Sunday, March 27, 2011

Ajali, fidia na Mtanzania

Ajali, fidia na Mtanzania

NI wakati kama huu wa ajali ndipo Watanzania wengi wanapotambua kwamba sio tu hawana kinga dhidi ya ajali lakini pia baada ya ajali kutokea wanaweza wasipate msaada wa maana kuendelea na maisha yao.

Watetezi wa umma, hata hivyo, huu ndio wakati wa kuingilia kati na kujaribu kuubadili mfumo uliopo ili uangalie pia maslahi ya wanyonge na wasio nacho katika jamii.

Wenye nacho na walioko madarakani hawana sababu ya kuwapenda wanaotetea maslahi ya walio wengi. Lakini vile vile watetezi wa umma hawana sababu ya kuwaogopa wenye nacho na walioko madarakani katika kutetea haki za wanyonge. Huu ni wito na sio kazi ya kutafuta cheo au ukubwa au utajiri.

Mfumo uliopo
Mfumo wa bima na fidia uliopo hivi sasa umejengwa katika mihimili ya kuwasaidia walionacho na wakubwa.

Mnyonge hana nafasi katika mfumo huu. Ukitaka ushahidi nenda kawahoji walioathirika na ajali kama zile za MV Bukoba, ajali mbalimbali za mabasi na majini nchini kwa miaka tuseme saba tu iliyopita. Kadhalika kawahoji watu wa Merelani kwa matukio mawili matatu na usikie fidia waliyopata.

Ukitoka hapo kaangalie upande wa pili na mahesabu ya mashirika ya bima kuhusu ajali zilizowahusu walionacho na wenye nchi.

Baada ya maswali na udadisi huo utagundua kuwa mfumo wa bima na fidia upo kwa ajili ya tabaka fulani tu katika jamii na sio kwa umma wote.

Swali linakuja. Je, huu ndio mfumo nchi kama yetu yenye asili ya kijamaa unaostahili kuwa nao? Kweli kuna sababu ya kuruhusu mfumo huu uendelee au kwa maneno mengine kwanini mfumo huu bado unalindwa? Je, maslahi ya wengi yakiangaliwa yale ya wachache yatapotea?

Kama mabadiliko yanahitajika, je, nchi hii inahitaji mfumo gani wa bima na fidia kwa faida ya umma?

Mashirika ya umma na fidia
Eti kwa kuwa TANESCO, DAWASA, TRC, ATC na mashirika mengine enzi hizo yalikuwa ya umma ilikuwa haiyumkiniki mtu kufidiwa kitu.

Si mnakumbuka wale ambao friji, TV, redio na vyombo vyenu vingine vya nyumbani vilivyoharibiwa na umeme wa TANESCO? Wangapi kati yenu walilipwa fidia?

Treni hadi leo ikisababisha ajali hata kama ni kwa uzembe wa shirika husika eti ni wewe mpita njia ndiye unayewajibika na sio wao. Makubwa haya jama.
Pamoja na haya yote ni kwamba hakuna shirika linalowajibishwa hapa nchini hivi sasa kwa kushindwa kutimiza upande wake wa mkataba iwe ni kutoa huduma au kuuza bidhaa mbovu kwa wananchi.

Mtanzania kwa kifupi hana haki kabisa dhidi ya mashirika yanayotakiwa kumpatia bidhaa au huduma. Yakimpatia huduma au bidhaa safi na bora sawa. Yakitoa huduma ovyo na bidhaa zilizooza sawa! Hataweza kuyashtaki na kuambulia chochote katika mfumo uliopo.

Sheria na udhibiti wa uzembe
Ieleweke kuwa kazi mojawapo ya sheria na katiba ya nchi yoyote ile ni kulinda raia na mali zao. Sheria na katiba inayoshindwa kufanya hili inakuwa na walakini.

Vyombo vya sheria vina jukumu sio tu la kuona kuna sheria fulani lakini kuhakikisha kuwa sheria hizo zinakwenda na wakati na zinatimiza yale ambayo katika macho ya jamii ni haki na wajibu.

Mojawapo kati ya mambo hayo ni kuona kuwa raia na wasio raia wanapata fidia maridhawa pale wanapofikwa na janga lolote nyumbani, kazini au safarini. Jingine ni kuhakikisha kuwa sheria inatumika kama kinga dhidi ya ulegevu na uzembe unaoweza kusababisha kifo au mtu kuwa kilema maisha yake yote.

Kifo kinapomkuta, kwa mfano, msafiri wa treni ina maana kuna familia na hasa watoto watakaokosa baba au mama. Je, ni nani atawalea hawa? Sheria ina haki kunyamaza kuhusu hili?

Jamaa huyo huyo anaweza akawa pia alikuwa akitegemewa na wazazi wake-baba, mama na pengine kwa mila zetu za Kiafrika-babu na bibi. Na pengine baba huyo ndio wale jamaa waliostaafishwa na jumuia ya Afrika Mashariki na kulipwa sh. 320 kama mafao. Ni nani atawatunza wazee hawa? Sheria inaliona hili?

Katika kujadili masuala kama haya ni wazi kuwa hatma ya yote itaonekana kuwa Tanzania haina mfumo wa bima na fidia unaoweza kuwalinda Watanzania walio wengi wakati wa maafa ya aina yoyote ile.

Kwa mantiki hii kazi iliyobaki ni kwa vyombo vya sheria vikipata changamoto kutoka vikundi vya hiari na taasisi nyingine zinazotetea maslahi ya wanyonge kuhakikisha nchi inakuwa na sheria zitakazowesha kuwa na jamii na uchumi usiotetereshwa na maafa na majanga.

Aidha ni muhimu kuwa na mfumo unaolinda nchi na watu wake dhidi ya uzembe wa wenye mali.

Kwa mfano, hivi kuna ugumu gani kuwa na sheria itakayotaka familia ifidiwe shilingi milioni 5 -10 kwa kupoteza jamaa yao? Fidia ya milioni 1-2 kwa mtu kuvunjika mguu?

Je, kwa namna hii kuna dereva, meneja au mwenye gari au chombo cha usafiri atakayecheza na maisha ya watu.

Kwa mantiki hii kama inaonekana uzembe ulifanyika na kisha kusababisha ajali basi fidia inaweza kuwa mara mbili au zaidi ya hapo.

Fidia ni njia pekee inayoweza kuwasaidia watoto na wajukuu wanaobaki bila mtafuta riziki wake. Fidia ni njia pekee inayoweza kuwasaidia wazazi waliozeeka wanaoachwa bila mtu wa kuwasaidia.

Fidia ni njia pekee inayoweza kumsaidia mtu anayefanywa kilema katika ajali fulani aweze kujitegemea kimaisha. Kukiwa na mfumo wa bima na fidia unaowezesha hayo hapo juu ni dhahiri kuwa nchi itanufaika pia kiuchumi.

Kutokana na kuzungusha upya pato la nchi linalokwenda aghalabu zaidi kwa wachache basi kunakuwa na msukumo mkubwa zaidi wa uzalishaji mali utakaonufaisha sehemu mpya na sio zile za asili tu.

Ulaya, Marekani na fidia
Ingawa Tanzania haiwezi kuwa kama Marekani na Ulaya katika masuala ya bima na fidia ni muhimu hata hivyo kujifunza falsafa iliyowafanya waheshimu na kuendeleza mfumo wa sheria unaowanufaisha watu wanaoathirika kwa maafa mbalimbali.

Anayeumia kidole kazini, kwa mfano, huko Ulaya au Marekani anaweza akajikuta ametajirika fumba na kufumbua.

Watoto na wazazi wanaowategemea wengine huwa hawaambulii patupu wanapompoteza mtafutaji wao katika ajali iliyosababishwa na uzembe wa wengine na pengine hata maafa yalio nje ya kazi za binadamu. Kwa mfano moto unaochanja mbuga huko Texas hivi sasa. Hakuna aliyeusababisha lakini wote waliopoteza makazi yao huko wanaweza kuja kufidiwa kwa namna moja au nyingine.

Huu ni mfumo kwa kweli unaowapa watu imani na nchi yao, wananchi wenzao na serikali yao. Nadharia yake sio ngeni katika masikio yetu. Miaka kadhaa iliyopita Mwalimu J.K. Nyerere katika Ujamaa wa Kiafrika alilizungumzia hili.

Kama jamii ya wakati huo iliweza kumpa msaada mtu na kumwezesha kurejea maisha yake ya zamani kwa kiasi fulani kwanini leo nchi na taasisi zake za fedha ishindwe kuiga mfano huu unaotokana na mila na utamaduni wetu?

Bima ya umma
Ni dhahiri kuwa hakuna mwenye basi, mwenye meli au ndege atakayesumbuliwa na suala hili la bima na fidia kwa wanaofikwa na balaa wakisafiri katika vyombo vyao.

Huu ndio ukweli wa binadamu na mali yake. Hujali mali yake zaidi kuliko maisha ya watu wengine. Kama ndivyo, je, sio jukumu la serikali ya watu kuingilia kati hapa.

Ninapendekeza kuwa kwa kila abiria anayesafiri na basi, meli, ndege serikali itoze sh. 100 tu kuanzisha mfuko wa Bima dhidi ya ajali za vyombo vya usafiri.

Tusiwasumbue wenye vyombo vya usafiri katika hili. Njia rahisi ni kukadiria kuwa kwa mwezi chombo fulani, mathalan, treni ya TRC inabeba abiria elfu ishirini na TRC wanastahili kulipa shilingi laki mbili kwa mwezi. Iwe vivyo hivyo kwa mabasi na ndege.

Wakati wa fidia mwenye chombo atalipa nusu ya fidia na nusu iliyobaki italipwa na mfuko huu kwa fidia yoyote itakayoamuliwa. Kazi kwenu wawakilishi wa umma Dodoma kuchambua pendekezo hili.

Tume za maafa na faida zake
Vyombo vya habari ndani na nje za nchi inaelekea havioni umuhimu wa Tume zinazoanzishwa kuchunguza maafa kama haya ya juzi na jana. Yaani Merelani na Dodoma. Kwa upande mwingine, hata hivyo, kama Tume ya Ajali ya Treni Dodoma itashughulikia na masuala yatakayochangia pia kuubadili mfumo wa bima na fidia kama njia ya kudhibiti ajali zinazotokana na uzembe ingefaa iungwe mkono. Vinginevyo, fedha itakayoliwa na wajumbe hao wapewe wafiwa na mejeruhi.

Haki kulindwa na mahakama ya Afrika, Dunia?

Sio watu wengi wanaojua kuwa iwapo umefuata taratibu zote za mahakama katika nchi yako na hukuridhika na maamuzi ya mahakama basi unaweza kukata rufaa kwenye kamati maalum ya Umoja wa Afrika inayoshugulikia masuala ya haki za binadamu.

Kamati au tume hiyo hivi sasa iko mbioni kufanywa mahakama kama viongozi wa Afrika wataridhia suala hili kwenye mkutano wa kilele ujao kunako mwezi Juni.

Kwa mfano mjane anayeamini kuwa kanyimwa haki za kurithi mali aliyochuma na mumewe na akapeleka kesi mahakamani lakini ikatupwa nje; akakata rufaa mahakama kuu akashindwa; akakata rufaa tena mahakama ya rufaa na bado akashindwa bado atakuwa na nafasi kama hiyo tena kwenye mahakama hiyo ya Afrika.

Uanzishwaji wa Mahakama Kuu ya Afrika unakwenda sambamba na uanzishwaji wa mahakama ya Umoja wa Mataifa ambayo malengo yake bado yana shabaha ya kufanikisha vita vya haki ya binadamu duniani.

Kwa bahati mbaya sio wengi wanaojua juu ya kile kinachoendelea duniani katika ujenzi wa taasisi na taratibu zitakazohakikisha kuwa haki na usawa mbele ya vyombo vya sheria inakuwa ni ndoto ya kweli kwa kila mtu popote pale alipo duniani.

Hali ilivyo sasa ni kuwa anaweza kuibuka mtu mahala popote pale duniani na kwa kutumia nafasi yake ya uongozi; mipaka ya kile anachoita taifa lake huru; na kwa ushirikiano na wajanja wachache akafanya uhuni mkubwa katika nchi yake ikiwamo kudhulumu watu mali zao; kujitajirisha kwa wizi au rushwa; na hata kuiuza nchi yake na raia katika nchi yake na dunia nzima kwa ujumla isiwe na lolote la kufanya kumkomesha mtu huyo.

Isitoshe yapo matukio kadhaa katika nchi mbalimbali za Kiafrika hivi sasa kuonesha kuwa baadhi ya wale walioko madarakani wanadiriki kuficha au kufukia vitendo viovu, dhuluma, uonevu au vitendo vingine vya ukiukwaji wa haki za binadamu katika milki yao.

Kwa kuwa na Mahakama Kuu ya Afrika na Dunia na pengine mahakama za rufani katika ngazi hizo pia kutaimarisha uhuru wa mahakama za nchi moja moja na kuboresha haki na usawa kwa raia wa nchi husika.

Inavyoonekana ni kuwa dunia imeona udhaifu wa taasisi za kimataifa ambazo zinakosa meno ya kikatiba na kisheria.

Hali hii imesababisha kwa baadhi ya nchi mahakimu na majaji kuonekana wanawajibika kwa viongozi waliowateua na hivyo kuzifanya mahakama kutokuwa huru.

Ubinafsi pia umejitokeza katika vyombo vya sheria kufikia kiwango cha mwenye fedha kununua haki dhidi ya mnyonge anayestahili haki hiyo.

Maadili yameshuka katika baadhi ya nchi na rushwa sio kitu kigeni katika vyombo vingi vya sheria karibu katika kila nchi Afrika. Mahakama ya Afrika na dunia zitarudisha heshima ya mahakimu na majaji popote pale kwani wale wanaokiuka maadili wataadhiriwa na ngazi za juu.

Uzuri wa Mahakama ya Afrika ni kuwa itakuwa na majaji toka nchi mbalimbali za Kiafrika na pengine hata kutoka nje ya Afrika (kutegemeana na aina ya kesi na uzoefu wa majaji husika). Kitakachopambana katika duru hizi ni ubingwa wa kuitafsiri sheria kwa mujibu wa sheria na mikataba ya kimataifa kwa lengo la kuhakikisha Waafrika wote wanakuwa sawa mbele ya sheria hizo na mwenye haki ndiye anayestahili kunufaika na sio vinginevyo.


Haki za binadamu
Waafrika na wasio Waafrika kwa muda mrefu wamekuwa wakililaumu bara hili kwa kushindwa kuheshimu haki za binadamu.

Vyombo vya dola, yaani polisi, magereza na upelelezi aghalabu vinalaumiwa kwa kukiuka haki za binadamu.

Mathalani, hali ya magereza ya Afrika ukifananisha na yale ya Ulaya au Marekani ni ya kusikitisha na kutisha. Upo uwezekano mkubwa kuwa mahakama ya Afrika itashughulikia suala hili kikamilifu zaidi kuliko mahakama za nchi moja moja ambazo zinaelekea kuistahi au kuihurumia serikali ya nchi husika.

Wenye fedha au madaraka vijijini, kwenye kata, wilaya hadi ngazi za mikoa kwenye nchi mbalimbali wamekuwa wakikiuka haki za binadamu kwa kutumia nafasi zao kunyamazisha vitendo vyao ambavyo sasa vinaweza kumulikwa na kurunzi la mahakama ya Afrika na Dunia.

Demokrasia
Kwa kuwa kumekosekana chombo sahihi cha kushughulikia kutafsiri sheria na katiba katika nchi zetu hivi sasa viongozi walioko madarakani wamepora jukumu hilo na kuanza kutafsiri sheria hizo kwa mujibu wa uelewa wao na kile wanachokiamini wao kuwa ndio haki.

Mahakama Kuu ya Afrika itachangia sio kwa kiasi kidogo kutafsiri demokrasia na nafasi yake katika sheria na katiba mbalimbali za nchi zetu.

Kwa mantiki hii hapatakuwa na seti kadhaa za tafsiri kutegemeana na wale walioko madarakani na kile wanachokitaka wao.

Fujo na matatizo mengine yanayosababishwa na ukiukwaji wa misingi ya demokrasi sasa vinaweza kupata ufumbuzi wa kudumu kwa kuwa na Mahakama ya Afrika na Dunia na jopo la majaji kushughulikia kesi za demokrasia na uchaguzi.

Uwazi na rushwa
Mikataba mingi ya kibiashara ndani na nje ya nchi mbalimbali za Kiafrika inaghubikwa na giza la usiri na kinachofanyika huku kinajulikana na M…. na wahusika.

Mahakama ya Afrika na dunia itamulika masuala yote ambayo ni vivutio dhahiri vya rushwa kama vinafanyika bila uwazi.

Suala la uwazi limekuwa gumu sana kwa viongozi wa Afrika hasa pale maslahi binafsi na yale ya kutaka kuhakikisha chama tawala kinabakia madarakani baada ya kipindi cha utawala wake kwisha. Fedha inahitajika na kiongozi mwenyewe ili aweze kuwa na maisha mazuri baada ya kuondoka madarakani lakini vile vile fedha inahitajika ili kuhakikisha chama kinabakia tena madarakani kipindi kijacho.

Uwazi unakuwa kikwazo mbele ya masaula hayo hapo juu. Na kiongozi hata awe na nia nzuri namna gani kitendo cha kuleta uwazi katika uongozi wake anajikuta katika matatizo makubwa ndani ya chama chake na katika serikali yake.

Hata iundwe tume gani ikifikia kwenye hatua ya uwazi mwanga wa tume hiyo hufifia na kisha kufa kabisa.

Hatuwezi kutegemea viongozi wetu wajikosoe wenyewe; haiwezekani viongozi wetu kujitathmini wao wenywe; na haiwezekani viongozi wetu kujiadhibu wao wenyewe. Ni kwa mantiki hii taasisi ya kimataifa yenye uwezo wa kuwawajibisha hata viongozi au hata kuonesha tu kuwa wana makosa au aibu wanazoficha itasaidia kuongeza hadhi ya utawala katika Afrika.

Utawala bora
Utawala bora hauwezi kuja Afrika bila kuwa na chombo cha juu kinachoweza kukosoa taasisi zetu za ndani.

Mazoea, kutokujua na ukomo wa uwezo wa watendaji katika ngazi mbalimbali siku zote vitachangia kuwa na serikali dhaifu zisizowajibika kwa wananchi.

Hali ilivyo sasa karibu Afrika yote ni ile inayoonesha kuwa watawala ni mabwana na wananchi ni watwana.

Hali hii haiwezi kuruhusiwa kuendelea kama kweli tunataka kuwakomboa watu wetu kijamii, kiuchumi na kimawazo.

Ni pale tu wananchi wetu watakapokuwa na kauli na uwezo wa kuwawajibisha viongozi wao ndio maendeleo ya kweli yataanza kuonekana Afrika.

Mahakama Kuu ya Afrika itaweza pia kuchangia kwa kiasi kikubwa katika kuleta utawala bora Afrika kwa kusikiliza kilio cha wale wanaoamini kuwa kijiji, mji, wilaya au mkoa au nchi yao haifuati utawala wa sheria wala katiba iliyopo haikidhi haki za chini na za juu za wananchi katika nchi husika.

Msingi wa UA
Mahakama ya Afrika itakuwa jiwe la msingi la Umoja wa Afrika. Misingi mingine ni pamoja na haki ya wananchi kusafiri, kuishi na kufanya kazi popote Afrika; jeshi moja la Afrika; bunge la Afrika ambavyo ni vitu pekee vitakavyoweza kufanikisha kuwa na serikali moja ya Afrika.

Yapo mambo mengine muhimu ya kuzingatiwa na hasa unapoelewa kuwa nchi za Kiafrika hazifanani na kila moja ina historia yake na matatizo yake kutokana na sababu za kisiasa, kijamii na mazingira.

Hata hivyo, misingi hiyo hapo juu inaweza kuwa mwanzo wa kufanikisha kuondoa matatizo ya kila nchi kwani utawala wa sheria na taratibu zinazokubalika zina nguvu na uwezo wa kurahisisha maazimio na mipango mingine kwa kila nchi.

Taasisi zingine ziige mfano
Umoja wa Afrika utaendelea kuwa ndoto kama Waafrika watategemea viongozi wao tu ndio watakaoufanikisha.

Kinachotakiwa hivi sasa ni kwa makundi mbalimbali hapa Afrika kama vile waandishi wa habari, walimu, madaktari, manesi, watumishi wa serikali, maprofesa, wahandisi, wahasibu, vijana, wazee, wanawake na kadhalika kuunda taasisi zao chini ya Umoja wa Afrika na kuanza kuandaa ajenda mbalimbali zitakazoongoza Afrika kule wao na wenzao wote wanakotaka iende.

Heshima na usawa
Umoja na maendeleo ya Afrika lazima ujengwe katika misingi ya usawa na heshima kwa wote.

Bila shaka mahakama ya Afrika itatoa msukumo unaotakiwa katika kuhakikisha kuwa kila nchi inazingatia kuwepo sio tu kwa haki bali usawa na heshima kwa kila mwananchi kama nguzo za kusimamisha mkusanyiko wa watu mkubwa kuliko ule wa utaifa mmoja mmoja kwa nchi mbalimbali za Kiafrika.

Afrika ina nafasi chungu nzima za kujifunza kutoka mabara mengine jinsi ya kufanikisha kuwepo kwa umoja wa Afrika utakaochangia tu sio kuondoa umaskini bali pia kujenga mkusanyiko wa watu utakaopewa usawa na heshima toka popote pale duniani.

Itakuwa ni kitendo cha faraja kama viongozi wetu wataunga mkono kwa hali na mali mpango wa uanzishaji wa mahakama kamili ya Afrika na ile ya dunia.

Haki kulindwa na mahakama ya Afrika, Dunia?

Sio watu wengi wanaojua kuwa iwapo umefuata taratibu zote za mahakama katika nchi yako na hukuridhika na maamuzi ya mahakama basi unaweza kukata rufaa kwenye kamati maalum ya Umoja wa Afrika inayoshugulikia masuala ya haki za binadamu.

Kamati au tume hiyo hivi sasa iko mbioni kufanywa mahakama kama viongozi wa Afrika wataridhia suala hili kwenye mkutano wa kilele ujao kunako mwezi Juni.

Kwa mfano mjane anayeamini kuwa kanyimwa haki za kurithi mali aliyochuma na mumewe na akapeleka kesi mahakamani lakini ikatupwa nje; akakata rufaa mahakama kuu akashindwa; akakata rufaa tena mahakama ya rufaa na bado akashindwa bado atakuwa na nafasi kama hiyo tena kwenye mahakama hiyo ya Afrika.

Uanzishwaji wa Mahakama Kuu ya Afrika unakwenda sambamba na uanzishwaji wa mahakama ya Umoja wa Mataifa ambayo malengo yake bado yana shabaha ya kufanikisha vita vya haki ya binadamu duniani.

Kwa bahati mbaya sio wengi wanaojua juu ya kile kinachoendelea duniani katika ujenzi wa taasisi na taratibu zitakazohakikisha kuwa haki na usawa mbele ya vyombo vya sheria inakuwa ni ndoto ya kweli kwa kila mtu popote pale alipo duniani.

Hali ilivyo sasa ni kuwa anaweza kuibuka mtu mahala popote pale duniani na kwa kutumia nafasi yake ya uongozi; mipaka ya kile anachoita taifa lake huru; na kwa ushirikiano na wajanja wachache akafanya uhuni mkubwa katika nchi yake ikiwamo kudhulumu watu mali zao; kujitajirisha kwa wizi au rushwa; na hata kuiuza nchi yake na raia katika nchi yake na dunia nzima kwa ujumla isiwe na lolote la kufanya kumkomesha mtu huyo.

Isitoshe yapo matukio kadhaa katika nchi mbalimbali za Kiafrika hivi sasa kuonesha kuwa baadhi ya wale walioko madarakani wanadiriki kuficha au kufukia vitendo viovu, dhuluma, uonevu au vitendo vingine vya ukiukwaji wa haki za binadamu katika milki yao.

Kwa kuwa na Mahakama Kuu ya Afrika na Dunia na pengine mahakama za rufani katika ngazi hizo pia kutaimarisha uhuru wa mahakama za nchi moja moja na kuboresha haki na usawa kwa raia wa nchi husika.

Inavyoonekana ni kuwa dunia imeona udhaifu wa taasisi za kimataifa ambazo zinakosa meno ya kikatiba na kisheria.

Hali hii imesababisha kwa baadhi ya nchi mahakimu na majaji kuonekana wanawajibika kwa viongozi waliowateua na hivyo kuzifanya mahakama kutokuwa huru.

Ubinafsi pia umejitokeza katika vyombo vya sheria kufikia kiwango cha mwenye fedha kununua haki dhidi ya mnyonge anayestahili haki hiyo.

Maadili yameshuka katika baadhi ya nchi na rushwa sio kitu kigeni katika vyombo vingi vya sheria karibu katika kila nchi Afrika. Mahakama ya Afrika na dunia zitarudisha heshima ya mahakimu na majaji popote pale kwani wale wanaokiuka maadili wataadhiriwa na ngazi za juu.

Uzuri wa Mahakama ya Afrika ni kuwa itakuwa na majaji toka nchi mbalimbali za Kiafrika na pengine hata kutoka nje ya Afrika (kutegemeana na aina ya kesi na uzoefu wa majaji husika). Kitakachopambana katika duru hizi ni ubingwa wa kuitafsiri sheria kwa mujibu wa sheria na mikataba ya kimataifa kwa lengo la kuhakikisha Waafrika wote wanakuwa sawa mbele ya sheria hizo na mwenye haki ndiye anayestahili kunufaika na sio vinginevyo.


Haki za binadamu
Waafrika na wasio Waafrika kwa muda mrefu wamekuwa wakililaumu bara hili kwa kushindwa kuheshimu haki za binadamu.

Vyombo vya dola, yaani polisi, magereza na upelelezi aghalabu vinalaumiwa kwa kukiuka haki za binadamu.

Mathalani, hali ya magereza ya Afrika ukifananisha na yale ya Ulaya au Marekani ni ya kusikitisha na kutisha. Upo uwezekano mkubwa kuwa mahakama ya Afrika itashughulikia suala hili kikamilifu zaidi kuliko mahakama za nchi moja moja ambazo zinaelekea kuistahi au kuihurumia serikali ya nchi husika.

Wenye fedha au madaraka vijijini, kwenye kata, wilaya hadi ngazi za mikoa kwenye nchi mbalimbali wamekuwa wakikiuka haki za binadamu kwa kutumia nafasi zao kunyamazisha vitendo vyao ambavyo sasa vinaweza kumulikwa na kurunzi la mahakama ya Afrika na Dunia.

Demokrasia
Kwa kuwa kumekosekana chombo sahihi cha kushughulikia kutafsiri sheria na katiba katika nchi zetu hivi sasa viongozi walioko madarakani wamepora jukumu hilo na kuanza kutafsiri sheria hizo kwa mujibu wa uelewa wao na kile wanachokiamini wao kuwa ndio haki.

Mahakama Kuu ya Afrika itachangia sio kwa kiasi kidogo kutafsiri demokrasia na nafasi yake katika sheria na katiba mbalimbali za nchi zetu.

Kwa mantiki hii hapatakuwa na seti kadhaa za tafsiri kutegemeana na wale walioko madarakani na kile wanachokitaka wao.

Fujo na matatizo mengine yanayosababishwa na ukiukwaji wa misingi ya demokrasi sasa vinaweza kupata ufumbuzi wa kudumu kwa kuwa na Mahakama ya Afrika na Dunia na jopo la majaji kushughulikia kesi za demokrasia na uchaguzi.

Uwazi na rushwa
Mikataba mingi ya kibiashara ndani na nje ya nchi mbalimbali za Kiafrika inaghubikwa na giza la usiri na kinachofanyika huku kinajulikana na M…. na wahusika.

Mahakama ya Afrika na dunia itamulika masuala yote ambayo ni vivutio dhahiri vya rushwa kama vinafanyika bila uwazi.

Suala la uwazi limekuwa gumu sana kwa viongozi wa Afrika hasa pale maslahi binafsi na yale ya kutaka kuhakikisha chama tawala kinabakia madarakani baada ya kipindi cha utawala wake kwisha. Fedha inahitajika na kiongozi mwenyewe ili aweze kuwa na maisha mazuri baada ya kuondoka madarakani lakini vile vile fedha inahitajika ili kuhakikisha chama kinabakia tena madarakani kipindi kijacho.

Uwazi unakuwa kikwazo mbele ya masaula hayo hapo juu. Na kiongozi hata awe na nia nzuri namna gani kitendo cha kuleta uwazi katika uongozi wake anajikuta katika matatizo makubwa ndani ya chama chake na katika serikali yake.

Hata iundwe tume gani ikifikia kwenye hatua ya uwazi mwanga wa tume hiyo hufifia na kisha kufa kabisa.

Hatuwezi kutegemea viongozi wetu wajikosoe wenyewe; haiwezekani viongozi wetu kujitathmini wao wenywe; na haiwezekani viongozi wetu kujiadhibu wao wenyewe. Ni kwa mantiki hii taasisi ya kimataifa yenye uwezo wa kuwawajibisha hata viongozi au hata kuonesha tu kuwa wana makosa au aibu wanazoficha itasaidia kuongeza hadhi ya utawala katika Afrika.

Utawala bora
Utawala bora hauwezi kuja Afrika bila kuwa na chombo cha juu kinachoweza kukosoa taasisi zetu za ndani.

Mazoea, kutokujua na ukomo wa uwezo wa watendaji katika ngazi mbalimbali siku zote vitachangia kuwa na serikali dhaifu zisizowajibika kwa wananchi.

Hali ilivyo sasa karibu Afrika yote ni ile inayoonesha kuwa watawala ni mabwana na wananchi ni watwana.

Hali hii haiwezi kuruhusiwa kuendelea kama kweli tunataka kuwakomboa watu wetu kijamii, kiuchumi na kimawazo.

Ni pale tu wananchi wetu watakapokuwa na kauli na uwezo wa kuwawajibisha viongozi wao ndio maendeleo ya kweli yataanza kuonekana Afrika.

Mahakama Kuu ya Afrika itaweza pia kuchangia kwa kiasi kikubwa katika kuleta utawala bora Afrika kwa kusikiliza kilio cha wale wanaoamini kuwa kijiji, mji, wilaya au mkoa au nchi yao haifuati utawala wa sheria wala katiba iliyopo haikidhi haki za chini na za juu za wananchi katika nchi husika.

Msingi wa UA
Mahakama ya Afrika itakuwa jiwe la msingi la Umoja wa Afrika. Misingi mingine ni pamoja na haki ya wananchi kusafiri, kuishi na kufanya kazi popote Afrika; jeshi moja la Afrika; bunge la Afrika ambavyo ni vitu pekee vitakavyoweza kufanikisha kuwa na serikali moja ya Afrika.

Yapo mambo mengine muhimu ya kuzingatiwa na hasa unapoelewa kuwa nchi za Kiafrika hazifanani na kila moja ina historia yake na matatizo yake kutokana na sababu za kisiasa, kijamii na mazingira.

Hata hivyo, misingi hiyo hapo juu inaweza kuwa mwanzo wa kufanikisha kuondoa matatizo ya kila nchi kwani utawala wa sheria na taratibu zinazokubalika zina nguvu na uwezo wa kurahisisha maazimio na mipango mingine kwa kila nchi.

Taasisi zingine ziige mfano
Umoja wa Afrika utaendelea kuwa ndoto kama Waafrika watategemea viongozi wao tu ndio watakaoufanikisha.

Kinachotakiwa hivi sasa ni kwa makundi mbalimbali hapa Afrika kama vile waandishi wa habari, walimu, madaktari, manesi, watumishi wa serikali, maprofesa, wahandisi, wahasibu, vijana, wazee, wanawake na kadhalika kuunda taasisi zao chini ya Umoja wa Afrika na kuanza kuandaa ajenda mbalimbali zitakazoongoza Afrika kule wao na wenzao wote wanakotaka iende.

Heshima na usawa
Umoja na maendeleo ya Afrika lazima ujengwe katika misingi ya usawa na heshima kwa wote.

Bila shaka mahakama ya Afrika itatoa msukumo unaotakiwa katika kuhakikisha kuwa kila nchi inazingatia kuwepo sio tu kwa haki bali usawa na heshima kwa kila mwananchi kama nguzo za kusimamisha mkusanyiko wa watu mkubwa kuliko ule wa utaifa mmoja mmoja kwa nchi mbalimbali za Kiafrika.

Afrika ina nafasi chungu nzima za kujifunza kutoka mabara mengine jinsi ya kufanikisha kuwepo kwa umoja wa Afrika utakaochangia tu sio kuondoa umaskini bali pia kujenga mkusanyiko wa watu utakaopewa usawa na heshima toka popote pale duniani.

Itakuwa ni kitendo cha faraja kama viongozi wetu wataunga mkono kwa hali na mali mpango wa uanzishaji wa mahakama kamili ya Afrika na ile ya dunia.

Matumizi duni ya Tovuti yanadumaza uchumi

Katika siku za hivi karibuni nimekuwa nikipata barua-pepe nyingi za watu wa nje wanaotaka kuja kutalii, kuwekeza au kufanya biashara na Tanzania.

Baadhi ya watu hao wala sio wageni ni Watanzania waliokaa nje muda mrefu au ambao wamechukua uraia wa nchi nyingine lakini hivi sasa wanataka kurejea baada ya kuvutiwa na mageuzi ya uchumi yanayoendelea nchini.

Baadhi ya maswali yao yamekuwa magumu kwangu kujibu na nikayaelekeza au nikawaelekeza wahusika kwa taasisi kama vile Wizara ya Mambo ya Nje, TCCIA, taasisi zinazohusika na utalii, Tanzania Investment Center na kadhalika.

Majibu ambayo watu waliowasiliana nami wananipa ni kuwa ama e-mail za wahusika hazifanyi kazi, nyingine zina virusi, na kwa kila hali hakuna anayewajibu wala kushughulikia shida zao.

Kwa mfano, kuna makampuni ya utalii nchini Venezuela na Brazil yaliyokuwa na watu wanaotaka kuja kutalii Tanzania. Hadi leo wanahaha kupata visa za kuja Tanzania.
Ubalozi wa karibu (naomba kusahihishwa) nadhani ni Washington lakini japo ubalozi huo una web-site na email wakala hao wanasema hakuna jibu walilolipata.

Anwani ya websaiti ya ubalozi huo ni http://www.tanzaniaembassy-us.org na kama sikosei email yao ni: balozi@tanzaniaembassy-us.org Wabrazili na Wavenezuela wanasema ni anwani bubu.

Katika websaiti hiyo pamoja na mambo mengine kuna nembo ya taifa, bendera inayopepea lakini inaelekea anwani ya barua pepe yao haipepei na kuna twiga anayekimbia na maneno -TANZANIA ON THE GO- lakini inaelekea kwa hakika sivyo bado Tanzania imelala katika kutumia mtandao ili kukuza uchumi wake kutokana na biashara nyingi ambazo hivi leo zinafanyika kwa kutumia email na internet.

Kuna bwana yuko Uarabuni anataka kuanza biashara ya kununua na kuuza mifugo na Tanzania. Inaelekea huyu kazaliwa hapa maana anazungumza Kiswahili fasaha. Nimejaribu kumuelekeza kwa wahusika lakini anasema hapati majibu anaomba mimi nimsaidie. Lakini ninadhani kuna walioajiriwa kufanya kazi hiyo au sio-pengine Wizara inayohusika inaweza kumsaidia kwa kuwasiliana nami.

Leo ninapoandika makala hii nina barua pepe zaidi ya kumi. Baadhi yake zinataka kununua korosho kutoka Tanzania; Huyu mwingine anataka kujua kama Bombay Bazar na Manek Traders ni kampuni halali na wanaweza kufanya biashara nazo; kuna kijana wa Kimarekani anasema mkimbiaji mbio aliyewika miaka kama 20 iliyopita hivi ni baba yake na anataka kuwasiliana naye (sijui kama ni kweli au uongo), hata hivyo mwanariadha aliyesoma Marekani na anajua ana mtoto huko awasiliane nami nimuunganishe na mwanae; kuna wanaotaka madini; kuna wanaotaka kuuza nguo ili mradi kuna fursa mbalimbali kwa Watanzania na taifa kuongeza kipato chake.

Labda hapa tuwaambie Watanzania wanaotaka biashara hizo au ambao wametajwa hapo juu wawasiliane nami kupitia anwani yangu ya sammy.makilla@columnist.com niwaunganishe na wahusika bila malipo yoyote.

Kwanini email & internet hazitumiki
Hali hii, hata hivyo, imenifanya nijiulize hivi kweli serikali, taasisi mbalimbali na makampuni yaliyoko kwenye mtandao yanautumia kikamilifu ili kuikwamua nchi kutokana na umaskini?

Kuna wizara ambazo katika miaka hii ya sayansi na teknolojia zinatakiwa kuwa na websaiti na watu wanaofuatilia email kwa saa ishirini na nne.

Tanzania haiko tena kwenye miaka ya kulala masaa 16 kila siku jamani. Hivi kweli tutaendelea kama zaidi ya asilimia 60 ya maisha yetu hapa duniani ni ya usingizini au kwenye anasa nyingine?

Kwa mfano websaiti ya Wizara ya Nje ya Afrika ya Kusini inayoitwa Department of Foreign Affairs inayopatikana kwenye http://www.dfa.gov.za Inafanya kazi masaa ishirini na nne.

Ukituma email wakati wowote unajibiwa katika muda usiozidi saa moja. Mnaona hayo na sisi bado tumelala.

Hao wawekezaji watatoka wapi kama wakituma email hakuna anayewajibu? Taasisi zinazohusika na biashara na huduma mbalimbali na hasa kama vile bodi ya utalii, makampuni ya utalii, mahoteli, vyombo vya usafiri na kadhalika navyo kwa namna moja au nyingine lazima ziwe na mtandao hai na unaofanya kazi ikiwezekana kwa saa ishirini na nne.

Dunia ilivyo ni kuwa Tanzania ikiwa ni usiku Marekani na Japani ni asubuhi au mchana.
Bado hatujaamka na kujua ukweli huu? Tusifikiri sisi tunapolala basi watu wote duniani wamelala. Wengine ndio kwanza wanakunywa chai, wengine wamo kwenye lanchi na wengine ndio kazi zimeanza tena.

Makala hii inakusudia kutoa wito kwa Watanzania kuamka na kuanza kuchangamkia matumizi ya email na internet kwa ukamilifu kwa sababu hii sasa ndio njia muhimu ya mawasiliano ya kibiashara pengine kuliko njia nyingine yoyote duniani.

Haifai kuwa na websaiti za mapambo. Websaiti lazima ziwe ni viungo hai vinavyoiunganisha nchi na watu wengine duniani ili biashara au shughuli fulani ifanyike kwa haraka na kwa ufanisi mkubwa zaidi.

Ni tatizo gani linakwamisha…
Wanaojua ni nini kinachokwamisha kwa mfano wizara muhimu kuwa na websaiti na webmasta na wasaidizi wake wanaofanya kazi kwa kupokezana kwa masaa ishirini na nne kila siku ni wizara zinazohusika.

Sababu zinaweza kuwa za kifedha, nguvu kazi, gharama za kuweka kiunganisho cha internet na kadhalika.

Lakini kama haya ni matatizo kwanini tusiyaongelee? Kwanini serikali isivutwe sikio na kuambiwa kuwa kuna tatizo kama hili? Lakini matatizo yote haya kwa upande wangu ninaona ni matatizo ya mficha maradhi tu.

Tatizo la fedha kwa mfano linaweza likawa la urongo na kweli. Maana nina hakika katika nchi nyingi kampuni zinazotoa huduma za mtandao ziko tayari kusaidia serikali na taasisi zote zile zinazotaka kukuza uchumi wa nchi tena wakati mwingine bure. Lakini watu hao wasipofuatwa wakaelezwa shida hii hakuna atakayejua kuwa tatizo ndio hilo la kifedha.

Kuhusu utaalamu hapa serikali lazima ielezwe ukweli kuwa inapaswa kutoa mchango mkubwa ili Tanzania iwe na wataalamu wa kompyuta na shughuli zinazoendana na teknolojia hii.

Na uzuri wa kuwekeza katika sekta hii ni kuwa wataalam wa mambo haya wana soko kubwa karibu kila sehemu duniani.

Nina hakika nchi ikiwa na nia tunaweza kutoa wataalamu wa kujitosheleza na ziada ambao watatuingizia fedha za kigeni kwa kwenda kufanya kazi nchi za nje. Hao wanaobaki nyumbani watatusaidia kuifanya Tanzania kuwa namba wani kikweli kweli katika teknolojia hii muhimu katika enzi za utandawazi na ushindani mkubwa wa kiuchumi.

Serikali inastahili pongezi kwa kurahisisha upatikanaji wa vifaa vya teknolojia hii kwa bei nafuu sana ukilinganisha na sehemu nyingine Afrika. Na hili ni muhimu liendelee ili kompyuta Tanzania zifike hadi vijijini. Kama wananchi wa Ruvuma vijijini wanaweza kufanya biashara na nchi za nje kupitia mtandao, kwanini vijiji vingine navyo visifanye hivyo?

Gharama za kuunganisha
Baadhi ya wizara na taasisi mbalimbali ninaamini zilianza vibaya kwa kutumia internet ya kupitia kwenye laini za simu.

Njia hii ni ghali sana. Njia bora zaidi ni kutumia kitu kinachoitwa ‘wireless’ au kuunganishwa na mtoa huduma bila haja ya kuwepo kwa simu.

Kwa hakika gharama za mwanzo za uunganishaji ni kubwa lakini baada ya hapo internet inakuwa kama ni bure. Wizara na taasisi zote zinazostahili kuwa na mtandao lazima zitumie wireless na sio vinginevyo.

Gharama hivi sasa zinafikia milioni tatu hivi kuunganishwa. Kwanini serikali na taasisi zinazohusika zisikae chini na kuona ni jinsi gani gharama hizi zinaweza kupunguzwa. Nina hakika gharama zikifika milioni moja sio tu makampuni bali hata watu binafsi wataweza kuwa na huduma hii muhimu katika miaka ya hivi sasa.

Kingine kilichobaki na ambacho nacho kina umuhimu sawa ni hili la kuona kuwa tunakuwa na wataalamu na mafundi wengi kadri iwezekanavyo katika nyanja za kompyuta na internet.

Na hapa serikali na wabia wengine washirikiane ili Tanzania iwe ni mfano wa kuigwa Afrika baada ya Afrika Kusini katika mambo ya internet na matumizi ya kompyuta kwa ujumla.

Tutawashingilia wengine hadi lini?

Watanzania ni Waafrika na wiki hii wana kila sababu ya kuishangilia timu pekee ya Afrika iliyobaki katika kinyang’anyiro cha Kombe la Dunia huko Japan na Korea mwaka huu wa 2002.

Kwa kuwa Tanzania na Afrika Mashariki kwa ujumla hazikufuzu basi wawakilishi wetu sasa ni timu ya Taifa ya Senegal, nchi iliyoko huko Afrika Magharibi.

Historia ya Kombe la Dunia inaonesha Afrika Mashariki haijawahi kutoa timu yenye kiwango cha mpira wa Kombe la Dunia. Ni Afrika Kaskazini, Afrika Magharibi na Afrika ya Kati tu zinazochukua nafasi hizo mwaka nenda, mwaka rudi.

Swali hapa ni je, tutaendelea kuwashangilia wenzetu hawa mpaka lini? Nchi za Afrika Mashariki kila moja peke yake na zote kwa umoja wao haziwezi kuweka mkakati wa kuhakikisha zinasaidiana kuwa angalau na timu moja ya nchi hizi (pamoja na Rwanda na Burundi) kwenda Kombe la Dunia?

Njia ya mkato kwenda Kombe la Dunia
Njia ya mkato kwenda Kombe la Dunia ni kuhakikisha kuwa bara la Afrika na nchi ya Marekani (USA) zinagawanya katika sehemu tano tano (kutokana na nchi/majimbo yao).

Kila moja itoe timu 5 za Taifa (ili kuhakikisha uwakilishi unaoenda kwa uwiano wa idadi ya watu na nchi/majimbo). Afrika iwakilishwe na timu 10 kwa utaratibu wa Afrika Magharibi-timu 3; Afrika Kaskazini-timu 2; Afrika ya Kati –timu 2; Visiwa vya Afrika-timu 1; Afrika Mashariki-timu 1 na Afrika Kusini-timu 1.

Hili litakuwa ni jibu zuri kwa Ulaya ambayo inatoa timu nyingi zaidi kuliko wingi wa watu na ukubwa wa eneo hilo la dunia.

Marekani (USA) kwa kuwa ndiyo imeanza kuchangamkia mpira wa miguu itoe timu tano-kila moja toka Kaskazini, Kusini, Kati, Magharibi na Mashariki. Kwa kufanya hivi FIFA itachangia kasi ya kukubalika kwa soka huko Marekani na hivyo kuongeza utamu na sifa ya mchezo huu kuwa namba moja duniani.

Lakini kama nilivyosema hii ndio njia ya mkato kwenda Kombe la Dunia. Kwa bahati mbaya FIFA inaweza ikachukua miaka 10 kufanya mabadiliko kama haya. Je, tusubiri hadi mteremko au tuwe ngangari na kupambana na hali halisi ya sasa ili tutoe timu ya hadhi ya kimataifa?

Uongozi na maendeleo
Tupende tusipende, michezo kwa kiasi fulani inategemea ari ya kiongozi aliyeko kwenye kigoda. Tazama mashirika au taasisi nyingi ambazo zimewahi kutoa timu bora utakuta kiongozi wa juu mahala pale alikuwa mwanamichezo namba moja yeye mwenyewe au shabiki wa kutupwa wa timu yake ya michezo.

Kwa taifa pia hali si tofauti. Kama kiongozi wa nchi anajali, anathamini na anachangia kuendeleza michezo, vijana wake wanaweza kufanya maajabu katika viwanja vya michezo mahala popote pale duniani.

Wala tusiende mbali. Tazama China ya Mao Dze Dung; Ujerumani Mashariki ya wakati ule; na Cuba ya Castro. Karibu na nyumbani Nelson Mandela kama shabiki wa mpira, ngumi na michezo mingine amechangia sio haba kuwafanya vijana wa Afrika Kusini kuwika kimichezo haraka kuliko ilivyotarajiwa.

Ni dhahiri kuwa pamoja na kazi nzuri inayofanywa na uongozi wa nchi kutilia mkazo michezo majukwaani au bungeni bado kuna kazi kubwa ya wao kuonekana wanaichukulia michezo sio kama michezo (kitu cha bure na kisicho na maana) bali kama kazi au ajira ya uhakika kwa maelfu ya vijana ambao kwa namna nyingine yoyote hawatobahatika kuajiriwa.

Na ajira, mathalani, katika mpira wa miguu ikiwa ni nje ya nchi inalipa mara kadhaa ukilinganisha na kazi zenye vyeo vya juu hapa nchini.

Wizara inayohusika na michezo ina kazi kubwa ya kuhakikisha kuwa tunaondoa uswahili na ushambenga katika vilabu na vyama vya michezo. Ni lazima viongozi wa vilabu na vyama wawe sio tu ni wanamichezo bali wana taaluma ya menejimenti na uongozi bora ili waweze kuendeleza nchi kimichezo. Huu si wakati wa kuvumilia viongozi wababaishaji, mbumbumbu na wasiojua dunia inakwenda wapi kimichezo.

Uhasibu na Ukaguzi
Viongozi wababaishaji hugeuza vilabu na vyama vya michezo kama mahala pa kutafuna fedha ya wajinga au mali isiyo na mwenyewe. Wakati umefika sasa wa kulazimisha kila klabu na kila chama cha michezo sio tu kuwa na mhasibu wa kutengeneza mahesabu yake lakini pia wakaguzi wa ndani na wa nje kukagua mahesabu hayo kwa vipindi maalum vitakavyowekwa.

Binadamu hakamiliki ila….
Michezo ni sehemu ya utu wetu. Kitendo chochote kinachomnyang’anya Mtanzania michezo ni kitendo cha kupunguza utu na heshima ya Mtanzania.

Na katika miaka ya leo ambapo michezo hutoa ajira maridhawa kuliko tarafu za aina nyingine ni kumpora mtu pia mkate wake wa kila siku na fursa yake ya kuukata kutokana na michezo.

Kama walipa kodi Watanzania wote kwa umoja wao wana haki ya kudai mitaa, vijiji, kata, tarafa, wilaya na mikoa yao kuwapa viwanja vya michezo.

Hivi sasa kumejitokeza tabia potofu ya viongozi mbalimbali kuona, mathalani, kuwa na majengo ya shule tu ni bora kuliko kuwa na viwanja vizuri na michezo kwa watoto wetu.

Na katika shule hizo ni asilimia ndogo tu itakayopata ajira maofisini au katika makampuni mbalimbali nchini. Laiti kungelikuwa na viwanja vya kutosha vya michezo basi wanafunzi wengi zaidi wangelipatiwa fursa ya kujiajiri wenyewe kama wachezaji soka, tenisi, masumbwi, riadha na kadhalika.

Kwa maneno mengine, viongozi wetu bado hawajatambua umuhimu wa michezo kiuchumi na kijamii na bado wanang’ng’ania kutaka kuiendesha michezo kama sehemu ya siasa.

Michezo kama siasa huendeshwa kwa lengo la kuwapatia viongozi sifa. Michezo kama shughuli ya kiuchumi na kijamii huendelezwa ili kuwapatia vijana ajira inayowawezesha kukimu maisha yao na pia kuwanyanyua kimaisha wazazi na jamaa zao.
Haimsaidii kiongozi yeyote wala taifa kupuuza maendeleo ya kimichezo ya kijana yeyote hata kama sio ndugu yake. Kwa yakini kitu kama hicho hulipunguzia taifa nafasi ya kuingiza mapato dhahiri toka nje.

Ili tunyanyue michezo
Kwangu binafsi ni kosa kuwanyima watoto wa chekechea na shule za msingi nafasi ya kucheza na kukua kutokana na michezo.

Wanasaikolojia wanashauri kwa usahihi kabisa kuwa asilimia kubwa ya muda katika chekechea utumike katika michezo ili kuwa na makuzi yanayowiana kati ya mwili na akili; katika shule za msingi muda wa kusoma na michezo uwe ni hamsini kwa hamsini; katika sekondari na vyuo vya juu iwe ni asilimia 75 (masomo) kwa 25 (michezo). Uwiano huu unafaa kufuatwa pia hata baada ya kumaliza chuo kama mtu anataka aepuke magonjwa mbalimbali yanayosababishwa na kukosa mazoezi ya kutosha (ikiwemo shinikizo la damu, vitambi kwa polisi na viongozi wa michezo).

Kuwekeza katika michezo
Michezo ni kwa ajili ya wote. Kama hivyo ndivyo hii ina maana michezo ni sawa na usalama na ulinzi (kulinda afya za Watanzania na pengine maadili mema); michezo ni sawa na huduma ya afya (kila mtu ahudumiwe); na michezo ni nishati muhimu kuijenga rasilimali muhimu kuliko zote katika taifa-watu.

Kama ndivyo pamoja na watu wenyewe, serikali kuu na serikali za mitaa lazima ziwekeze katika miundo-mbinu ya michezo.

Ianzishwe kampeni ya kuijenga Tanzania upya kimichezo na katika kampeni hiyo kila mtaa, kijiji, kata, tarafa lazima iwe na viwanja vya michezo ya aina zote. Na miongozo na taratibu ziwepo za kuviendesha ili kufikia malengo ya kutoa wanamichezo bora baadaye.

Timu kwa daraja mbalimbali
Pendekezo linaloweza kwenda mbali katika kuendeleza soka na michezo mingine hapa nchini ni kuhakikisha kuwa panakuwa na timu za mtaa, kata, tarafa, wilaya, mikoa na taifa kwa kila mchezo.

Njia zitafutwe kuhakikisha kuwa michezo inakuwa ni sehemu ya kazi/masomo na panakuwa na mashindano wakati wote ili kuhakikisha nchi hii ina wanamichezo walioko kwenye fomu wakati wowote.

Ni muhimu kwa hivyo mitaa, kata, vijiji, tarafa, wilaya, mkoa na taifa kuwa na bajeti za wazi zinazoonesha mapato na matumizi katika michezo mbalimbali. Japan na Korea kama wenyeji wa Kombe la Dunia wamepata faida kadhaa mojawapo ni ile ya kiuchumi au kibiashara. Vijiji, miji, wilaya, mikoa na nchi inatakiwa kuiga mfano huu na kuutumia kujineemesha kwa namna moja au nyingine.

Aidha lazima tuwe na makocha au walimu wa kimataifa na tusijidanganye na watu wasiofuzu au kuwa na uzoefu wa kusimamia timu za kitaifa. Hii si gharama kubwa kama tunaweza kuwalipa mameneja wa kampuni moja tu mamilioni, kwanini tushindwe kwa kocha wa taifa zima? Tena wakati FIFA inamwaga mapesa Afrika.

Kwa kumalizia nirudie tu kuwa kama Tanzania haitajizatiti kwa namna hiyo hapo juu kimichezo basi kuna hatari ya nchi hii kuwa Dunia ya Tatu kama sio ya nne kimichezo katika bara hili hili la Afrika wakati nchi kama Senegal, Cameroun na Bourkina Fasso zikiwa Dunia ya kwanza.

Tanzania ifanye nini kufaidika na AU

Miaka 39 iliyopita viongozi wa Afrika walikutana huko Addis Ababa, Ethiopia na kuunda Umoja wa nchi Huru za Afrika.

Tarehe 9, Septemba 1999 tamko la Sirte lilianza kufanyiwa kazi ili hatimaye kuundwe Umoja wa Afrika (AU). Waraka wa madhumuni na ushirikishwaji wa nchi za Afrika katika uanzishwaji wa AU ulikubalika rasmi huko huko Sirte mnamo Machi 2001 katika kikao maalum ambacho pamoja na mambo mengine kiliamua kuwa kazi itakwisha pale theluthi mbili ya nchi za Kiafrika zitakaposaini kukubali kuanzishwa kwa umoja huo.

Afrika Kusini na Nigeria zinazokubalika kama nchi viongozi Afrika zilisaini Azimio hilo Aprili 23 na 28 mwaka huo huo na hivyo kufanya nchi zilizosaini kuwa 36 na hivyo kutimiza theluthi mbili iliyokuwa ikihitajika kuundwa kwa AU rasmi. AU inasemekana kisheria ilianza toka tarehe Nigeria walipoanguka saini katika mkataba huo.

Pamoja na maneno mengi yanayosemwa kama vile huu ni mvinyo mpya katika chupa ya zamani ukweli unabakia pale pale kuwa hili ni wazo na ni hatua ambayo wakati wake umefika.

Ndoto kuu ya kina Nyerere, Nkrumah, Kenyatta, Haile Sellasie na wengineo ilikuwa ni ile ya kuiona siku ambayo Afrika itatamka bayana kuwa inadhamiria kuungana na ili tuungane tutafanya moja, mbili, tatu.

Kama ni wazo ambalo wakati umefika kinachobakia sio tena kujadili kufaa au kutokufaa kwake bali kuweka mikakati ambayo kwayo nchi moja moja zitanufaika na kwa upande mwingine bara zima litanufaika kwayo.

Ili tuliweke hili katika mwanga utakaotusaidia kupata hoja za nini Tanzania ifanye ili inufaike na kuanzishwa kwa Umoja wa Afrika ni muhimu kupitia madhumuni ya OAU kwanza, kisha yale ya AU.

Madhumuni ya OAU
Madhumuni ya OAU yalikuwa kwanza, kuendeleza umoja na ushirikiano kati ya nchi za Kiafrika. Kazi hii imefanyika kwa kiasi fulani lakini bado kazi iliyobaki ni kubwa zaidi na ndio maana kuna umuhimu wa kuwa na AU.

Kuratibu na kuimarisha ushirikiano kati ya nchi za Kiafrika ili kupiga vita umaskini na udhaifu wa kiuchumi wa nchi za Afrika. Kazi hii bado kabisa haijafanyika. Afrika bado iko nyuma kiuchumi na ni jalala la bidhaa toka mabara mengine.

Kulinda utaifa, mipaka na uhuru wa nchi za Kiafrika. Kwa kuwa mkoloni hajarudi tena kisiasa tunaweza kusema kazi hii ilifanikiwa. Lakini mkoloni huyo kawahadaa Waafrika karudi kiuchumi na isitoshe hata wasiokuwa wakoloni katika bara la Afrika kama vile Japan sasa wanaitawala Afrika kiuchumi.

Ulinzi; huu pia umetafsiriwa vibaya kiasi cha kuruhusu madikteta kuwaburuza watu wao na OAU kushindwa kukemea vitendo vilivyochangia ukiukwaji wa haki za binadamu na kuongezeka umaskini katika nchi kadhaa za Kiafrika.

Kufutilia mbali ukoloni Afrika. Hili limefanikiwa kwa asilimia 98 na pindi Morocco ikiiachia Sahara itakuwa ni asilimia 100.

Kuendeleza ushirikiano wa kimataifa. Hili limefanikiwa sana maana kila nchi Afrika inategemea nchi moja au mbili au zaidi za nje. Lakini ushirikiano huo wa kimataifa katika ngazi ya nchi za Kiafrika kwa Kiafrika bado ni mchanga ukilinganisha na uhusiano wa nchi hizo na nchi zilizoko nje ya bara lenyewe.

Madhumuni ya AU
Madhumuni ya AU kama nilivyoyaelewa ni kama ifuatavyo:
• Kufanikisha umoja na ushirikiano mkubwa zaidi kati ya nchi za Kiafrika na watu wa Afrika;
• Kulinda utaifa, mipaka na uhuru wa nchi wanachama;
• Kuharakisha kasi ya umoja wa kisiasa na kiuchumi wa Afrika;
• Kuendeleza na kulinda kwa pamoja yale yote yenye maslahi kwa bara hili na watu wake;
• Kupigia debe ushirikiano wa kimataifa kwa kuzingatia Azimio la Umoja wa Mataifa na Tamko la haki za binadamu la Umoja wa Mataifa;
• Kuendeleza amani, ulinzi na utulivu katika bara hili;
• Kuendeleza misingi na taasisi za kidemokrasia, ushirikishwaji umma na utawala bora;
• Kuendeleza na kudumisha haki za binadamu na haki za watu kulingana na Tamko la Afrika juu ya haki za Binadamu na watu na taasisi zinazohusika;
• Kuweka mazingira muafaka yatakayowezesha bara hili kushika nafasi yake stahilivu katika shughuli za kiuchumi za dunia na mapatano ya kimataifa;
• Kupigia debe shughuli–endelevu katika nyanja za kiuchumi, kijamii na kiutamaduni ikiwa ni pamoja na kujenga uchumi mmoja kwa Afrika;
• Kuendeleza ushirikiano katika nyanja zote za maisha ya wananchi ili kuinua hali ya maisha ya Waafrika;
• Kuratibu na kusawazisha sera zilizopo kati ya maeneo mbalimbali yaliyopo hivi sasa na yatakayoanzishwa ili kurahisisha kufikiwa kwa malengo ya Umoja wa Afrika;
• Kusukuma mbele maendeleo ya bara hili kwa kuendeleza utafiti katika nyanja mbalimbali na hasa sayansi na teknolojia; na
• Kushirikiana na mapatna wa kimataifa mbalimbali wanaostahili ili kufuta kabisa magonjwa yanayofutika na kuwa na huduma bora za afya barani humu.
Sidhani kama kuna Mwafrika atakayekataa kuwa haya sio malengo yake. Kama ndivyo sasa tuone Tanzania tunahitajika kufanya nini ili fursa zinazotokana na AU ziwe zetu zote.

Tanzania ifanye nini?
Kwanza, tusipoteze muda kuwa na Katiba mpya itakayozingatia matarajio ya Watanzania na matakwa ya AU.

Serikali ya Tanzania ijitoe kwa hali na mali kuendeleza Kiswahili ili kishike nafasi yake ya kimataifa na vile vile kurahisisha Umoja wa nchi za Afrika Mashariki na Kati.

Serikali ifute sheria ya kuvizuia vyombo vya habari kutangaza kwa zaidi ya asilimia 25 ya nchi na vyombo hivyo visaidiwe ikiwezekana ili visikike Afrika nzima. Vyombo hivyo ni pamoja na redio, televisheni na magazeti yanayotoka kwenye mtandao.

Kituo cha uwekezaji Tanzania (IPC) kisiwe kwa ajili ya watu wanaowekeza tu Tanzania bali pia kiwe na kitengo cha kuwasaidia Watanzania wanaotaka kuwekeza nje ya nchi. Iwe Kenya, Uganda, Msumbiji au hata Ulaya.

Kazi kubwa ya serikali na hasa Balozi zetu za nje iwe ni kusaidia tuwe na miguu ya kiuchumi ndani ya nchi mbalimbali zinazotuzunguka. Wenzetu wa Nigeria wamefanikiwa sana katika hili twendeni tukajifunze kwao.

Kuzisaidia nchi zinazotuzunguka kwa kuwapa walimu, manesi, madaktari, na wafanyakazi au wataalam wengine wanaowahitaji. Kusaidia kuendeleza na kupanua shule za msingi, vyuo na vyuo vikuu ili viweze kupokea wanafunzi toka nje ya mipaka yetu.

Kiingereza, Kiarabu, Kifaransa na Kiswahili yawe masomo ya lazima sekondari na kwa baadhi ya shule za msingi. Hii itawasaidia vijana wa Kitanzania kupata kazi katika shirika lolote la AU bila mikwara.

Tanzania ikubali kuwapokea wageni; wawe Waafrika au wasio Waafrika wenye vipaji au ufundi tusio nao sisi kuja kufanya kazi na ikiwezekana kuwa raia wa Tanzania katika kipindi kifupi tu endapo wanataka wenyewe.

Kuikumbatia na kuieneza teknolojia ya habari na mawasiliano hadi kufikia ngazi za mitaani na vijijini katika muda mfupi kuliko nchi nyinigine yoyote ya Kiafrika ili tuwe na wataalamu wa kwenda kufanya kazi nchi nyingine na kutuingizia mapato kiulaini.

Kuigeuza Tanzania kama soko la Kimataifa kwa eneo hili la Afrika ili kuondoa uwezekano wa nchi yetu kumezwa kabisa kiuchumi na Afrika Kusini.

Kwa kuagiza bidhaa toka Indonesia, Thailand, Taiwan, Korea Kusini, Malaysia kwa bei rahisi na kisha kuziuza tena nje ya mipaka yetu kwa bei nzuri kama Nigeria inavyofanya itatuhakikishia mapato yatakayochangia kufufua uwezo wetu wa kuzalisha baadhi ya bidhaa nchini mwetu.

Askari walipwe mishahara mizuri ili kuhakikisha wanafanya kazi yao ya usalama wa raia na mali zao ili tuwe mfano wa kuigwa na nchi nyingine na askari wetu kupata ajira nje kutokana na rekodi yao nzuri.

Mikakati ya ujenzi na ukarabati wa barabara iwe endelevu na isiyokwama mahala na wakati wowote ili shughuli za uchumi zizunguke saa ishirini na nne bila kusimama.

Maji, umeme na huduma mbalimbali za jamii isiwe kero tena nchini. Vipatikane kama vile hewa tunayopewa bure na Mwenyezi Mungu.

Tuwalipe madaktari na manesi uzuri ili wafanye maajabu. Tuwe na teknolojia ya wakati huu katika mahospitali ili tusilazimike kupeleka wagonjwa wetu nje ya nchi.

Nchi hii ijitosheleze kwa chakula, mavazi na makazi ili kuwapa watu wote heshima na staha wanayostahili.

Magereza yetu yawe na utu na ubinadamu pamoja na kuwa vyuo vya kurekebisha tabia na sio vyuo vya kuozesha tabia.

Kosa kubwa linaloweza kufanywa na Tanzania ni kubakia au kuendelea kuwa mwanachama wa jumuiya hiyo kama: itakuwa ni kilabu ya kulindana viongozi; itapata viongozi wababaishaji na wasioisogeza hata hatua moja Afrika kuelekea kuungana; itawavumilia viongozi wanaowaua watu wao kwa sababu ya tamaa ya kubaki madarakani; au itakuwa na viongozi ambao dhahiri bin shayiri ni madikteta na watu wasiokubali wala kuipenda wala kuitaka demokrasia kwa lolote lile.


Leo AU wakati wowote kuliko huko nyuma inaonekana ni klabu iliyoundwa na viongozi wa Afrika ili kulindana wenyewe kwa wenyewe. Dhana ya kuingiliwa mambo ya ndani ni dhana iliyopitwa na wakati. Dhana hii haina tofauti na baba mlevi ambaye kashika panga na shoka ndani ya nyumba yake akitaka kumkatakata mkewe na wanawe na dirisha la kioo linaonesha wazi haya, halafu eti majirani waseme si ruhusa kwao kuingilia mambo ya ndani ya baba mlevi huyu wa pombe au madaraka au uanaume wake!

Uhalifu na mfumo wa kijamii-uchumi

Tuanze na mchapo. Huko Uganda walimu wa shule za msingi siku moja walijikuta wanafanya mitihani ile ile waliyokuwa wakiwapa wanafunzi wao. Wengi wao walifeli. Serikali ikawafukuza kazi.

Huko huko Uganda mamia ya askari polisi wanaodaiwa awali walikuwa walevi hivi sasa wanapigishwa kwata la nguvu. Atakayeshindwa mazoezi hayo, yakiwemo, kukimbia, kubeba mizigo mizito na kadhalika atakuwa kajifukuzisha kazi.

Na huko Uganda tena, hivi sasa bila angalau digrii moja sahau kuwa mwandishi wa habari maisha.

Wenzetu wamecharuka. Wanataka kama mtu ameajiriwa kwa kazi fulani basi kweli si tu aagizwe ifanyike lakini aonekane akiifanya kazi hiyo.
Nchi haiwezi kuwa na maendeleo ya kweli, Waganda wanaamini, kama una wababaishaji sehemu za kazi muhimu na sio wachapa kazi.

Katika mtiririko wa haya yote Waganda wanayoyafanya inaelekea wana mkakati fulani wa kuijenga jamii yao iwe imara kiuchumi na kijamii.

Kwanini ujambazi unakuwa tishio?
Tuache utani. Ujambazi sasa ni tishio kwa biashara na makampuni nchini. Kila mtunza-fedha au mbebaji fedha wa kampuni au taasisi nyingine daima yuko katika hofu ya kutolewa roho.

Hvi leo jamaa hawa wanaweza wakaibukia sehemu yoyote wakafanya vitu vyao na wakaondoka na asitokee polisi yeyote kwa kitambo kiasi. Katika hali kama hii kila mtu anajiona ni yeye na lwake. Wakati kila raia ameanza kupoteza imani kabisa na jeshi lao la polisi.

Kwa kifupi watu wamekata tamaa na wanaamini kuwa unaweza kushambuliwa wakati wowote na usipate msaada. Na hii ndio sababu ya ujambazi kuwa sasa ni tishio la kitaifa linalochipukia.

Hata hivyo, wanasiasa bado wamekaa kimya na hakuna anayezungumzia jambo hili kwa uzito unaotakiwa. Pengine wakiamini kuwa unaweza kulifumbia macho nalo likapita. Lakini hili kwa nionavyo mimi sio jambo la kupita. Ni kitu tutakachokuwa nacho siku zote kama vile tutakavyokuwa na maskini siku zote.

Vita vinaweza kuliyumbisha taifa. Ujambazi ukikithiri hulisambaratisha taifa. Na ukitaka kuiona mifano nenda Somalia.

Kama ndivyo basi huu ni wakati wa viongozi nchini kujiuliza maswali mengi kadri iwezekanavyo ili kupata majibu sahihi na mikakati ya kuitumia ili kutafuta ufumbuzi wa tatizo hili.

Maswali ya kujiuliza
Ingawa mimi sio bingwa wa masuala ya sayansi ya jamii, hata hivyo, nina maswali kadhaa ya kuuliza ambayo natarajia yakipata majibu yatatupa mwanga juu ya tatizo linalotukabili.

Ni kwa kiasi gani mpito toka ujamaa kuingia siasa isiyo na jina (Ubepari usiotajwa) hapa nchini unachangia kuongezeka kwa wimbi la ujambazi wa kutumia silaha.

Wakati ule tunavaa Chou-en-lai inaelekea wote tulijiona kuwa ni sawa. Kwa malezi ya Baba wa Taifa kila mtoto alijiona hana tofauti na mtoto mwenzake. Na hili alilifanya kuanzia nyumbani kwake mwenyewe.

Hivi leo mtoto wa muuza samaki feri ambaye kuambulia elfu moja ni kazi akiwa rafiki wa mtoto wa mwanasiasa au meneja ambaye baba yake humpa laki moja atumie kwa siku! Ni binadamu gani ataacha kuwa na maswali ya kujiuliza na yeye afanye nini awe kama huyu wa pili? Hebu fikiri!

Achilia mbali watoto; leo wazazi wanashindana kwa wingi wa majumba, magari, nguo na kila aina ya vikorokoro. Wazazi wengine wanona ilhali wengine hawana uwezo na wanabaki kumezea mate na matumbo kuwanguruma. Watoto wao siku ya siku wanapofanya vitu vyao dhidi ya hao ‘wanaoringa’ mzazi atakataa nyumba mpya anayopewa? Mark II na dereva ikija nyumbani na kuambiwa ni yake aitumie jinsi anavyotaka? Mzazi atasema nini? Atamlaumu mwanae? Amelogwa? Achekwe?

Katika hali tuliyo nayo sasa baadhi ya wazazi wanaowaona watoto wao ‘wezi’ kuwa ni kina Robbin Hood wa miaka yetu. Kama humjui jamaa huyu basi nikuelezee kwa kifupi. Huyu alikuwa ni jambazi maarufu wa Kiingereza ambaye alikuwa anawaibia matajiri na kuwapa maskini. Unaona hiyo?

Fursa finyu
Katika miji yetu mbalimbali kumezuka ubia usio mtakatifu kati ya wanasiasa-wafanyabiashara na watumishi wa serikali kuwapora vijana mabanda ya biashara; viwanja vya michezo; tenda; vibali na kila aina ya fursa ambayo ingelimuwezesha kijana kujiendeshea maisha yake na pengine kutajirika bila kutumia njia haramu. Sasa tujiulize kama mtu ananyimwa fursa halali za kuukata afanye nini. Ashukuru. Atoe Allhamdullilahi kisha asahau?

Elimu bila kazi
Mamia ya vijana wanaomaliza shule ndani na nje ya nchi hivi sasa hawapati kazi. Ni nini kitakachotokea hapa. Tumewahi kujiuliza swali hili? Biblia inatuambia: ‘mikono isiyo na kazi, shetani ataitafutia kazi bila wasiwasi wowote!’

Watu waliosoma hawawezi kuwa sawa na vibaka. Hawa ni watu wenye akili eti. Wengine wamesomea udaktari wa mifugo; wengine wahandisi; wengine wanasayansi na kadhalika. Na ole wako wakikutana watu zaidi ya wawili kama hawa mambo wanayoweza kuyafanya ni ya ajabu. Tatizo ni pale ambapo wanachokifanya ni biashara ya uvunjaji sheria. Nani ataona ndani?

Sheria zinazopendelea
Vijana wa Kitanzania sio vipofu, sio viziwi. Wanaona kila siku, wanasikia kila kitu. Na aghalabu wanajua kuwa kuna seti mbili za sheria. Moja ni ile ya walalahoi, na nyingine ni ile ya vigogo na vizito. Mlalahoi ama ni kuvunjiwa vyombo vyake na kupoteza mtaji wake wa kimaskini au ni kulipa faini au ni kwenda jela. Sheria hiyo hiyo kwa upande wa vizito ni kuhakikisha mali yao inalindwa kwa jino na ukucha wa polisi wetu wenyewe; kutokulipa faini na kutokwenda jela hata wakifanya kosa gani.

Katika hali kama hii inafaa tuwaulize wanasayansi-jamii je watu na hasa vijana wenye wingi wa jazba na pupa ya maisha watalichulia hili suala namna gani. Ni vyema kufuata sheria na kunyanyasika hata pale wewe unapostahili kuwa ndiye mdhulumiwa au mtu aliyeonewa, au ni kuvunja sheria na kuhakikisha vyombo vya sheria havikubambi hata siku moja? Na wakikuzingira basi uchukue njia ya Mkwawa?

Hili linaendana na haki kununuliwa. Hivi sasa kwa sababu moja au nyingine mtu mwenye fedha au mwanasiasa anaweza akakukosea. Lakini badala ya wewe uliyekosewa kulipwa fidia ukajikuta wewe ndiye unayedaiwa kama sio kwenda lupango kabisa.

Katika kijiji ambacho sitaki kukitaja jina visa kama hivi vimetokea. Na watu wasiokuwa na hatia, na hasa vijana, labda kwa sababu ya kugombea mwanamke na kumshinda tajiri anajishtukia yuko ndani na kosa halijui. Hili linafanyika vijijini, ninaamini, karibu vyote Tanzania na sio hicho kimoja tu nilichotolea mfano wake.

Njaa na umaskini
Hapana haja ya kusema mengi kuhusu hili. Maana ni wazi kuwa kuna njaa na umaskini wa kutisha katika jeshi letu la polisi. Hatusemi wakimwagiwa fedha basi ujambazi utakwisha. La, hasha. Tuwaachie wanasayansi-jamii watupe majibu ya swali hili: je, mishahara midogo na umaskini wa polisi unachangia kwa kiasi gani matatizo ya usalama nchini? Na kwa kiasi gani hili linachangia haki ya mtu kuuzwa au kununuliwa?

Uharamia na ushindani
Pengine ni muhimu kwa wanasayansi-jamii kuuliza pia kama ushindani ambao ni matokeo ya soko huru nchini unaweza kusababisha uharamia wa kibiashara? Je, mfanyabiashara fulani anaweza kukodi majambazi ili wapore kutoka kwa mshindani wake na hivyo kumkomesha mwenzie? Au pale biashara au kampuni fulani zinapopewa upendeleo na mamlaka na wengine kutaka kujibu mapigo?

Je, watu wanaofukuzwa kazi ovyo katika makampuni na taasisi siku hizi wanaweza kutumbukiwa na nyongo na kuamua kula sahani moja na majambazi ili kuwakomesha waajiri wao?

Kisaikolojia hasa ni kitu gani kinachomfanya mtu kudiriki kutoa roho ya mwenzie na pengine mtu anayemjua kwa sababu ya shilingi millioni 10, 30 au hata 100?

Elimu, uwezo na vifaa vya polisi
Aidha katika hili ni muhimu kujiuliza kama elimu waliyo nayo polisi waliofaa kulinda usalama wakati wa siasa ya ujamaa kama inatosha kulinda usalama katika enzi za ubepari na ushindani?

Wananchi wengi wanaamini kuwa polisi wetu wana elimu duni na hawawezi kabisa kukabiliana na hali inayojitokeza sasa. Hawa, inadaiwa, ni watu waliofundishwa kutumia zaidi nguvu na sio akili. Kadhalika mbele ya mitandao kama ile ya simu za mikononi na kompyuta ni rahisi polisi wetu ‘kuchengenywa’ na wasijue chochote kinachoendelea. Maana ni polisi wangapi wenye simu za mkononi au wanaojua kutumia kompyuta?

Mfumo unaofaa
Ni dhahiri ujamaa ulikuwa una kasoro nyingi. Kadhalika ndivyo ilivyo kwa ubepari. Wenzetu katika nchi za Scandinavia walitambua hili miaka kadhaa iliyopita. Wao hawafuati ujamaa moja kwa moja, wala hawafuati ubepari kichwa na miguu. Wamebuni siasa inayoitwa ujamaa-wa-kidemokrasia.

Mfumo unaomruhusu kila mtu kutajirika kwa kadri ya uwezo wake, lakini wakati huo huo hauruhusu mtu kufa njaa au kukosa kabisa eti ili fulani tu atajirike. Huu ni wakati muafaka wa vyama vya siasa kupitia siasa za nchi hizo na kuona ni mazuri gani tunayoweza kuyaiga kama sehemu ya mapambano yetu ya muda mrefu dhidi ya uvunjaji sheria nchini mwetu.

Bila shaka majibu yoyote yatakayopatikana hapa yatalazimu kuibadili katiba ya nchi na vyama vyetu. Maana badala ya maneno ujamaa na kujitegemea lazima pawe na maneno yasemayo kuwa nchi yetu ni nchi inayofuata ujamaa-wa-kidemokrasia.(Ujaki) Kwani mfumo huu utawapiga jeki wasionacho! Aidha mfumo huu si mgeni hapa nchini; ulikuwepo Zanzibar enzi za marehemu Karume. Wakati Zanzibar ilipokuwa haina wizi, umalaya, madawa ya kulevya na uhalifu mwingine uliopo hivi sasa. Mwenzetu alijua anachokifanya, je sisi tunajua tunachokifanya?

Kila mwaka unapoisha tujiulize: Tumepanda, tunapalilia na tumevuna nini?

Mtu mmoja mmoja kwa ujumla wao ndio wanaounda taifa. Inapofikia mwisho wa mwaka inafaa kila mtu kujipima na kuona amefanikisha nini na ameshindwa nini katika kipindi cha mwaka mmoja uliopita.

Wengi wanaamini kuwa wamekuwa wakipiga ‘maktaimu’ kwa kipindi chote hicho na sababu kubwa ikiwa ni kuwa kipato hakilingani kabisa na mahitaji yao ya kimaendeleo na matumizi ya kawaida.

Hii haiondoi ukweli kuwa katika nchi hii bado kuna visiwa vya utajiri na kila siku iendayo kwa Mungu tunaona maghorofa yakisimamishwa, magari mapya yakinunuliwa, biashara mpya zikifanyika na ‘dili’ za mabilioni zikitangazwa.

Hata hivyo kwa Watanzania walio wengi mwaka 2002 ulikuwa mwaka wa mapambano ambayo hayakuweza kutoa washindi lakini kuna wengi waliokata tamaa na kushindwa.

Taifa linalotaka kuwa imara kiuchumi lazima lichunguze kwa makini kwanini hali kama hii inatokea. Haiwezekani kuona kuwa kuna maendeleo ya kiuchumi katika nchi lakini mifukoni mwa wananchi hamna kitu na wao wamebaki pale pale walipokuwa mwaka mmoja au miwili iliyopita.

Utasema nini juu ya hili? Mtu anatumia vibaya fedha yake? Mahitaji yake yameongezeka kupita uwezo wake au mfumo wa kuzawadiwa umepitwa na wakati?

Ukitaka kujua kwa undani maisha ya familia nyingi za Kitanzania ni zile zisizoweza kula nyama sembuse kuku au samaki wasioshikika bei mpaka sikukuu tu.

Kama sera ni kuzuia mzunguko wa fedha ili watu wajifunze kubana matumizi basi sera hiyo imegonga ukuta maana imefikia kikomo cha watu kufunga mikanda na sasa wanaona serikali yao haiwatakii mema.

Familia zilizokuwa na watoto wasiokwenda shule mwaka 1995 serikali ya awamu ya tatu ilipoingia madarakani hivi leo zina watoto wanaokwenda shule za msingi, walioko sekondari na wanaokaribia kuingia Chuo Kikuu.

Ukitazama mfumo wetu wa elimu kama ulivyo hata kama kuna madai ya kuwepo elimu ya bure hapa na pale bajeti kubwa ya Mtanzania katika miaka michache iliyopita imeishia kwenye elimu na nyumbani watu wanalazimika kula mchicha, kisamvu na ugali mchana na usiku.

Katika hali kama hii ni dhahiri kuwa japo watoto wanasoma lakini unyafuzi na utapiamlo unawanyemelea kwa kuwa wazazi wao wana kipato duni kulinganisha na mahitaji ya lishe kamili; hali hii haiwezi kuwaachia wafanye vizuri kamwe shuleni.

Huu ni wakati muafaka wa serikali kuu na serikali za mitaa kuangalia ni jinsi gani wanaweza wakamsaidia mtu mmoja mmoja na familia kuongeza kipato chake badala ya serikali zote kukaa mkao wa kucha na meno wa kutaka ima-fa-ima kumtoza mwananchi kodi hata kama hali yake ni taabani na mtu hawezi hata kuitosheleza familia yake.

Kwa kuwa macho yetu yameelekezwa kwa wageni kama wawekezaji tumesahau kabisa kuwa tunaweza kuwahamasisha wanamtaa wakawa na miradi inayochangia kuimarisha kipato chao na hivyo kupunguza makali ya maisha.

Ni dhahiri hili ni kama lilivyo kwa sababu wengi wetu na hasa tulioko serikalini tunataka kuvuna pale tusipopanda wakati tunashindwa hata kuwaandaa watu kulima, kupanda na kupalilia vyanzo mbalimbali vya kodi ya kesho na keshokutwa.

Kama ilivyo kwa mtaa ndivyo ilivyo kwa kijiji. Vijiji vingi vina uwezo wa kuwa na miradi inayoingiza fedha ikiwa ni ya mtu mmoja au makundi ya watu katika sekta tofauti kama vile maji, elimu, usafiri na uchukuzi, kilimo, biashara, utalii na kadhalika lakini kwa kuwa tumekamia kuvuna pale tusipopanda basi kuna serikali chache sana za vijiji zenye mpango wa kuimarisha uzalishaji mali kwanza kabla ya kuanza kutoza kodi. Kodi ambazo aghalabu huua hata zile shughuli chache za kiuchumi na kijamii zinazoanzishwa na wale wanaothubutu kufanya hivyo katika mazingira magumu ya nchi hii ambayo yamemsahau mwekezaji wa ndani kwa kumkumbatia mwekezaji wa nje.

Kodi ‘kichaa’
Kwa kukosa ubunifu Tanzania sasa hivi sio tu ina utitiri wa kodi zinazowachanganya wananchi lakini pia zina kodi kichaa. Kodi kichaa ni zile ambazo gharama ya kuzikusanya ni kubwa kuliko mapato yanayopatikana kutokana na chanzo husika. Kodi kichaa ni zile zinazoua miradi michanga au miradi ambayo ndiyo kwanza inaanza kubuniwa.

Kodi kichaa ni zile zinazomuonea mlipakodi mfanyakazi ambaye hana njia ya kuzikwepa maana ni ‘fixed and unavoidable’ lakini zinampa mwanya mfanyabiashara anayeingiza mara elfu au elfu kumi au milioni ya mfanyakazi huyo kukwepa kodi kubwa ambayo ingeliweza kuwa nafuu kwa mfanyakazi wa Tanzania.

Mfanyakazi huyo huyo akienda sokoni, dukani au kupata huduma yoyote ya kimaisha au ya kuanzisha mradi bado anakumbana na kodi nyingine nyingi kichaa ambazo aghalabu humfanya ajiulize hivi kweli-‘serikali hainiibii kumnufaisha mtu mwingine na ni nani huyo…?’

Maana kila akizunguka huku na huko haoni kazi iliyofanywa na kodi aliyokatwa. Na zile zinazofanyika zinafanyika nusu nusu tu.


Fedha zinaoza benki
Wakati huo huo, vyombo vya habari vinaruka na habari kuwa kuna mabilioni yamekaa benki kwa sababu hakuna wa kukopesha.

Hakuna wa kukopesha kwa sababu Benki yetu kuu haina utaratibu wa kumnyanyua mzawa kwa mikopo ya riba nafuu wala kuchangia kwenye miradi inayoweza kuajiri malaki ya vijana wa Kitanzania wasio na ajira leo.
Fedha zinaozea kwenye mabenki mengine yale ya ndani na ya nje kwa sababu yanataka kujiendesha kama benki zinavyoendeshwa huko Ulaya au Marekani na sio kama Benki ya Grameen huko Bangladesh.

Juu ya hayo benki zimekosa uongozi kupitia BOT unaoweza kupunguza hatari na hasara ya kukopesha kwa kuzifanya benki 5 au kumi kumkopesha mtu mmoja na hivyo kugawa ‘risk’ hiyo kwa wengi.

Kubwa zaidi ni kuwa mabenki yote kwa kiasi kikubwa bado hayajakaa mkao wa kusaidia Watanzania kuzalisha mali na kuongeza utajiri wa nchi kwa huduma na biashara ili mabenki na wananchi wote kwa pamoja wafaidike.

Tanzania ina kila kitu kwa hivi sasa cha kuifanya iwe nchi imara kiuchumi kama mabenki yatajigeuza kuwa vituo vya kuchochea uzalishaji mali, upanuzi wa biashara kimataifa na utoaji huduma za kimataifa katika sekta mbalimbali na hivyo kukuza uchumi wa nchi kwa kasi zaidi.

Hofu kuwa Watanzania ni wakopaji wazuri lakini wasiolipa haina msingi. Tatizo ni uaminifu wa watumishi wa benki wenyewe, elimu na maarifa ya kuutumia mkopo kwa upande wa wakopaji. Ipo mifano ya kutosha kuwa Watanzania wazawa wakielimishwa kuhusu kukopa na kuzalisha ili kulipa madeni yao wanaweza kuchangia kuujenga uchumi wa nchi hii kwa kiasi kikubwa.

Mzunguko wa fedha katika uchumi wowote ndio kielelezo cha ufanisi na usanifu ikiwa ni pamoja na tija ya nchi husika.

Mzunguko huo hivi sasa kwa Tanzania unakwaza kwa makusudi ili kuwafunza Watanzania thamani ya fedha. Lakini somo limeshasomwa na likirudiwa rudiwa tena tutawachosha wanafunzi. Hivi sasa watu hawazungumzii tena fedha kwa matumizi bali kwa uwekezaji. Ni wakati gani mzuri kama huu wa kuachia mzunguko ufanye kazi yake na wawekezaji wa ndani waanze kufanya vitu vyao.

Tulichopanda katika elimu ni majengo mazuri na vifaa vya kufundishia kuwepo kitu kilichokuwa hakipo huko nyuma.

Lakini ipo haja ya kuangalia ni jinsi gani tunaweza kupanda na kupalilia mapato, lishe na huduma bora kwa wahusika wenyewe yaani wanafunzi na walimu. Hatuwezi kuboresha elimu kama hatutaboresha kipato na mazingira ya kazi ya walimu.

Hatuwezi kuboresha elimu kama hatuwezi kuwasaidia wazazi kuingiza kipato cha kutosha ili watoto wao wale vizuri na hivyo kuwa na afya ya kuweza kumudu masomo darasani.

Katika afya madai ya baadhi ya watu ni kuwa nchi za Kiafrika ikiwemo Tanzania zinang’ang’ana na ukimwi tu na kusahau magonjwa mengine yanayoua maelfu kila mwezi kwa kuwa gonjwa la kwanza lina mfadhili anayetaka kuona dunia nzima ina maadili ya zinaa kama yenyewe na pili gonjwa hilo eti ni la wakubwa na ndio sababu ya kelele zote hizi.

Sijui ukweli uko wapi hapa. Kwangu mimi, hata hivyo, la muhimu ni kutoa kipaumbele kwa magonjwa mengine na kuachana na projekti za kitoto zinazowafaidisha walio kwenye miradi na sio waathirika iwe ni kwa malaria au magonjwa ya zinaa.

Zoezi la Ubinafsi-shaji, kuuza mali ya umma na mifuko minono ya akiba ya hili au lile nayo ni mambo mengine yaliyopandwa na kupaliliwa kwa misingi ya kunufaisha wakubwa zaidi na bila kuwajali wale wanaokatwa pesa zao. Tuuone ukweli huu na sio kuzika kichwa kwenye mchanga kama mbuni mwerevu.

Tanzania imeonyesha mapinduzi makubwa katika Habari, Teknolojia ya Habari na Mawasiliano na kinachotakiwa ni kwa viongozi wa serikali kubadilika na kwenda na wakati ili vitu hivi vitumike kuipa nchi nguvu ya kimataifa katika eneo hili la Kiafrika.

Tunaweza kutishwa na wawekezaji katika sekta nyingine lakini sio hii kama serikali itawasaidiwa wazawa barabara. Na kuwasaidia kwenyewe ni kuondoa kodi kichaa na sheria kichaa. Kodi na sheria zinazoua ari ya kukua na kupanua biashara hizo kwa faida ya nchi na wananchi.

Ushindani na ubepari unahitaji Watanzania wasifungwe fungwe na sheria zisizowafunga wawekezaji toka nje.

Hisia kuwa nchi inauzwa kwa wageni inatokana na ukweli kuwa sisi wenyewe tunadanganyana na tunapeana maneno mengi lakini vitendo daima hamna. Tubadilike na tuanze kupanda na kupalilia moyo wa kutaka kuona kila Mtanzania ananyanyuka na kufaidika na maendeleo ya kiuchumi kesho na keshokutwa.

Ubepari na hatma ya umaskini Afrika

‘Utajiri sio unachozalisha, bali unachobaki nacho!’-Nukuu

Hoja kuwa mali aliyonayo tajiri imetokana na jasho au akili zake mwenyewe ilichambuliwa na J. K.Nyerere vizuri na kwa undani kabisa na kilichodhihirika ni kuwa hakuna mtu mmoja hata awe na akili namna gani anayeweza kuwa na uwezo wa kujitajirisha mwenyewe bila kuinyonya jamii kwa njia moja au nyingine.

Katika medani ya kimataifa ukweli huu ni wazi zaidi. Nchi tajiri ni tajiri kwa sababu zinanunua malighafi kwa bei rahisi kutoka nchi maskini na kuwauzia maskini hao hao bidhaa zitokanazo na mali ghafi hizo kwa bei ghali zaidi.

Mishahara katika nchi maskini ni ya kitumwa wakati huko Ulaya mishahara ni mikubwa kutokana na tofauti za kipato kati ya nchi maskini na tajiri.

Kama ilivyo kati ya nchi maskini na nchi tajiri ndivyo ilivyo kati ya mtu tajiri na mtu maskini. Nchi maskini zinataka bei halali, wakati maskini wanataka malipo halali kama mishahara au kipato ili nao wawe na fursa ya kudunduliza na kujikwamua kutokana na umaskini siku moja.

Tunachokizungumza hapa ni kuwa kile kinachozalishwa nchini au duniani kisipogawanywa kwa haki basi tofauti kubwa kati ya maskini na tajiri huzuka. Jitihada zikifanywa kuhakikisha kuwa kinachozalishwa kinagawanywa kwa haki zaidi basi na umaskini nao unapungua kwa kiasi kikubwa.

Tunasema India kuna umaskini wa kutisha kwa sababu kina Bill Gates hawaruhusiwi kuchipua huko lakini umaskini wa India sio kukosekana kwa matajiri bali kukosekana kwa mgawanyo mzuri wa keki ya taifa.

Kweli binadamu ni mgumu kubadilika na nchi inatakiwa kujenga mazingira ya kuzalisha kina Bill Gates wengi kadri iwezekanavyo. Lakini kina Bill Gates hao watasaidia asilimia ndogo tu ya wananchi wa nchi husika kuwa nao matajiri pia.

Kwa Tanzania wawekezaji wanaweza kuchangia kiasi fulani vita vyetu dhidi ya umaskini lakini hili haliondoi ukweli kuwa mchango mkubwa wa kuondoa umaskini utatoka kwenye vyombo vyetu wenyewe vya fedha vikiongozwa na Benki Kuu. Vyombo hivi vikibweteka kama vilivyobweteka sasa katika harakati za kupunguza umaskini tusahau kabisa kuupunguza hata kwa miaka 300 ijayo.

Mtu binafsi ana ukomo wa maisha. Serikali au vyombo vya fedha havina ukomo wa maisha. Pakijengwa mfumo mzuri wa kiuchumi unaowajibika kuhakikisha pato la Taifa linagawiwa kwa namna ambayo saa zote majaribio ya kuwazalisha kina Bill Gates yanafanyika basi hili peke yake linaweza kuwa chachu inayotosha katika uzalishaji mali na kupambana na umaskini.

Vyombo na taasisi zifanyazo kazi
Tatizo letu Afrika iwe ni wakati tunafuata mfumo wa kijamaa au kibepari ni kuwa na vyombo visivyofanya kazi.

Na pale vyombo hivyo vilipofanya kazi vilifanya kazi hiyo kwa ajili ya waliokabidhiwa vyombo kujitajirisha wao wenyewe na familia zao; kuwatajirisha wageni; lakini sio kutajirisha nchi na watu wake.

Kampuni au shirika liwe katika mfumo wa ujamaa au ubepari kama likiendeshwa kwa namna ya mwenye mali kujinufaisha yeye mwenyewe bila kunufaisha wateja/wananchi bado tatizo linakuwa palepale.

Sio chombo kinachozalisha ili nchi itajirike bali kinazalisha kumtajirisha mtu mmoja au wachache potelea mbali kama nchi inapoteza kitu fulani kwa kufanya hivyo.

Mali inayozalishwa sio mali isiyohamishika. Na ili mradi wazalishaji wawe ni wananchi au wawekezaji toka nje wanahamisha mali hiyo na haikai hapa nchini ni muhali kuona jinsi gani tunaweza kuondokana na umaskini.

Biashara hapa itakuwa ni sawa na ya mchumia-tumbo, yaani, kwa hapa mwekezaji mwenyewe ndiye anayefaidika lakini nchi haipati lolote isipokuwa statistiki za uongo na kweli kuwa wawekezaji wameongezeka na uzalishaji mali umeongezeka.

Swali linakuwa baada ya mali na faida hiyo kuzalishwa imebaki nchini au imekwenda nje? Utajiri sio kile kinachozalishwa bali ni kile watu na nchi inachobaki nacho.

Utamaduni kama mizizi
Mti hustawi pale tu mizizi yake inaposhika ardhini. Uchumi wa nchi hauwezi kujengwa juu ya utamaduni au tabia za kigeni. Matajiri wanaozuka katika mazingira na utamaduni wa aina hiyo ni sawa na maua yanayochipua jangwani.

Umaskini Afrika kwa kiasi fulani unachangiwa na nchi nyingi kushindwa kudumisha utamaduni wake na kuutumia kama chambo cha kuvuta utajiri wa aina mbalimbali.

Mathalani, Tanzania, nchi inayosemekana kama mama wa Kiswahili imeshindwa kabisa kutumia lugha yake hiyo inayothaminiwa na kila mmoja Afrika kujinufaisha.

Mila na desturi za makabila mbalimbali Tanzania leo imekuwa ni kitu cha kuonea aibu na sio fahari. Kwa mantiki hii mila na desturi hizo; kutoweka kwake kunachangia umaskini zaidi kwa nchi kukosa asili wala fasili.

Nchi nyingi za Kiafrika tofauti na Uchina au India zimeshindwa kutumia mitishamba yao kujinufaisha kwa sababu walioko katika sekta ya afya tayari wamenunuliwa na makampuni na wafanyabiashara wa madawa ya Kizungu. Na wanaona bora kukubali dawa feki kuliko kuboresha dawa zetu asilia.

Michezo kama nyenzo ya utamaduni imara imeachwa kama yatima na matokeo yake leo Tanzania ni kichekesho karibu katika kila aina ya mchezo. Tukumbuke wakati sisi ni kichekesho majirani zetu leo wanatajirika na kuneemeka kutokana na hiyo hiyo michezo.

Kwa hiyo utamaduni wa uongozi dhaifu unaotegemea fadhila na huruma ya wafanyabiashara umejenga nchi kujidhalilisha na kujiuza kwa bei rahisi kwa yeyote yule anayetaka kutukaanga kwa mafuta yetu wenyewe.

Kwa kukubali tamaduni za wengine kichwa-na-miguu tumejiweka mahala pabaya ambapo hatuna msingi wa kujengea mtaji, teknolojia na utajiri wetu wa asili.

Japan, China, Uarabuni, Korea Kusini, Malaysia tofauti na nchi za Marekani ya Kusini kwa kutokubali utamaduni wao kuchafuliwa mno na wageni wamejenga aina ya uchumi ambao sio rahisi kushindwa kufanya kazi labda pale dunia nzima inapokuwa kwenye matatizo makubwa.

Hili ndilo linalotokea Afrika Kusini pia ambako Wazungu wa huko wamekubaliana na Waafrika kuunda taifa lenye utamaduni tofauti na ule wa Magharibi au wa kuiga.

Na siri yao wote hawa ni kuwa wananchi na viongozi wanakumbatia na kuenzi utamaduni wao. Hapa kwetu viongozi wetu kama Yuda Iskarioti wanaukana utamaduni wao.

Hivi sasa wamezuka manabii wa kisiasa na kadhalika wanaotaka ghafla bin vuu tuusahau utamaduni wetu na kukubali kukumbatia yale wazungu wanayotaka tuyakubali eti kwa faida yetu wenyewe.

Dawa ya umaskini wetu pamoja na mambo mengine ni kutafuta yote mazuri yaliyokuwepo katika utamaduni wetu na kuyarejesha upya kwa faida ya kizazi hiki na vizazi vijavyo.

Tusipofanya hivyo kama wana Israel tutaendelea kutangatanga nyikani kwa miaka 40 kama sio zaidi. Wataalamu wanasema kwa uhakika ni miaka 166. Utamaduni wa uzalishaji mali kwa njia bora zaidi na zenye usanifu, ufanisi na tija zaidi bado ni mgeni kwa Waafrika.

Ukiangalia kwa undani, hata hivyo, utakuta tatizo sio kitu kingine ila elimu. Elimu inayotolewa hivi sasa ni ile isiyochangia moja kwa moja kwenye shughuli za kibiashara au uzalishaji mali.

Katika dunia hii ya ushindani na kama kweli tunataka kuusogeza nyuma umaskini hatuna muda wa kupoteza kusoma vitu visivyo na maana katika maisha yetu ya kila siku.

Hii ni dunia ya kusoma na kuelewa menejimenti, masuala ya fedha, uchumi, biashara, masoko, teknolojia, uzalishaji mali, uhasibu na staid-kazi na taaluma nyingine ambazo moja kwa moja zitachangia kuuondoa umaskini wa mtu binafsi na nchi kadhalika.

Masomo hayo yakifundishwa kwa lugha ya Kiswahili ndiyo itakuwa mteremko kabisa kuupunguza umaskini kwa asilimia kubwa tu.

Katika kufanikisha hili lazima tuwe na utawala bora kuanzia ngazi ya mtaa hadi taifa. Na uongozi bora kwangu mimi ni uongozi usioingia madarakani kwa nia ya kujitajirisha wao wenyewe bali kuwatajirisha wananchi kwa ujumla wao. Tumeona wangapi waliojitajirisha wenyewe kama viongozi wamekuja na kuondoka lakini nchi wameiacha katika umaskini ule ule? Na wao wenyewe wala hawakwenda na utajiri huo wala kuacha sifa yoyote ya maana ya kusaidia watu wao kupambana na umaskini.

Pamoja na haya yote tukubali kuwa ubepari umeingia nchini, Afrika. Lakini je, tuufuate kama unavyoendeshwa huko Ulaya na Marekani. Au Waafrika wanaweza wakawa na mfumo wa kisiasa na kiuchumi unaoitwa ubepari-wa-kijamaa?

Mfumo unaotoa fursa sawa kwa wote kujitajirisha lakini wakati huo huo unawalinda watu wetu wasiadhirike kama wazungu maskini wanavyoadhirika huko kwao?

Hatima ya umaskini Afrika kamwe haiwezi kuamuliwa kwa misaada au ushauri wa wageni. Hatima yetu itaamuliwa na siasa zetu wenyewe humu ndani, siasa zitakazokataa ubinafsi, ubadhirifu na ulafi ili wote tuweze kuwa na maisha bora.