio njia ya mkato kwenda Kombe la Dunia. Kwa bahati mbaya FIFA inaweza ikachukua miaka 10 kufanya mabadiliko kama haya. Je, tusubiri hadi mteremko au tuwe ngangari na kupambana na hali halisi ya sasa ili tutoe timu ya hadhi ya kimataifa?
Uongozi na maendeleo
Tupende tusipende, michezo kwa kiasi fulani inategemea ari ya kiongozi aliyeko kwenye kigoda. Tazama mashirika au taasisi nyingi ambazo zimewahi kutoa timu bora utakuta kiongozi wa juu mahala pale alikuwa mwanamichezo namba moja yeye mwenyewe au shabiki wa kutupwa wa timu yake ya michezo.
Kwa taifa pia hali si tofauti. Kama kiongozi wa nchi anajali, anathamini na anachangia kuendeleza michezo, vijana wake wanaweza kufanya maajabu katika viwanja vya michezo mahala popote pale duniani.
Wala tusiende mbali. Tazama China ya Mao Dze Dung; Ujerumani Mashariki ya wakati ule; na Cuba ya Castro. Karibu na nyumbani Nelson Mandela kama shabiki wa mpira, ngumi na michezo mingine amechangia sio haba kuwafanya vijana wa Afrika Kusini kuwika kimichezo haraka kuliko ilivyotarajiwa.
Ni dhahiri kuwa pamoja na kazi nzuri inayofanywa na uongozi wa nchi kutilia mkazo michezo majukwaani au bungeni bado kuna kazi kubwa ya wao kuonekana wanaichukulia michezo sio kama michezo (kitu cha bure na kisicho na maana) bali kama kazi au ajira ya uhakika kwa maelfu ya vijana ambao kwa namna nyingine yoyote hawatobahatika kuajiriwa.
Na ajira, mathalani, katika mpira wa miguu ikiwa ni nje ya nchi inalipa mara kadhaa ukilinganisha na kazi zenye vyeo vya juu hapa nchini.
Wizara inayohusika na michezo ina kazi kubwa ya kuhakikisha kuwa tunaondoa uswahili na ushambenga katika vilabu na vyama vya michezo. Ni lazima viongozi wa vilabu na vyama wawe sio tu ni wanamichezo bali wana taaluma ya menejimenti na uongozi bora ili waweze kuendeleza nchi kimichezo. Huu si wakati wa kuvumilia viongozi wababaishaji, mbumbumbu na wasiojua dunia inakwenda wapi kimichezo.
Uhasibu na Ukaguzi
Viongozi wababaishaji hugeuza vilabu na vyama vya michezo kama mahala pa kutafuna fedha ya wajinga au mali isiyo na mwenyewe. Wakati umefika sasa wa kulazimisha kila klabu na kila chama cha michezo sio tu kuwa na mhasibu wa kutengeneza mahesabu yake lakini pia wakaguzi wa ndani na wa nje kukagua mahesabu hayo kwa vipindi maalum vitakavyowekwa.
Binadamu hakamiliki ila….
Michezo ni sehemu ya utu wetu. Kitendo chochote kinachomnyang’anya Mtanzania michezo ni kitendo cha kupunguza utu na heshima ya Mtanzania.
Na katika miaka ya leo ambapo michezo hutoa ajira maridhawa kuliko tarafu za aina nyingine ni kumpora mtu pia mkate wake wa kila siku na fursa yake ya kuukata kutokana na michezo.
Kama walipa kodi Watanzania wote kwa umoja wao wana haki ya kudai mitaa, vijiji, kata, tarafa, wilaya na mikoa yao kuwapa viwanja vya michezo.
Hivi sasa kumejitokeza tabia potofu ya viongozi mbalimbali kuona, mathalani, kuwa na majengo ya shule tu ni bora kuliko kuwa na viwanja vizuri na michezo kwa watoto wetu.
Na katika shule hizo ni asilimia ndogo tu itakayopata ajira maofisini au katika makampuni mbalimbali nchini. Laiti kungelikuwa na viwanja vya kutosha vya michezo basi wanafunzi wengi zaidi wangelipatiwa fursa ya kujiajiri wenyewe kama wachezaji soka, tenisi, masumbwi, riadha na kadhalika.
Kwa maneno mengine, viongozi wetu bado hawajatambua umuhimu wa michezo kiuchumi na kijamii na bado wanang’ng’ania kutaka kuiendesha michezo kama sehemu ya siasa.
Michezo kama siasa huendeshwa kwa lengo la kuwapatia viongozi sifa. Michezo kama shughuli ya kiuchumi na kijamii huendelezwa ili kuwapatia vijana ajira inayowawezesha kukimu maisha yao na pia kuwanyanyua kimaisha wazazi na jamaa zao.
Haimsaidii kiongozi yeyote wala taifa kupuuza maendeleo ya kimichezo ya kijana yeyote hata kama sio ndugu yake. Kwa yakini kitu kama hicho hulipunguzia taifa nafasi ya kuingiza mapato dhahiri toka nje.
Ili tunyanyue michezo
Kwangu binafsi ni kosa kuwanyima watoto wa chekechea na shule za msingi nafasi ya kucheza na kukua kutokana na michezo.
Wanasaikolojia wanashauri kwa usahihi kabisa kuwa asilimia kubwa ya muda katika chekechea utumike katika michezo ili kuwa na makuzi yanayowiana kati ya mwili na akili; katika shule za msingi muda wa kusoma na michezo uwe ni hamsini kwa hamsini; katika sekondari na vyuo vya juu iwe ni asilimia 75 (masomo) kwa 25 (michezo). Uwiano huu unafaa kufuatwa pia hata baada ya kumaliza chuo kama mtu anataka aepuke magonjwa mbalimbali yanayosababishwa na kukosa mazoezi ya kutosha (ikiwemo shinikizo la damu, vitambi kwa polisi na viongozi wa michezo).
Kuwekeza katika michezo
Michezo ni kwa ajili ya wote. Kama hivyo ndivyo hii ina maana michezo ni sawa na usalama na ulinzi (kulinda afya za Watanzania na pengine maadili mema); michezo ni sawa na huduma ya afya (kila mtu ahudumiwe); na michezo ni nishati muhimu kuijenga rasilimali muhimu kuliko zote katika taifa-watu.
Kama ndivyo pamoja na watu wenyewe, serikali kuu na serikali za mitaa lazima ziwekeze katika miundo-mbinu ya michezo.
Ianzishwe kampeni ya kuijenga Tanzania upya kimichezo na katika kampeni hiyo kila mtaa, kijiji, kata, tarafa lazima iwe na viwanja vya michezo ya aina zote. Na miongozo na taratibu ziwepo za kuviendesha ili kufikia malengo ya kutoa wanamichezo bora baadaye.
Timu kwa daraja mbalimbali
Pendekezo linaloweza kwenda mbali katika kuendeleza soka na michezo mingine hapa nchini ni kuhakikisha kuwa panakuwa na timu za mtaa, kata, tarafa, wilaya, mikoa na taifa kwa kila mchezo.
Njia zitafutwe kuhakikisha kuwa michezo inakuwa ni sehemu ya kazi/masomo na panakuwa na mashindano wakati wote ili kuhakikisha nchi hii ina wanamichezo walioko kwenye fomu wakati wowote.
Ni muhimu kwa hivyo mitaa, kata, vijiji, tarafa, wilaya, mkoa na taifa kuwa na bajeti za wazi zinazoonesha mapato na matumizi katika michezo mbalimbali. Japan na Korea kama wenyeji wa Kombe la Dunia wamepata faida kadhaa mojawapo ni ile ya kiuchumi au kibiashara. Vijiji, miji, wilaya, mikoa na nchi inatakiwa kuiga mfano huu na kuutumia kujineemesha kwa namna moja au nyingine.
Aidha lazima tuwe na makocha au walimu wa kimataifa na tusijidanganye na watu wasiofuzu au kuwa na uzoefu wa kusimamia timu za kitaifa. Hii si gharama kubwa kama tunaweza kuwalipa mameneja wa kampuni moja tu mamilioni, kwanini tushindwe kwa kocha wa taifa zima? Tena wakati FIFA inamwaga mapesa Afrika.
Kwa kumalizia nirudie tu kuwa kama Tanzania haitajizatiti kwa namna hiyo hapo juu kimichezo basi kuna hatari ya nchi hii kuwa Dunia ya Tatu kama sio ya nne kimichezo katika bara hili hili la Afrika wakati nchi kama Senegal, Cameroun na Bourkina Fasso zikiwa Dunia ya kwanza.
Kwa kuwa Tanzania na Afrika Mashariki kwa ujumla hazikufuzu basi wawakilishi wetu sasa ni timu ya Taifa ya Senegal, nchi iliyoko huko Afrika Magharibi.
Historia ya Kombe la Dunia inaonesha Afrika Mashariki haijawahi kutoa timu yenye kiwango cha mpira wa Kombe la Dunia. Ni Afrika Kaskazini, Afrika Magharibi na Afrika ya Kati tu zinazochukua nafasi hizo mwaka nenda, mwaka rudi.
Swali hapa ni je, tutaendelea kuwashangilia wenzetu hawa mpaka lini? Nchi za Afrika Mashariki kila moja peke yake na zote kwa umoja wao haziwezi kuweka mkakati wa kuhakikisha zinasaidiana kuwa angalau na timu moja ya nchi hizi (pamoja na Rwanda na Burundi) kwenda Kombe la Dunia?
Njia ya mkato kwenda Kombe la Dunia
Njia ya mkato kwenda Kombe la Dunia ni kuhakikisha kuwa bara la Afrika na nchi ya Marekani (USA) zinagawanya katika sehemu tano tano (kutokana na nchi/majimbo yao).
Kila moja itoe timu 5 za Taifa (ili kuhakikisha uwakilishi unaoenda kwa uwiano wa idadi ya watu na nchi/majimbo). Afrika iwakilishwe na timu 10 kwa utaratibu wa Afrika Magharibi-timu 3; Afrika Kaskazini-timu 2; Afrika ya Kati –timu 2; Visiwa vya Afrika-timu 1; Afrika Mashariki-timu 1 na Afrika Kusini-timu 1.
Hili litakuwa ni jibu zuri kwa Ulaya ambayo inatoa timu nyingi zaidi kuliko wingi wa watu na ukubwa wa eneo hilo la dunia.
Marekani (USA) kwa kuwa ndiyo imeanza kuchangamkia mpira wa miguu itoe timu tano-kila moja toka Kaskazini, Kusini, Kati, Magharibi na Mashariki. Kwa kufanya hivi FIFA itachangia kasi ya kukubalika kwa soka huko Marekani na hivyo kuongeza utamu na sifa ya mchezo huu kuwa namba moja duniani.
Lakini kama nilivyosema hii ndio njia ya mkato kwenda Kombe la Dunia. Kwa bahati mbaya FIFA inaweza ikachukua miaka 10 kufanya mabadiliko kama haya. Je, tusubiri hadi mteremko au tuwe ngangari na kupambana na hali halisi ya sasa ili tutoe timu ya hadhi ya kimataifa?
Uongozi na maendeleo
Tupende tusipende, michezo kwa kiasi fulani inategemea ari ya kiongozi aliyeko kwenye kigoda. Tazama mashirika au taasisi nyingi ambazo zimewahi kutoa timu bora utakuta kiongozi wa juu mahala pale alikuwa mwanamichezo namba moja yeye mwenyewe au shabiki wa kutupwa wa timu yake ya michezo.
Kwa taifa pia hali si tofauti. Kama kiongozi wa nchi anajali, anathamini na anachangia kuendeleza michezo, vijana wake wanaweza kufanya maajabu katika viwanja vya michezo mahala popote pale duniani.
Wala tusiende mbali. Tazama China ya Mao Dze Dung; Ujerumani Mashariki ya wakati ule; na Cuba ya Castro. Karibu na nyumbani Nelson Mandela kama shabiki wa mpira, ngumi na michezo mingine amechangia sio haba kuwafanya vijana wa Afrika Kusini kuwika kimichezo haraka kuliko ilivyotarajiwa.
Ni dhahiri kuwa pamoja na kazi nzuri inayofanywa na uongozi wa nchi kutilia mkazo michezo majukwaani au bungeni bado kuna kazi kubwa ya wao kuonekana wanaichukulia michezo sio kama michezo (kitu cha bure na kisicho na maana) bali kama kazi au ajira ya uhakika kwa maelfu ya vijana ambao kwa namna nyingine yoyote hawatobahatika kuajiriwa.
Na ajira, mathalani, katika mpira wa miguu ikiwa ni nje ya nchi inalipa mara kadhaa ukilinganisha na kazi zenye vyeo vya juu hapa nchini.
Wizara inayohusika na michezo ina kazi kubwa ya kuhakikisha kuwa tunaondoa uswahili na ushambenga katika vilabu na vyama vya michezo. Ni lazima viongozi wa vilabu na vyama wawe sio tu ni wanamichezo bali wana taaluma ya menejimenti na uongozi bora ili waweze kuendeleza nchi kimichezo. Huu si wakati wa kuvumilia viongozi wababaishaji, mbumbumbu na wasiojua dunia inakwenda wapi kimichezo.
Uhasibu na Ukaguzi
Viongozi wababaishaji hugeuza vilabu na vyama vya michezo kama mahala pa kutafuna fedha ya wajinga au mali isiyo na mwenyewe. Wakati umefika sasa wa kulazimisha kila klabu na kila chama cha michezo sio tu kuwa na mhasibu wa kutengeneza mahesabu yake lakini pia wakaguzi wa ndani na wa nje kukagua mahesabu hayo kwa vipindi maalum vitakavyowekwa.
Binadamu hakamiliki ila….
Michezo ni sehemu ya utu wetu. Kitendo chochote kinachomnyang’anya Mtanzania michezo ni kitendo cha kupunguza utu na heshima ya Mtanzania.
Na katika miaka ya leo ambapo michezo hutoa ajira maridhawa kuliko tarafu za aina nyingine ni kumpora mtu pia mkate wake wa kila siku na fursa yake ya kuukata kutokana na michezo.
Kama walipa kodi Watanzania wote kwa umoja wao wana haki ya kudai mitaa, vijiji, kata, tarafa, wilaya na mikoa yao kuwapa viwanja vya michezo.
Hivi sasa kumejitokeza tabia potofu ya viongozi mbalimbali kuona, mathalani, kuwa na majengo ya shule tu ni bora kuliko kuwa na viwanja vizuri na michezo kwa watoto wetu.
Na katika shule hizo ni asilimia ndogo tu itakayopata ajira maofisini au katika makampuni mbalimbali nchini. Laiti kungelikuwa na viwanja vya kutosha vya michezo basi wanafunzi wengi zaidi wangelipatiwa fursa ya kujiajiri wenyewe kama wachezaji soka, tenisi, masumbwi, riadha na kadhalika.
Kwa maneno mengine, viongozi wetu bado hawajatambua umuhimu wa michezo kiuchumi na kijamii na bado wanang’ng’ania kutaka kuiendesha michezo kama sehemu ya siasa.
Michezo kama siasa huendeshwa kwa lengo la kuwapatia viongozi sifa. Michezo kama shughuli ya kiuchumi na kijamii huendelezwa ili kuwapatia vijana ajira inayowawezesha kukimu maisha yao na pia kuwanyanyua kimaisha wazazi na jamaa zao.
Haimsaidii kiongozi yeyote wala taifa kupuuza maendeleo ya kimichezo ya kijana yeyote hata kama sio ndugu yake. Kwa yakini kitu kama hicho hulipunguzia taifa nafasi ya kuingiza mapato dhahiri toka nje.
Ili tunyanyue michezo
Kwangu binafsi ni kosa kuwanyima watoto wa chekechea na shule za msingi nafasi ya kucheza na kukua kutokana na michezo.
Wanasaikolojia wanashauri kwa usahihi kabisa kuwa asilimia kubwa ya muda katika chekechea utumike katika michezo ili kuwa na makuzi yanayowiana kati ya mwili na akili; katika shule za msingi muda wa kusoma na michezo uwe ni hamsini kwa hamsini; katika sekondari na vyuo vya juu iwe ni asilimia 75 (masomo) kwa 25 (michezo). Uwiano huu unafaa kufuatwa pia hata baada ya kumaliza chuo kama mtu anataka aepuke magonjwa mbalimbali yanayosababishwa na kukosa mazoezi ya kutosha (ikiwemo shinikizo la damu, vitambi kwa polisi na viongozi wa michezo).
Kuwekeza katika michezo
Michezo ni kwa ajili ya wote. Kama hivyo ndivyo hii ina maana michezo ni sawa na usalama na ulinzi (kulinda afya za Watanzania na pengine maadili mema); michezo ni sawa na huduma ya afya (kila mtu ahudumiwe); na michezo ni nishati muhimu kuijenga rasilimali muhimu kuliko zote katika taifa-watu.
Kama ndivyo pamoja na watu wenyewe, serikali kuu na serikali za mitaa lazima ziwekeze katika miundo-mbinu ya michezo.
Ianzishwe kampeni ya kuijenga Tanzania upya kimichezo na katika kampeni hiyo kila mtaa, kijiji, kata, tarafa lazima iwe na viwanja vya michezo ya aina zote. Na miongozo na taratibu ziwepo za kuviendesha ili kufikia malengo ya kutoa wanamichezo bora baadaye.
Timu kwa daraja mbalimbali
Pendekezo linaloweza kwenda mbali katika kuendeleza soka na michezo mingine hapa nchini ni kuhakikisha kuwa panakuwa na timu za mtaa, kata, tarafa, wilaya, mikoa na taifa kwa kila mchezo.
Njia zitafutwe kuhakikisha kuwa michezo inakuwa ni sehemu ya kazi/masomo na panakuwa na mashindano wakati wote ili kuhakikisha nchi hii ina wanamichezo walioko kwenye fomu wakati wowote.
Ni muhimu kwa hivyo mitaa, kata, vijiji, tarafa, wilaya, mkoa na taifa kuwa na bajeti za wazi zinazoonesha mapato na matumizi katika michezo mbalimbali. Japan na Korea kama wenyeji wa Kombe la Dunia wamepata faida kadhaa mojawapo ni ile ya kiuchumi au kibiashara. Vijiji, miji, wilaya, mikoa na nchi inatakiwa kuiga mfano huu na kuutumia kujineemesha kwa namna moja au nyingine.
Aidha lazima tuwe na makocha au walimu wa kimataifa na tusijidanganye na watu wasiofuzu au kuwa na uzoefu wa kusimamia timu za kitaifa. Hii si gharama kubwa kama tunaweza kuwalipa mameneja wa kampuni moja tu mamilioni, kwanini tushindwe kwa kocha wa taifa zima? Tena wakati FIFA inamwaga mapesa Afrika.
Kwa kumalizia nirudie tu kuwa kama Tanzania haitajizatiti kwa namna hiyo hapo juu kimichezo basi kuna hatari ya nchi hii kuwa Dunia ya Tatu kama sio ya nne kimichezo katika bara hili hili la Afrika wakati nchi kama Senegal, Cameroun na Bourkina Fasso zikiwa Dunia ya kwanza.
Subscribe to:
Posts (Atom)
